WanaJF habari zenu!...
Kuna kitu kidogo kinanisumbua, hivi kwa mtu ambaye ameoa 'out of love'..
Yaani amemuoa mtu asiyempenda ana haki ya kuwa na mpenzi nje ya ndoa ambaye he/she truly loves?
Unajua Avatar mi sioni tabu hapo katika kupenda,
ni haki ya kila mmoja kupenda, ila sasa unampenda nani?
hilo ndo la kujiuliza.
Huu uzi wako unanikumbusha issue moja hapo zamani,
kuna bwana mmoja aliwahi kuhoji kuwa hivi kupenda kuna fadhila kweli?
Yaani inatokea kuwa wawili wapendanao katika safari yao ya mapenzi,
mmoja anakuja kujitoa, lakini katika hiyo safari yao huyo aliejitoa alikuwa,
kwa namna moja amesaidiwa sana katika kuendelezwa kimaisha,
labda amesaidiwa sana kifedha, kielimu n.k.
sasa mwisho wa siku anajitoa na kujikuta anapendana na mtu mwingine,
Na muda mchache tu baada ya kufahamiana wanajikuta wanafunga na ndoa kabisa.
Sasa ndo linakuja swali hapo, kwani mapenzi/kupenda kunaendana na fadhila?
''Eti kwakuwa tulivyokuwa mapenzini nilikusaidia a, b, c, na d,
sasa mbona huna hata fadhila, yaani umeniacha na kwenda kumuoa/kuolewa,
na mtu mwingine...lol....''
Asanteni wapendwa!!!!!mbarikiwe nyote...