Pro-Chadema JF utasikia wanasema Mahakama aitendi haki baada ya kesi ya Mbowe kutupiliwa mbali.
Hamna namna Mbowe alipe deni.
Kamanda hataki kuamini macho yake.Ametaja source reliable, unalako jambo
Taritibu, utakuja kutukana bure.Atalipa tu bilioni kitugani ! Kikubwa sheria ifuate mkundo wake
Mleta mada mbona unaharaka sana?hebu ivisha kwanza hii habari kwa maana sijaona maneno kama "kwa mujibu wa kifungu namba...,neno katiba nk
Hahahahahaaa sawaa kamandaa pipoooooozzzzzMakamanda tuipongeze mahakama kwa kutenda haki.
Lakini tusisahau Mbowe anatakiwa kujitokeza kueleza kuhusu elimu yake...
aisee umewaza kiundani sana big upKwa masuala binafsi wanakimbilia mahakamani, kwa maslahi yao ya kisiasa, wanatumia vyombo vya habari, mikutano ya hadhara na maadamano, kudai kile kisichokuwepo, mradi waonekane wapo na wasikike
Nimecheka sanaTarehe ya mnada wa vitu kufidia kadi naomba tufahamishane, mimi naitaka ile mixer.
Hata yule mwanahabari huru leo kimya.akina ben saa tisa , yereko nyerere, wako wapi maana ndio wanakuwa ma PS wa huyu jamaa
lissu yuko wapi yule bingwa wa kushinda kesi za dhamana. Jaji huyu ameenda kutoa haki sio kufuata ubabaishaji on technicalities ambapo kina lissu wamebobea. kama dalali hana leseni kwa jaji mtoa haki kwa mwenyewe ameona si issue.Hii inasikitisha sana kwa siasa zetu pamoja na sura halisi ya viongozi wetu
kitaifa. Je Mbowe ni kama Trump kuwepa kodi tangu miaka ya 90?
-------------
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameangukia pua mahakamani baada ya Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi kutupilia mbali maombi yake katika mgogoro wake wa umiliki wa jengo la Shirika la Nyumba (NHC).
Mbowe alifungua maombi mahakamani hapo kupitia kampuni yake ya Mbowe Hotels Ltd, akipinga uamuzi wa NHC kumuondoa katika jengo ambalo alikuwa akilitumia kama ofisi ya kampuni yake ya Magazeti ya Free Media na klabu ya Bilicanas.
Katika maombi hayo, pamoja na mambo mengine Mbowe alikuwa akidai kuwa aliondolewa katika jengo hilo jinyume cha sheria kwa kuwa hakupewa taarifa na kwamba kampuni ya udalali iliyotumiwa kumuondoa haijasajiliwa kama dalali wa mahakama.
Hata hivyo katika uamuzi wa mahakama hiyo uliotolewa leo na Jaji Sivangilwa Mwangesi, imetupilia mbali maombi hayo ya Mbowe ikisema kuwa hayana msingi
Jaji Mwangesi alikubaliana na hoja za NHC na akasema kuwa Mbowe aliondolewa katika jengo hilo kisheria.
Chanzo: Mwananchi