News Alert:...... Uteuzi cabinet


"Tusiwadanganye wananchi, kuwa tukiwaondoa wala rushwa, matatizo ya Watanzania yataisha.


"Tunaanza kuwa na utamaduni wa kutafuta dosari hasa za viongozi na kusahau mambo ya msingi ya kulisaidia taifa. Ombi langu, hii tabia ya kupakana matope haiisaidii nchi, waandishi hizi habari ndizo zinapaswa kupewa kipaumbele?"
[/SIZE]

Kuhani Mkuu,

Na huu ni ndio upumbavu na uhuni watanzania tunaoupigia makelele... ati tunafikiri billioni moja(1) ya mzee wa vijisenti itaondoa tatizo la uchumi.

Siku moja nikakutana na mkaanga Samaki pale Dar es Salaam akaniuliza hivi, "Hivi kaka hizo fedha za EPA zikirudishwa mambo yatabadilika eeeh" nikamwambia sio fedha za EPA tu, na Za Meremeta n.k. ni maji ya kifuu kwenye bahari... ni kitu kidogo sana kwa uchumi wa nchi... tufanye kazi ndio njia ya kukomboa taifa.

Lingine ni Ujinga pia kudhani kwamba Rais alitakiwa kufanya mabadiliko makubwa kipindi hiki ambacho baraza lina miezi michache sana.

Kibaya zaidi vyama vyetu makini wakombozi wa wananachi wanafanya kwamba hizo ndio hoja kuu za kufanya uchumi ukue!!! Taifa linazama hili chini ya CCM au hata chini ya Kile chama makini.

Kwanza:
Ilikuwa ni Jambo jemaa kutoleta waziri mwingine mpya... kwanza kama habari ziko kamili kweli, atakuwa ampenguza waziri mmoja, kwenye baraza lake.

Pili:
Wizara ya Miundo Mbinu ni wizara nyeti sana, fedha nyingi zinaenda huko kupeleka mwadilifu na huenda mtu anayemwamini ni njia moja ya kulinda masilahi yetu wananchi.

Tatu:
Tusichanganye mambo mawaziri ni wanasiasa, kazi ya msingi inafanywa na makatibu wakuu na wakurugenz;

Nne;
Waziri ni mtizama masilahi ya wananchi akipenda of course maana anaweza angalia masilahi yake... lakini zaidi Waziri ni mtu anayeangalia kwamba sera za chama chake kama zinatekelezwa vizuri.
 
Kama alivyosema Mwanakijiji, hakukuwa na sababu ya Rais kupangua wizara tena wakati alifanya hivi miezi miwili iliyopita! Angemteua waziri wa miundombinu hata kutoka nje ya hawa mawazi tulionao! Hii habari ya kuwahamisha watu ndio nini! Ndio kuwaongezea CV, kuwa waliongoza wizara nyingi!!! Sikubaliani na hoja kwamba waziri hana role kubwa kwenye wizara isipokuwa katibu mkuu!! Kwa nchi changa kama TZ´, waziri is everything kwa sababu ndiye mpika majungu kwa Rais!!! Simply JK amechanganyikiwa na kwa mtindo huu tusitarajie jipya, labda more disappointments! Tukae mkao wa msiba mpaka 2010! Na hapo tena tukijichanganya ndio hivyo tutakuwa na sisi ni mafisadi haohao!
 
Kama alivyosema Mwanakijiji, hakukuwa na sababu ya Rais kupangua wizara tena wakati alifanya hivi miezi miwili iliyopita! Angemteua waziri wa miundombinu hata kutoka nje ya hawa mawazi tulionao! Hii habari ya kuwahamisha watu ndio nini! Ndio kuwaongezea CV, kuwa waliongoza wizara nyingi!!! Sikubaliani na hoja kwamba waziri hana role kubwa kwenye wizara isipokuwa katibu mkuu!! Kwa nchi changa kama TZ´, waziri is everything kwa sababu ndiye mpika majungu kwa Rais!!! Simply JK amechanganyikiwa na kwa mtindo huu tusitarajie jipya, labda more disappointments! Tukae mkao wa msiba mpaka 2010! Na hapo tena tukijichanganya ndio hivyo tutakuwa na sisi ni mafisadi haohao!

Haki.Tupu;

Upande mwingine wa wazo lako ni kwamba kama unataka kutochukua muda sana kwa waziri kusoma politics za uwaziri ni bora reshufle kuliko kuleta waziri mpya....

Tusubiri nasi tukishika nchi tutafanya tunavyotaka!!! Tulipompa urais tulimpa taasisi na mamlaka yote... hatukumpa nusu nusu.. kwi kwi kwi
 
Kitu kimoja kizuri katika mabadiliko kadhaa anayofanya JK ni kupandisha manaibu kuwa Mawaziri. Hili ni zuri. Naunga mkono uteuzi wa Kombani TAMISEMI. Hivi hakuteua naibu Waziri TAMISEMI? Maana sijaona hapa au mmesahau?

Mwanri pia ni mzalendo sana, ni chaguo zuri ingawa angefaa kuwa Waziri Kamili. Jamaa ni marxist huyu, acha!
 
Mkuu,

ikiwemo e-governance.ambayo inaweza kuondoa matatizo chungu nzima ikiwa ni pamoja na corruptions na safari zisizo na maana kwenye mikutano isiyoisha.
Mbona issue ya E-governace iko ofisi ya rais utumishi na ipo jikoni tembelea pale kuna mtandao wa serikali upo jikoni(Gov intranet/WAN)
 
Msolla tena, huyu jamaa hawezi kabisaaaa, arudi tu SUA tu akafanye research. Kuwa prof sio kuweza kila kitu anajishusha tu hapo, anashindwa kumuomba muungwana amrelease kama walivyofanya kina mungai? duh kaazi kweli kweli. Tanzania hivi hakuna watu wengine wenye uwezo zaidi ya hawa?
Arudishwe SUA akaendelee kuiba,Kwanza huyu Mzee ni Mwizi sana,alipokuwa wazizara ya Elimu ya juu alijaza ndugu zake pale Bodi ya mikopo1.Aliweka Mkurugenzi wa Mawasiliano,sera na utafiti kutoka SUA,huyu kijana ni mtoto wa Rafiki yake na Msolla,na anafundisha SUA2.Msolla aliendelea kwa kumuweka Msaidizi wa huyo Mkurugenzi kijana kutoka SUA tena,Bila utaratibu kufuatwa sababu hata kazi hazikutangazwa magazetini3.Mhe. Msolla Pia amemuweka Mkwe wake pale Bodi ya Mikopo,sasa unataka arudishwe SUA akaibe Zaidi??hawa ndio watu ambao wanatakiwa kutoka,ninatamani nikutane na JK tena nitamuuliza kwanini amemrudisha Msolla Tena??Huyu Msolla si ndiye1.Aliyewakana wana wa watanzania ambao walikuwa Ukraine?2.Msolla huyu si ndiye aliyeiba pesa za SUA3.Msolla huyu ndiye bingwa wa kulea Migomo??Ukitaka Kumjua Mtu basi angalia Rafiki zake,alyemteua naye ni mtu wa hivyo
 
Tanzactive!

Na sisi ni washauri! Kama hao nao ni watanzania, basi lao na letu ni moja - kumshauri rais kwa nia njema! Sio kwa sababu ya vested interests! Lakini pili hao washauri wa rais nadhani nao wanahitaji washauri! Kumbuka hata Hitler nk walikuwa na washauri BWANA! Inashangaza kuona mtu unakuwa na uchungu sana na comments huru zinazotolewa! Kwa nini uwe na hasira, toa maoni yako! Kama umeupenda uteuzi sema, na sababu zake toa! La sivyo unaweza kufikiriwa nawa kuwa na masilahi ya moja kwa moja na haya madudu katika uteuzi!
 
rais emejishokea bora naye ajiuzulu,hakuna jipya kwa sisi watanzania,bora ajiondee katika uteuzi wa mawaziri
 
Nchi iko njia Panda Muda MrefuJk should be a one Term President,i thought angepunguza Mawaziri..Zitto Check PM yako.
 
Kitu kimoja kizuri katika mabadiliko kadhaa anayofanya JK ni kupandisha manaibu kuwa Mawaziri. Hili ni zuri. Naunga mkono uteuzi wa Kombani TAMISEMI. Hivi hakuteua naibu Waziri TAMISEMI? Maana sijaona hapa au mmesahau?

Mwanri pia ni mzalendo sana, ni chaguo zuri ingawa angefaa kuwa Waziri Kamili. Jamaa ni marxist huyu, acha!
Zitto,

Kuna matatizo madogo kwenye news alert
...ingawa ni kawaida ukitaka kuwa wa kwanza kutoa taarifa....
sahihi Iko hivi:-

1. Miundo Mbinu --- Dr. Kawambwa

2. Mawasiliano ---Pro. Msolwa

3. TAMISEMI -----Celina Kombani

4. Kilimo ----- Wasira

5. Naibu Miundo Mbinu --- Chibunje

6. Naibu Kazi, Vijana --- Makongoro

7. Naibu TAMISEMI ---- Agrey Mwanri (Kada wa Chama) huyu ni kada mpinzani...

My take; Mabadiliko sio makubwa kama watu wanavyodhani... Wasira alikuwepo kilimo; Celina yuko kwenye TAMISEMI hiyo hiyo...

Kwa hiyo mabadiliko, huwa tunaangalia kwenye mawaziri nayo ni... pale mawasiliano... na Miundo Mbinu tu.

Wachambuzi wa siasa correct me if i'm wrong...
 
Tanzactive!

Na sisi ni washauri! Kama hao nao ni watanzania, basi lao na letu ni moja - kumshauri rais kwa nia njema! Sio kwa sababu ya vested interests! Lakini pili hao washauri wa rais nadhani nao wanahitaji washauri! Kumbuka hata Hitler nk walikuwa na washauri BWANA! Inashangaza kuona mtu unakuwa na uchungu sana na comments huru zinazotolewa! Kwa nini uwe na hasira, toa maoni yako! Kama umeupenda uteuzi sema, na sababu zake toa! La sivyo unaweza kufikiriwa nawa kuwa na masilahi ya moja kwa moja na haya madudu katika uteuzi!
Nilidhania nawe ni Muikulu Mkuu!!!Well mimi kibaya nachokiona ni kumrudisha Msolla pale Elimu ya Juu,wakati alishashindwa!!! mengine naona safi tu isipokuwa sina uhakika na Mwanry Simfahamu huyu!!!
 
Mbona issue ya E-governace iko ofisi ya rais utumishi na ipo jikoni tembelea pale kuna mtandao wa serikali upo jikoni(Gov intranet/WAN)

Hiyo e-governance ya usanii na tunayoisema wengine ni vitu viwili tofauti.

E-governance ni kubwa mno kuliko websites zisizofanya kazi. Mfano tu kwasasa hakuna haja tena ya watu wakitaka kitu kwa mfano passport lazima wakajipange foleni pale wizara ya mambo ya ndani. Mambo yote yanaweza kufanywa online na maombi yakikubaliwa basi mhusika anajulishwa na kwenda kutoa fingerprints kwenye sehemu maalumu.

Pia hata hiyo mikutano isiyoisha, sio lazima tena kwa JK akitaka kuonana na wakuu wa mkoa mpaka eti wakutane pamoja.

Hizi juhudi zote zinaweza kusimamiwa na wizara ya mawasiliano kwa kushirikiana na private companies.

Naamini hiyo ni sehemu ndogo tu ya mambo ambayo hiyo wizara inaweza kufanya. Kuna makubwa mengi ambayo yanaweza kupunguza matumizi ya serikali na kuongeza ufanisi.

Ukimweka prof. wa mifugo hapo, kuna kazi kweli mpaka aje aelewe dunia ya mawasiliano inaenda wapi.

Prof. Mwandosya alikuwa na mwelekeo mzuri kwenye hiyo wizara, ila tu wizara yake ilikuwa kubwa mno na hivyo kumezwa na miundo mbinu ambako kuna matatizo kila siku.
 
Kosa kubwa tunalofanya Watanzania na hata hapa JF ni kufikiri ubora wa kiongozi unatokana na kupiga kwake kelele bungeni au sehemu yoyote nyingine.

Ubora wa kiongozi unatokana na uwezo wake wa ku deliver na upimwe kwa mafanikio yake kwa kazi za nyuma.

Mtu anayeshindwa ku deliver kama mbunge sidhani kama ataweza kufanya hivyo kama waziri au kama rais.

Ni rahisi mno kuwa mpinzani au kuwa backbencher na kukosoa kila siku kama tunavyofanya hapa JF lakini ni kitu kingine kupewa usukani na kuambiwa sasa
lisukume hili gari letu kwenda kwenye nchi ya maziwa yanayotoka kwenye bomba.

Usomi ndio una faida lakini ni kigezo cha chini kabisa, ni indicator moja tu kati ya nyingi ambayo inakufanya uingie kwenye 100 bora kama lengo ni kumtafuta mtu mmoja.

