Ni kipi kipindi bora cha asubuhi kwenye radio?

PB is the best. Combo moja matata Sana la barbara H na Kipanya , siza na sasali na Bonge ila Fredwaa nadhani wangempumzisha. Huwa anaharibu chemistry.

Zamani Kipanya na Fina walinoga zaidi na Hando.

Kwenye TV clouds barbie na PJ wamebond vizuri sana asubuhi halafu content ya kushiba. Hongera kwa Director and producer na watu wote behind the scene maana Bila hawa tusingepata kilicho bora.

Swali fikirishi mbona tv za kenya kama Citizen,Ktn,ntv asubuhi zina content nzuri yaani interview kuliko za bongo. Mfano sasahivi sintofahamu angeletwa waziri wa habari atueleze hali ya mweshimiwa akapigwa maswali lakini waandishi wetu hawaendi na uhalisia.
 
BC ll,Hizo redio ulizo zitaja ziko kwa ajili ya mihemeko kwanza makelele mengi yani hamnakitu hapoo mauthui ya na fanana na ujanja janja mwingi..
Hakuna redio zenye mpangilio mzuri kama hizi vipindi vya subuhi REDIO FREE AFRICA, TBC FM, REDIO ONE hawa ndio wanajua maana na maudhui ya kukupasha habari.

umemaliza kila kitu mkuu.
Yaani fredwaa anakuwaga kama anajishtukia Fulani hivi yuko hewani hewani. Chemistry ilikataa kabisa kuungana na wenzake labda angepewa pindi jingine
 
PB is the best. Combo moja matata Sana la barbara H na Kipanya , size na sasali na Binge ila Fredwaa nadhani wangempumzisha. Huwa anaharibu chemistry.

Zamani Kipanya na Fina walinoga zaidi na Hando.

Kwenye TV clouds barbie na PJ wamebond vizuri sana asubuhi halafu content ya kushiba. Hongera kwa Director and producer na watu wote behind the scene maana Bila hawa tusingepata kilicho bora.

Swali fikirishi mbona tv za kenya kama Citizen,Ktn,ntv asubuhi zina content nzuri yaani interview kuliko za bongo. Mvano sass hivi sintofahamu angeletwa waziri wa habari atueleze hali ya mweshimiwa akapigwa maswali lakini waandishi wetu hawaendi na uhalisia.

hata vipindi vyao katika tv ni vizuri kuliko vipindi vya tv tanzania. redio zao wanavipindi vizuri kuliko tz kenya wapo vizuri
 
Naendelea kuhesabu kura.

ila kule mgahawa hawapo serious...sio rahisi mtu kumsikiliza Baba levo...na ile sala yao ya jioni huwa naonaga kama mambo ya ajabu tu..anyway, ni ubunifu wao ila kwa kipindi cha jioni zamani nilikuwa shabiki wa JAHAZI enzi za Kibonde ila now nimehamia UBAONI ya EFM.
Daah kama Mimi..Ubaoni ndo kila kitu,Imma Kapanga,Roman Shirima na Mpoki,,Traffic Jam siielewi
 
Timu ya breakfast ikiongozwa na Kipanya , Fina.
Walikuwa na miadi ya kuhoji baloz wa Denmark hapa nchini ktk ofisi yake.

Kuna vitu flani flani walienda kuhoji.

Jamana mwenye kuongezea aje asimulie hahaha

Kulitokea sintofaham yale mahojiano hayakwenda hewani.

Nadhani walitibuana baina ya KP na Uongozi wa Clouds media

Kp akafukuzwa kazi.

Lakini baaaaaaaaaaaadaye
Walimrudisha.

Ndo maana Masoud Kipanya kapunguza utu mbad
Nahisi walimuomba msamaha ndo maana akarudi

Ukiwa na uwezo wa kazi utafuatwa tu! alipoondoka Masoud Clouds kwenye PB walipwaya sana

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Hizo redio ulizo zitaja ziko kwa ajili ya mihemeko kwanza makelele mengi yani hamnakitu hapoo mauthui ya na fanana na ujanja janja mwingi..
Hakuna redio zenye mpangilio mzuri kama hizi vipindi vya subuhi REDIO FREE AFRICA, TBC FM, REDIO ONE hawa ndio wanajua maana na maudhui ya kukupasha habari.
Kwa PB bado hujanishawishi, akina Kipanya wako gado sanaa.
 
PB imejipambanua vizuri kabisa, kila mmoja ana role yake na anaimudu vizuri. Barbara ni Host mzuri kabisa, KP & Cza ni wachambuzi wanaochambua mambo kwa kina.

Sam anamudu vizuri usomaji wa magazeti kwa mtindo wa kipekee unaovutia masikio ya msikilizaji.

Bonge naye nafasi yake anaimudu vizuri jambo ambalo wanajikuta wanatengeneza timu moja hatari sana yaani akikosekana mmoja unaona kabisa kuna pengo.

Napenda sana pia segments zao zimepangiliwa vizuri sana ingawa huwa navutiwa zaidi na magazeti kutokana na namna Sam, KP na Cza wanavyoungana kuchambua mambo.

