Ni Aibu Vijana Kuishabikia CCM

Ni Aibu Vijana Kuishabikia CCM

Mkuu Elli, Ule mkutano wa vijana wa vyuo vikuu CCM ilikuwa ni kuandaa vifisadi vya baadae, unajua hata Simba akiona watoto wanakua inabidi awafundishe mbinu za kuwinda, kwa hiyo mkuu Elli usiwe na wasiwasi, hao ni the future thieves, ni mafunzo tu.

Kwanza huyo mama Tibaijuka mwenyewe ambae aliwahutubia anamiliki apartment kubwa yenye thamani ya mabilioni hapo Kinondoni, ambapo kutokana na kazi yake hawezi kuimiliki. Pia anamiliki eneo la ekari mia moja kigamboni. So, siku ile ilikuwa ni kufundishana vijana wizi
Eti unaunda mkoa wa vyuo vikuu na unamuweka katibu huko ni kushindwa kabla hujaanza,hivi wanavyuo wanapokuwa likizo huwa anazungukia mikoa yote kuwatathimini?.Ni ukweli mtupu kuwa vijana wanaoimba iyene iyena wengi wao wanapigania matumbo yao,hawaijui nchi wala hawana uchungu nayo,kwao wao muhimu ni vijisenti na kazi tuuuu.
 
Umeandika kwa uchungu sana ! Hii ni ishara ya kuguswa na matatizo ya nayowakabili vijana wa nchi hii , ni hivi , hao hawakuwa vijana tu bali walikuwa vijana marafiki , ndugu , watoto ama jamaa wa viongozi , walikuwa ni WATENDA DHAMBI WA KAWAIDA TU ,WACHUMIA TUMBO NA WAKUFURU MUNGU TU , MAANA IMEANDIKWA KWAMBA USISHABIKIE MAOVU .
 
Mmmhh ndio maana kuna mwana jamvi mmoja alileta uzi unaosema "UKIONA KIJANA ANAISHABIKIA MAGAMBA JUA AKIWA MZEE ATAKUWA MCHAWI" huo uzi niliupenda maana huyo mdau aliekezea kwa uchingu namna vijana wanavyo danganyika kwa kununuliwa na magamba kwa pesa mbuzi...hakina ni kweli kijana yoyote anaye unga mkono magamba jua upstairs hayuko sawa...
 
Kimsingi ujue unataka kusema Baba na Mama yake kwa sasa ni wachawi?
Maana walkway vijana walikuwa Chama kubwa CCM,,,,,,,,,,,PILI,kisiasa ni suala la kimsingi Kabisa vijana kupishana mawazo kuelekea maendeleo......Kama siasa huijui acha ushabiki utaishia kuwekwa front line.
 
Umeandika kwa uchungu sana ! Hii ni ishara ya kuguswa na matatizo ya nayowakabili vijana wa nchi hii , ni hivi , hao hawakuwa vijana tu bali walikuwa vijana marafiki , ndugu , watoto ama jamaa wa viongozi , walikuwa ni WATENDA DHAMBI WA KAWAIDA TU ,WACHUMIA TUMBO NA WAKUFURU MUNGU TU , MAANA IMEANDIKWA KWAMBA USISHABIKIE MAOVU .
Ni kweli kabisa unachokisema, watu tunaotarajia walete mageuzi ndio hao wameshageuzwa tayari
 
Kibongobongo kushabikia chama chochote au mwanasiasa yeyote unakuwa unajidhulumu nafsi yako..hawaaminiki hata kidogo wote wamekaa kipigajipigaji ...nimtizamo wangu binafsi katika siasa za hapa bongo
 
Kwanza inabidi upewe pole kwa upeo wako mdogo wa wazua mambo vijana siyo mbugila kwama wewe kiasi kwamba unaweza kuwadanganya kirahisi wakafuata mawazo yako ya kibavicha nchi yetu chini ya ccm imepiga hatua kubwa na kuwa kioo kwa mataifa mengine katiba mpya imeweka baraza la vijana ili vijana wawe na sehemu ya kusemea wakati chagadema kijana haruhusiwi hata kuhoji tu.

Nani anayesikia wakisema? Kwani tatzo ni kusema? Kama kusema mbona watu wamesema sana tu na hakuna kilixhotokea? hata bungeni wamesema, lakini wale 'wasikivu' wanapotezea na kudai kuwa 'ni upepo, utapita tu'. Kweli kwa mtindo wa fikra hizi, tujipange kuwa extinct!
 