Kwa dunia ya leo mtu yeyeote mwenye degree moja anaweza kabisa kuwa waziri mzuri sana ili mradi awe na sifa hizo zingine.

Tumeona maprofesa wetu wanavyochemsha kwenye wizara, tumeona madkatri ambao
hata hawafai kusimamia nyumba zao.

Hawa mawaziri wote ni wabunge, ingefaa tunapowajadili, basi tuanze na je kule wanakotoka wamefanya nini? Kama mtu anashinda kuzunguka Dar na Dodoma na kuacha jimbo lake linadumaa, mnafikiri akiwa waziri au rais kwanini asiwe naye Vasco Dagama? Wote tumeona ya JK, kila mtu alidhani ataleta maajabu, laiti tungejiuliza mapema, je kafanya nini kule kwenye jimbo lake? Huenda wala tusingeliweka matagemeo makubwa.
 
Hivi huko ikulu hakuna kazi ingine ya kufanya zaidi ya kuwapanga na kuwapangua mawiziri kila kukicha? Wataanza lini hasa kutekeleza ahadi zao walizotoa 2005?

Sijui wanapanga na kutunga nini ya kuja kutudanganya 2010? Nashangaa sana watatueleza nini tena tuwape kura. Watatuambia ni chaguo la Mungu tena? 2010 haipo mbali na wananchi wamechoka na hali hii ya uongozi butu wa nchi. Muungwana siku hizi hatumsikii wala team yake kusema habari ya kasi, nguvu wala ari tena.

Kwa kweli watanzania sasa hivi wanataka mabadiliko kwa hali ya NGUVU sana ila hawajamuona na kumtambua Kiongozi wa kuwapeleka kwenye hayo mabadiliko. Waheshimiwa Zito, Slaa, Mwakyembe, Kimaro na wazalendo wengine waTz ni wanakondoo wamepotezwa jangwani na mafisadi jamani mchungaji youko wapi awaongoze kurudi nyumbani kwao???

Yuko wapi mkombozi na mzalendo wa kweli wa kuwaonyesha waTz njia na watamfuata. Hakuna wakati wowote mzuri utakaotokea kama isipotumiwa nafasi hii ambayo wanakondoo wametawanyika wanaona chui na fisi wanakula mmoja baada ya mwingine kati yao na hawajui inafuata zamu ya nani!! Tusisubiri uchaguzi ndo tuje kusema CCM mafisadi kwa wananchi, tutumie nafasi hii wakati wananchi wana kiu ya kujua details za nani anayewafanya waishi kwa mlo mmoja usio na uhakika wakati yeye anakula na kutapika.

Tupo tayari kwa mabadiliko ila tunamtaka MUSA wa kutuvusha jangwani. EL alizomewa kwenye msiba wa Dito, wabunge wote kuitangaza bajeti yao, juzi tena BWM naye kazomewa. Hii inaonyesha juu ya waTz walivyojaa tension na hawaoni pa kuzitolea, wapo tayari sasa....... Tuamke sasa na tuelekee kunako mapinduzi na kuirudisha nchi yetu mikononi mwetu, tumeiweka rehani kiasi cha kutosha sasa
 
Hii nafikiri JK ameamua kuweka ni gia ya rivasi. Sioni kama kuna yeyote aliyechaguliwa ili ku-improve hizo wizara.

1. Miundo Mbinu --- Dr. Kawambwa _- Huyu ni mhandisi makanika sio ujenzi. Anakoenda ni ujenzi (Civil Engr.). Sidhani kama atakuwa na professional input yake mwenyewe.

NB: Sidhani kama ni Dr. maana bado hajamalizia PhD yake.

2. Mawasiliano ---Pro. Msolwa - Kilimo ndio kulikokuwa kunamfaa maana ndio elimu yake ilipo, huku ICT itabidi ajifunze hata definitions za broadband n.k. Ina maana atahitaji miezi 6-12 kuzoea tu terminologies.

3. TAMISEMI -----Celina Kombani - OK. Shule yake inafanana na majukumu aliyopewa

4. Kilimo ----- Wasira - Atengenezewe retirement

5. Naibu Miundo Mbinu --- Chibunje - OK

6. Naibu Kazi, Vijana --- Makongoro - Huyu ni kafisadi kadogo. Havitakiwi vibakishwe, vitakua.

7. Naibu TAMISEMI ---- Agrey Mwanri - OK lakini uongozi kwenye CCM ungemfaa zaidi

 
Back
Top Bottom