Huwa sifurahii kipindi Fredwaa akiwepo, sielewagi position yake pale CMG. Ila kwangu PB ya Clouds FM ipo juu sana na haina mpinzani kwenye shows za asubuhi kwenye redio za Tanzania.
Well said mkuu... Vipi kipindi cha Leo tena? Huwa wananivutia sanaa, hasa kipindi akiwepo yule Musa kama sikosei kwenye ile timu yao.
 
Hizo redio ulizo zitaja ziko kwa ajili ya mihemeko kwanza makelele mengi yani hamnakitu hapoo mauthui ya na fanana na ujanja janja mwingi..
Hakuna redio zenye mpangilio mzuri kama hizi vipindi vya subuhi REDIO FREE AFRICA, TBC FM, REDIO ONE hawa ndio wanajua maana na maudhui ya kukupasha habari.
Hakuna kitu kama hicho kwa sababu zifuatazo:-
1: Ifahamike kwamba kuna tofauti kubwa programe za asubuhi na jioni, MF kipindi cha asbh cha Radio 1 kilifaa kuwa jioni kwani wao wanaongelea mada zaidi na ndiyo maana wachangiaji wa simu ni wengi kwani jioni ni muda ambao watu wametoka kazini, wamepumzika nk. Tofauti na asubuhi ambapo Mara nyingi ni muda ambao hakuna mtu mwenye muda wa kupiga simu, ila ni muda ambao mtu anahitaji kupata habari na mambo yaliyojiri kwa wakati huo (Current story) na ndicho wanakifanya PB (Hongera kwao kwa ubunifu huo?

2: Utangazaji wa sasa ni modern si kama zamani, yaani media zinatakiwa kuwa na watu wenye ubunifu na zaidi ufahamu wa kuchambua mambo nyeti kulingana na nyakati, , , , kama utakumbuka ndani ya PB zamani kulikuwa na Segment inaitwa Jicho la Ng'ombe ilikuwa inaonesha ukosowaji wa moja kwa moja kwa njia ya mafumbo kwa serikali ila waliishtia na kuifuta hiyo segment, baadaye wakaleta kitu kinaitwa Kuperuzi na Kudadisi(Kwa sasa ni Kudonoa na Kudadisi) baada ya serikali kukataza media kusoma story kwenye magazeti na badala yake ikawa ni Headlines tu, wakamleta Sasali kwa kazi hiyo na bilashaka anaifanya vema kuliko PJ alivokuwa akifanya hapo kabla.

3: Kwa idadi ya watu kwenye vipindi hasa asbh na jioni karibu media zote kwa sasa ziko sawa kwani ni ngumu kipindi cha Massa 3/4 afanye mtu mmoja au wawili, ukweli ni kwamba Audience wanahitaji ladha tofauti masikioni, , , , hapo media zote ziko sawa.

4; Mwisho ni kwamba utangazaji siyo kuongea tu kwenye Mic, Bali uwezo wa kufikiri, kuchambua, ku- challenge nk, , , Nisem Clouds wamejitahidi kwa hilo ingawa Radio 1, E FM na Wasafi wanawatangazi wazuri lkn huwezi walinganisha uwezo wao na Kipanya, Cza, au Sasali, , , ,

Kama huyu Kitenge wakati yupo IPP alikuwa na akili lkn tangu aende Wasafi anaropoka ropoka tu studio na mwenzake Zembwela utadhani wanapita mtaroni wakati naye akiwa East Africa alikuwa timamu, Na huyu Mwaipaya sijui nani ndo hata hana kitu wao asbh asbh simu na mada za Ndoa kila siku kama vile wahubiri wakati kuna mambo nyeti ya kuzungumzia.

Sasa hawa niliowataja utaweza kulinhanisha uwezo wao na Kipanya, Cza au Sasali?
Yaani fikiria Kitenge, Zembela au Mwaipaya afanye Interview na Prof Lipumba, Zitto, Lissu, Majaliwa (wataishia kucheka tu)

Kwangu PB ni Bora zaidi!
 
PB n kipindi boraa ,siza, kipanya,Barbra,na kwenye magazeti Sam, wamejipangaa sana,ilaa hawa efm n 0 kwanzaa hawapeani muda wakuongea kila mtu anaropoka kivyakee,good morning wana watu wazuri ila wajipange zaidii
True ila kipindi kile yupo gerald hando na pemben paul james pj na barbara hassan na ciza aisee kipindi kilikuwa hot sana masudi naona anapooza sana
 
Naendelea kuhesabu kura.

ila kule mgahawa hawapo serious...sio rahisi mtu kumsikiliza Baba levo...na ile sala yao ya jioni huwa naonaga kama mambo ya ajabu tu..anyway, ni ubunifu wao ila kwa kipindi cha jioni zamani nilikuwa shabiki wa JAHAZI enzi za Kibonde ila now nimehamia UBAONI ya EFM.
Sala ipi mkuu maana mi sijawahi kusikia kipind hicho ni sala ipi?
 
Power Breakfast

Ila mimi nilikuwaga nafuatilia kipindi kile cha Barbara Hassan, Gerald Hando na PJ sijui kama hadi leo bado wanasemaga hivyo
Hapa hata mimi niliwakubari kinoma walifit kisawasawa, masudi mi naona kapooza sana
 
Back
Top Bottom