Unataka vijana washabikie chama gani?
hahahaahaaa sikufungua mada ili niwachagulie vijana chama, si jukumu langu kuwachagulia chama but ni jukumu langu Mimi kama Mtanzania kuonyesha ubaya wa CCM
 
jeshi lichukue nch tunyoshane tu huku mitaani after that tutaheshimiana kama Rwanda,hawa Chadema ,Cuf etc ni kama toilet paper iliyochambiwa maana haifai ,na CCM ndio kile kitu ambacho toilet paper imepangusa..i hate politics,CCM hawajui kijana anaishije,dnt talk about inflation rate..talk about hyper inflation rete,have you ever take a moment to think about unemployment level? watu wamemaliza chuo kikuu wanamiaka kumi hawajawhi hata kupata temple,mnaawaambia wakajiajili? wapi wakajiajili kwa mama zenu? mbona nyie,watoto zenu na mademu zenu mnawapa ajira tena bila hata interview na hamauwaambii wakajiajili?
nimeandika kwa staha wish kama mngekuwa mnasikia kile ninachowaza kichwani mwangu
 
CCM ni janga kwa taifa hili na mbaya zaidi vijana wanapewa elimu ya kikoloni ili kuwaandaa kuwa wachumia tumbo na watu wa kujipendekeza kwa hawa watawala mafisadi na wahujumu uchumi kwa ujira wa mkate na pombe! Pambafu sana
 
Mimi nilikua shabiki wa CCM, nikiamini kuwa kutokana na education level na culture ya Africans na Tanzania ilivyo a single strong party ndio njia sahihi ya kuleta maendeleo ya haraka kwa kipindi hichi. Kama ilivyokua kwa China.

Nilikua na imani hio sababu nilikua nafikiria kuwa CCM ina nia ya dhati ya kukomboa wananchi na kuleta maendeleo. Nilikua nafikiri ya kwamba ukija upinzani mkubwa tutaleta machafuko na malumbano zaidi ya maendeleo.

Ila I have never been so wrong!!

Kwa kweli kijana yeyote, mwenye akili timamu, nia ya dhati ya kuleta maendeleo kwa Tanzania nzima, asiye mbinafsi na kujali tumbo lake tu, hawezi ku support CCM.
Hata kama hataenda upinzani, HAWEZI KUBAKI CCM!!

Kijana au mtu yeyote aliyeko CCM ni aidha:
A. Hana elimu/mjinga
B. Ameweka maslahi yake yeye binafsi mbele ya maslahi ya nchi na watu wake.

Hao "wasomi" ni B. Maisha ni magumu wanatafuta namna ya kutoka kwa kujibembeleza CCM na kusahau kabisa wazazi wao na ndugu zao wanvyopata tabu mijini na vijijini na hawatambui kuwa kushibisha matumbo ya kibinafsi haitainua nchi kwa ujumla.

Huwezi ukawepo CCM na ukawa unania ya dhati kuikomboa Tanzania
 
Watu wanajua kuliko wewe unavyoona na ndio maana wanafanya maamuzi yaliyo sahihi. Na kila mtu ana mawazo na maono yake kwa hiyo si sahihi kumlazimisha aamini kile unachokiamini wewe. Mfano, mimi naamini mafanikio yangu ni nguvu zangu mwenyewe na kuwa mbunifu katika kufanya kazi zangu, na hii ndio silaha kubwa inayonibeba kila siku. Siamini mafanikio katika chama chochote cha siasa. Wanasiasa wote ni watafuta ajira kama walivyo wengine wanaozunguka na bahasha za khaki kusambaza CV. Maneno ya sukari wanayoyaongea majukwaani ni sawa tu na uandikaji CV unavyorembeshwa ili kumvutia mwajiri.
 
Leo unaweza mpka kuingia mitandaoni kueleza unayoyaeleza nchi ikiongozwa na hao hao CCM.

Bado unalalamika kijana?

Ulitaka uletewe kila kitu kama mgonjwa? au ni mgonjwa kweli?

Au ni mazungumzo baada ya habari?
 
Leo unaweza mpka kuingia mitandaoni kueleza unayoyaeleza nchi ikiongozwa na hao hao CCM.

Bado unalalamika kijana?

Ulitaka uletewe kila kitu kama mgonjwa? au ni mgonjwa kweli?

Au ni mazungumzo baada ya habari?

Kama hivi ?
 
Watu wanajua kuliko wewe unavyoona na ndio maana wanafanya maamuzi yaliyo sahihi. Na kila mtu ana mawazo na maono yake kwa hiyo si sahihi kumlazimisha aamini kile unachokiamini wewe. Mfano, mimi naamini mafanikio yangu ni nguvu zangu mwenyewe na kuwa mbunifu katika kufanya kazi zangu, na hii ndio silaha kubwa inayonibeba kila siku. Siamini mafanikio katika chama chochote cha siasa. Wanasiasa wote ni watafuta ajira kama walivyo wengine wanaozunguka na bahasha za khaki kusambaza CV. Maneno ya sukari wanayoyaongea majukwaani ni sawa tu na uandikaji CV unavyorembeshwa ili kumvutia mwajiri.
ni kweli mkuu , maana wakati wao wanaagiza VOGUE 600 huku hali iko hivi ,
 

Attachments

  • Wanafunzi---0ctober22-2014.jpeg
    Wanafunzi---0ctober22-2014.jpeg
    20.6 KB · Views: 84
Back
Top Bottom