Ni haki kumwabudu marehemu?

Ni haki kumwabudu marehemu?

Albosignathus

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2013
Posts
4,898
Reaction score
1,051
Wana JF.Hili swala la kumwabudu marehemu au kumwombea wakati yeye kashakufa na hana ufahamu wowote kweli ni jambo jema? Maiti haijui wala haisikii nijuavyo mimi sijui wenzangu mnajuaje?

Maiti haina thamani yoyote hata fungu la mchicha la mia mbili inaizidi thamani nijuavyo mimi. Naombeni na nyie mawazo yenu kuhusu hili watu wa jf.
 
Fungu la mchicha..........!!!!??.....
 
labda nikuulize ni haki kuenzi fikra na busara za nyerere? kama ni haki,kwan tusimuombee huko alipo kwa mema aliyotuachia?
 
labda nikuulize ni haki kuenzi fikra na busara za nyerere?kama ni haki,kwan tusimuombee huko alipo kwa mema aliyotuachia?

Kuenzi fikra na busara hiyo ni sawa.Lakini kumuombea huko aliko si sawa kwa maana yuko chini ya ardhi na analiwa na wadudu.
 
Wana JF.Hili swala la kumwabudu marehemu au kumwombea wakati yeye kashakufa na hana ufahamu wowote kweli ni jambo jema? Maiti haijui wala haisikii nijuavyo mimi sijui wenzangu mnajuaje? Maiti haina thamani yoyote hata fungu la mchicha la mia mbili inaizidi thamani nijuavyo mimi.Naombeni na nyie mawazo yenu kuhusu hili watu wa jf.

Naomba twende kwa mfano ili tuelewane.
Maiti ya mama yako na mchicha wa 2000, kipi unadhani ni bora kitupwe jalalani kiliwe na mbwa?!
 
kuabudu sio haki. ni maamuzi binafsi, ndio maana unaweza kutoabudu chochote au yeyote. pia kuombea na kuabudu ni mambo mawili tofauti.
kwa mtazamo wangu haina maana sana kwa kua maiti ni sehemu ya tuchokipata kutokea kwene dunia hii na kuzika ni part ya kukirudisha so kuombea maiti...ni kupoteza mda......

kitokacho kwa Mungu ndio kinarudi kuhukumiwa na hukumu inatokana na namna mtu alivotumia mda wake duniani kufanya mema au mabaya...cdhani kama maombi yanaweza kubadilisha chochote
 
Maua hunyauka, hadithi huisha na kumbukumbuku husahaulika. Siyo sawa.
 
Naomba twende kwa mfano ili tuelewane.
Maiti ya mama yako na mchicha wa 2000, kipi unadhani ni bora kitupwe jalalani kiliwe na mbwa?!

Kwanini utupe mchicha wakati kuna watu wanahuhitaji waule na kwa desturi za wanadamu maiti huzikwa na wengine huchoma ila mchicha huliwa je maiti unakusaidiaje mheshimiwa?
 
Ikishakuwa sawa au si sawa? Heri ufanye unaloliona wewe lipo sawa kuliko kuishi kwa kutegemea akili za watu
 
kuabudu sio haki. ni maamuzi binafsi, ndio maana unaweza kutoabudu chochote au yeyote.
pia kuombea na kuabudu ni mambo mawili tofauti.
kwa mtazamo wangu haina maana sana kwa kua maiti ni sehemu ya tuchokipata kutokea kwene dunia hii na kuzika ni part ya kukirudisha so kuombea maiti...ni kupoteza mda......kitokacho kwa Mungu ndio kinarudi kuhukumiwa na hukumu inatokana na namna mtu alivotumia mda wake duniani kufanya mema au mabaya...cdhani kama maombi yanaweza kubadilisha chochote

Mimi kwa upande wangu naona kuombea na kuabudu maiti haina maana kabisaaa na sio kidogo kama uonavyo wewe.
 
Kimsingi si sahihi na hata kibiblia pia c sahihi na nikosa kubwa Hakuna ibada ya wafu pia na MTU akifa ni hukumu nyinyi hata mkiomba Mara mia kwa cku haisaidia ushauri ACHENI KUTENDA MABAYA JIFUNZENI KUTENDA MENA

Asante kwa mchango wako mkuu.
 
Ikishakuwa sawa au si sawa? Heri ufanye unaloliona wewe lipo sawa kuliko kuishi kwa kutegemea akili za watu

Bila kutegemea akili za watu hata kusoma na kuandika usingejua elizabeth.jifunze kupitia kwa watu chuja mema uache mabaya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom