Nguo zenye rangi ya Jeshi

Nguo zenye rangi ya Jeshi

Huyo kibaka alovaa kofia ya jeshi alipaswa kuvuliwa nguo zote abaki uchi, watanzania mmekuwa viburi sana, vibaka kama hao nikiwakuta sehemu yoyote nawatia mbata nawavua nguo zote
Ndio maana ukawa muuza madafu hukuwa mjeda
 
Achaa akili za kiloko kama za police wa zamani walikua hawataki tupaki gari zetu aina ya BMW karibu na Bank, kisa tu zinakimbia sana,na wahalifu wanazitumia kuibia ma Bank! Suburini mpaka hapo Mtu atakapofanya uhalifu ndiyo umchukulie hatua!!
Damu iliyomwagika inarudije kinga ni bora
 
Kuna mdada mmoja alikutwa mtaani kavaa kipedo chenye rangi za kombati za jeshi wakamvua kibabe. Askari magereza nao waliwahi kuleta za kuleta kwa makonda wa daladala wakidai wamewaiga sare zao. Polisi nao waliwahi kuliamsha dude wakipiga mkwara sare zao zisivaliwe na raia hata kwenye sanaa

Mkuu huyo mdada alivyovuliwa akabaki na chupi?
 
uyo mjeda mshamba tu binafsi ninayo kofia ya combat navimbia usiku kwa sababu ya mambo kama haya
 
Sheria ya ulinzi inakataza raia yoyote kuvaa Mavazi yanayofanana na Jeshi lolote la Tanzania kwa rangi ama mshono. Kadhalila inakataza askari wa Jeshi A kuvaa au kufananisha uniform za Jeshi B bila kibali. Ukienda dukani au kwenye mitumba ukimkuta nguo yoyote inayofanana na Jeshi lolote Tanzania ,achana nayo tafuta nyingine inayoendana na wewe. Lengo la sheria hii ni kuthibiti matumizi mabaya ya uniform ambazo wahalifu wanaweza kuzitumia au kujitambulisha kama ni wahusika wa vyombo vya ulinzi na usalama kwa watu wasiojua na kufanya uhalifu.

Ewe msanii uwe wa maigizo au wa nyimbo epuka kuvaa nguo zinazofanana na za majeshi yetu

Ewe mwanasiasa achana kabisa na mashono ya majeshi au kushona vitambaa vinavyofanana na rangi za nguo za majeshi

Ewe mmiliki WA kampuni binafsi ya ulinzi hakikisha uniform za wafanyakazi wako hazifanani na za majeshi yaliyoamishwa na sheria ya nchi
Je nguo za watoto wa mwaka mmoja au miwili au mitatu nazo ni haramu?
 
Huyo askari,mjinga tu, akipigwa,aanze kulaumu vijana kupata mafunzo ya JKT na kukosa ajira.Mjinga sana.
 
Majeshi ya zamani alafu wengi wao ni wanajeshi wale Darasa la saba sasa mtu kavaa kofia ya kufanania tu we unamuogopea nini? Hajui silaha hana kozi yoyote.
Madhala ya kukosa vita hata vya kirafiki kunasababisha wanajeshi wetu kuanza kutafuta ma timberland trousers mtaani.
Ili watest mitambo!?
 
Sheria ya ulinzi inakataza raia yoyote kuvaa Mavazi yanayofanana na Jeshi lolote la Tanzania kwa rangi ama mshono. Kadhalila inakataza askari wa Jeshi A kuvaa au kufananisha uniform za Jeshi B bila kibali. Ukienda dukani au kwenye mitumba ukimkuta nguo yoyote inayofanana na Jeshi lolote Tanzania ,achana nayo tafuta nyingine inayoendana na wewe. Lengo la sheria hii ni kuthibiti matumizi mabaya ya uniform ambazo wahalifu wanaweza kuzitumia au kujitambulisha kama ni wahusika wa vyombo vya ulinzi na usalama kwa watu wasiojua na kufanya uhalifu.

Ewe msanii uwe wa maigizo au wa nyimbo epuka kuvaa nguo zinazofanana na za majeshi yetu

Ewe mwanasiasa achana kabisa na mashono ya majeshi au kushona vitambaa vinavyofanana na rangi za nguo za majeshi

Ewe mmiliki WA kampuni binafsi ya ulinzi hakikisha uniform za wafanyakazi wako hazifanani na za majeshi yaliyoamishwa na sheria ya nchi
Mkuu ni rangi ngapi ambazo ni marufuku haturuhusiwi kuvaa sisi raia?

Maana ninavyojua rangi ambazo huvaliwa katika sare za majeshi yetu ni nyingi sana.

Kuna nyeupe, nyeusi, nyekundu, njano, kijani, light blue, light green, ugoro, kijivu nk nk, yaani ni yingi mno na ndiyo hizo rangi za vitambaa vya suti zimejaa madukani!

Kwa mfano mimi napenda kutinga suruali ya kitambaa ya polyster jeupe lisilokuwa na madoa, kwa hiyo Traffic Police akiniona apite na mimi?

Karibia rangi zote nilizozitaja, suruali zake ninazo kwa hiyo nikaziteketeze?!

Basi angalao tuwekeeni vifungu vya sheria vinavyotoa haki miliki kwenu ninyi wanajeshi kuhodhi rangi hizo.

Maana isije kuwa ni vita vya kibiashara ambayo mnaipigana bila kujua.

Kuna kodi ya Serikali katika biashara ya nguo ujue!
 
Back
Top Bottom