NHC yambwaga Mbowe Mahakamani

NHC yambwaga Mbowe Mahakamani

Atalipa tu bilioni kitugani ! Kikubwa sheria ifuate mkundo wake
 
Hebu maliza kuchukua elfu 7 ya MB then tulia weka habari yenye afya......
 
Hoja ilikuwa kulipa kodi ya pango au kumiliki jengo la NHC.Hakulipa kodi kwasababu alidai anamiliki hilo jengo na ndio mashtaka yaliokuwa mahakamani.Labda kwa kuwa mahakama imetupilia mbali madai ya umiliki wa jengo,sasa ana haki ya kudai fidia ya gharama alizotumia kujenga na kukarabati hilo jengo.Kosa lake Mbowe ni kuwa Kiongozi wa Vyama vya upinzani bungeni UKAWA.
 
Hii inasikitisha sana kwa siasa zetu pamoja na sura halisi ya viongozi wetu
kitaifa. Je Mbowe ni kama Trump kuwepa kodi tangu miaka ya 90?

-------------
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameangukia pua mahakamani baada ya Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi kutupilia mbali maombi yake katika mgogoro wake wa umiliki wa jengo la Shirika la Nyumba (NHC).

Mbowe alifungua maombi mahakamani hapo kupitia kampuni yake ya Mbowe Hotels Ltd, akipinga uamuzi wa NHC kumuondoa katika jengo ambalo alikuwa akilitumia kama ofisi ya kampuni yake ya Magazeti ya Free Media na klabu ya Bilicanas.

Katika maombi hayo, pamoja na mambo mengine Mbowe alikuwa akidai kuwa aliondolewa katika jengo hilo jinyume cha sheria kwa kuwa hakupewa taarifa na kwamba kampuni ya udalali iliyotumiwa kumuondoa haijasajiliwa kama dalali wa mahakama.

Hata hivyo katika uamuzi wa mahakama hiyo uliotolewa leo na Jaji Sivangilwa Mwangesi, imetupilia mbali maombi hayo ya Mbowe ikisema kuwa hayana msingi

Jaji Mwangesi alikubaliana na hoja za NHC na akasema kuwa Mbowe aliondolewa katika jengo hilo kisheria.


Chanzo: Mwananchi
Nimeipenda
 
Haki ya mtu haipotei. Itacheleweshwa na baadaye atapewa.

Kama vile ilivyo kwa haki yetu ya kujua wasifu wa elimu wa viongozi wetu,shule gani walisoma na matokeo yao ni yepi. Wanatuchelewesha tu kuijua lakini ipo siku tataijua!
 
Back
Top Bottom