Hivi wametumia kigezo gani kupanga kima hicho cha chini?
Kigezo kilichotumika hapa ni kuwa "taja figure yeyote tu ili kuonyesha kuwa mishahara imepanda kwani hakuna atakayefuatilia kuona kama hili linatekelezeka." Hii mishahara hailipiki kwa hao waliotajwa na hakuna atakayedai maana ukipiga kelele unaaambiwa acha kazi na wewe utaachaje kazi wakati sehemu ya kudokoa vitu (ili kujiongezea kipato) ni hapo kibaruani.
Mnao hoji bajeti gani itawezesha kiwango hiki kulipwa bila shaka mnaikosa pointi, hii ni kwa ajili ya sekita binafsi. Kama Kada Mpinzani kwenye baa yako utaweka wahudumu 20 ni wewe mwajiri ndio utajua pesa ya kuwalipa inatoka wapi na si serikali.