NHIF watumie mfumo wa fingerprint scanner kutambua wanufaika/ watoto badala ya kusumbua wazazi

Trubarg

JF-Expert Member
Jan 8, 2020
4,261
6,908
Habari wadau. Kumekuwa na wimbi la wafanyakazi wa NHIF waliopo mahospitali kuwataka wazazi wabadilishe vitambulisho vya watoto kwakuwa picha zilizopo kwenye vitambulisho hazifanani na watoto kutokana na kubadilika.

Mimi hiki sikatai. Watoto wadogo wako katika hatua ya makuzi si jambo la kushangaza kuona mtoto akibadilika sura kila baada ya mwezi mmoja au kama si mwaka. Sasa sijafahamu kwanini hawa watu wanataka mtu abadilishe kadi kila sura inapobadilika, je hawajui kwamba hawa watoto wanakua. Kubadilisha kadi/ kitambukisho kinagharimu kiasi cha shilingi elfu ishirini. Kama mzazi ana mtoto zaidi ya mmoja inagharimu zaidi.

Nafahamu kwamba mzazi huwa anaulizwa details mbalimbali zinazohusu mtoto au mchangiaji kabla ya kadi au kitambulisho kutumika, lakini taarifa hizi kwao huwa bado hazitoshi wanasisitiza picha ya mtoto. Mimi nashauri badala ya kung'ang'ania mfumo tambuzi mmoja wa picha, wawekeze kwenye mifumo mingine ya utambuzi kama fingerprint scanner au scanner ya macho ambayo naamini ni za kudumu kuliko hii ya kusumbua wazazi kubadilisha vitambulisho mara kwa mara.

Mimi ndugu yangu mtoto wake mwenye mwaka mmoja alikataliwa kitambulisho cha mtoto wake kisa mtoto sura imebabadilika, huu ni uonevu wa hali ya juu.

Majibu ya NHIF, soma hapa - NHIF: Tutaanza kutambua Wanachama wetu kwa Kitambulisho cha NIDA
 
Kwanini watoe kadi yenye picha ya mtoto na maelezo kuwa kadi itatumika kuanzia mwaka fulani hadi mwaka fulani halafu ghafla hapo katikati waibuke na hoja ya utofauti wa picha? Kweli ni usumbufu kwa wanachama wa huo mfuko.
 
Mimi sijaelewa matumizi ya picha nimeona ji ya kizamani sana wao walitakiwa watumie dole gumba ndio linamuonesha picha yako kule sio hata ubadilike vipi italeta tuu...mbona uhamiaji tunatumia vidole na wao wanapata picha kwenye system yao na picha za huu mfuko sio bora watu wanabandika yeyote bila vigezo watawarudisha sana wagonjwa kwa mfumo wao mbovu niliona Hospital moja jamaa akizozana na hao watu wa Mfuko...
 
Mimi sijaelewa matumizi ya picha nimeona ji ya kizamani sana wao walitakiwa watumie dole gumba ndio linamuonesha picha yako kule sio hata ubadilike vipi italeta tuu...mbona uhamiaji tunatumia vidole na wao wanapata picha kwenye system yao na picha za huu mfuko sio bora watu wanabandika yeyote bila vigezo watawarudisha sana wagonjwa kwa mfumo wao mbovu niliona Hospital moja jamaa akizozana na hao watu wa Mfuko...
Naona wanaleta janja janja. Pesa wanakata kila mwezi but wanachiweza wao ni kusumbua walezi
 
Fingerprint za watoto sio reliable, zinakua bado haziko well formed
 
Nchi wataalamu na wasomi wameshindwa kutatua changamoto ndogo ndogo.
Yale yale ya vituo vya mafuta vinachanganya mafuta ya taaa na petrol.
Soln
Pandisha bei ya mafuta ya taa izidi ya petrol. Wakati huo huo masikini zaidi ndio wanaotumia sana mafuta ya taa
 
Kwanini watoe kadi yenye picha ya mtoto na maelezo kuwa kadi itatumika kuanzia mwaka fulani hadi mwaka fulani halafu ghafla hapo katikati waibuke na hoja ya utofauti wa picha? Kweli ni usumbufu kwa wanachama wa huo mfuko.

Halafu ndo tuseme kuna wasome NHIF yaani wanabuni vitu hata darasa la saba hawezi kufanya kitu kama hicho …watoto wachanga kila baada miezi mitatu sura inabadilika
Sasa hapo fikiria kama akiungua moto au kuugua ugonjwa wa kichwa kikubwa sijui watafanyeje
Finger print ni zuri sana
 
Kama wameweza kusomesha watoto bure wanashindwa nini kusaidia kila mzazi atleast awe na special card for certain years?
Mkuu suala hapa siyo kuomba kutibiwa bure, watu wanakatwa 6% yamshahara kila mwezi kwa ajili ya hii bima. Kinachotakiwa hapa ni kuboresha mifumo na kuacha kusumbua walezi na wazazi.
 
Kumbe huruhusiwi kumkatia bima mtoto unayemlea wewe ambaye sio mtoto wako wa kumzaa?
 
Back
Top Bottom