Scars
JF-Expert Member
- Apr 8, 2017
- 50,159
- 123,244
Sheria zingine zakiboya sana na hii inaonesha serikali ipo insecure.Sheria ya ulinzi inakataza raia yoyote kuvaa Mavazi yanayofanana na Jeshi lolote la Tanzania kwa rangi ama mshono. Kadhalila inakataza askari wa Jeshi A kuvaa au kufananisha uniform za Jeshi B bila kibali. Ukienda dukani au kwenye mitumba ukimkuta nguo yoyote inayofanana na Jeshi lolote Tanzania ,achana nayo tafuta nyingine inayoendana na wewe. Lengo la sheria hii ni kuthibiti matumizi mabaya ya uniform ambazo wahalifu wanaweza kuzitumia au kujitambulisha kama ni wahusika wa vyombo vya ulinzi na usalama kwa watu wasiojua na kufanya uhalifu.
Ewe msanii uwe wa maigizo au wa nyimbo epuka kuvaa nguo zinazofanana na za majeshi yetu
Ewe mwanasiasa achana kabisa na mashono ya majeshi au kushona vitambaa vinavyofanana na rangi za nguo za majeshi
Ewe mmiliki WA kampuni binafsi ya ulinzi hakikisha uniform za wafanyakazi wako hazifanani na za majeshi yaliyoamishwa na sheria ya nchi
Marekani ni ruhusa kuvaa sare za jeshi isipokuwa usitumie sare hizo kufanya fraud tu.