Neno La Leo: Ajizi Nyumba Ya Njaa, Nitabaki Kuwa Mjamaa...

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Ndugu zangu,

Na leo tena nina neno. Asubuhi ya leo niliongozana na watoto wangu wawili kwenda sokoni kupata mahitaji ya nyumbani. Ni pale Soko Kuu la Miyomboni. Sokoni pale nilisimama ili ninunue bamia, nyanya chungu na njegere. Aliyejitokeza kuniuzia alikuwa msichana mdogo wa chini ya miaka 13. Alifanya biashara ile akiwa amekaa chini juani.

Niliingiwa na simanzi kubwa, maana msichana yule alikuwa na umri uliokaribiana na watoto wangu. Nao niliwaona wakimwangalia mtoto mwenzao ambaye ameacha kuwa mtoto na kuchukua majukumu ya watu wazima. Nilimwuliza jina lake, anaitwa Rehema. Anafanya biashara ili arudi nyumbani na senti za mahitaji mengine ya nyumbani, ametumwa na wazazi wake. Ndivyo alivyonieleza, nilimwamini, nimesikia simulizi kama hizo kabla.

Nilimpa noti ya shilingi elfu mbili. Nilivyoona kuwa alivyonifungia vimejaa mfuko nikamwuliza kama kuna hela nyingine napaswa kuongeza. Alinijibu; ” Wewe ndio unanidai shilingi mia tatu, ngoja nikatafute chenji”. Nikamwambia asiende kutafuta chenji. Mia tatu ile abaki nayo.

Ilinitia simanzi zaidi. Hakika, msichana Rehema hana kosa. Tatizo ni la kimfumo zaidi. Ndio, tunazidi kuukumbutia ubepari, mfumo unaozidi kuongeza idadi ya masikini, idadi ya wanaoshindia mlo mmoja kwa siku, idadi ya wanaopitisha siku kama walivyoipokea. Idadi ya wasio na ajira na wasio na hakika ya kupata huduma bora za msingi za kijamii; shule na afya.

Wanaofuturisha yatima walipaswa kulipa kodi zitakazosaidia kugharamia elimu na afya za wanyonge walio wengi. Ndio, katika mfumo huu wa soko huria tulipaswa tujenge nidhamu ya kukusanya kodi ili zisaidie kuinua uchumi wa nchi na ustawi wa jamii. Iliwezekana huko nyuma, inawezekana sasa.

Maana, hii ni nchi yetu.Hatima yetu kama watu binafsi, kama vikundi vya watu na kama taifa inatutegemea sisi wenyewe. Umasikini wa watu wetu ni umasikini wetu. Kiitikadi mimi ni ‘ Social Democrat’ na bado naamini mfumo wa enzi za Mwalimu wa Ujamaa na Kujitegemea bado una nafasi katika jamii yetu. Mfumo wa Ujamaa na Kujitegemea uliofanyiwa mabadiliko ya kimsingi unaweza kutuhakikishia ulinzi wa maslahi ya nchi yetu. Ni kwa sera zenye kuhakikisha usawa wa watu. Sera zitakazohakikisha kodi inakusanywa na kutumika katika yaliyo muhimu na yenye kumsaidia pia mwananchi wa chini katika nchi yetu. Aweze kupata elimu bora na huduma bora za afya kati ya mengineyo ya msingi.

Tuazimie kuwajibika kwa pamoja kwa maslahi ya nchi yetu. Na tukifanya ajizi, tutaigeuza nchi yetu kuwa ‘nyumba ya njaa’. Na hilo ni Neno La Leo.


mjengwa
 
Maggid,

Asante kwa kipande chako hicho hapo juu.................tafadhali enedelea kuelimisha umma wa Watanzania wafanye uamuzi ulio mwema na sahihi mwisho wa mwezi Oktoba.................
 
Na Maggid Mjengwa,
Mfumo wa Ujamaa na Kujitegemea uliofanyiwa mabadiliko ya kimsingi unaweza kutuhakikishia ulinzi wa maslahi ya nchi yetu.
mjengwa

Maggid should know that Ujamaa ni kwa kulinda maslahi ya wananchi na sio kulinda maslahi ya nchi. Katika ulimwengu na Tanzania ya sasa, maslahi ya nchi na maslahi ya wananchi ni maji na mafuta.....inahitaji utaalamu wa hali ya juu na gharama kubwa kuweza kuchanganya
 
Tatizo ni la kimfumo,lakini wazazi pia tumekuwa na tabia ya kukwepa majukumu yetu na kuyahamishia kwa watoto (na ndugu pia).

Kwa mfano,mama yake kayumba anapomuacha mwanae akiosha vyombo na kuagiza akauze mayai kwa vile yeye anatoka,yeye kwa nini aifanye juhudi zote kumlinda mtoto wake na mumpatia elimu? (na unakuta mzazi mwenyewe mkorogo umekolea mabakamabaka mpango mzima).

Ben Carson ni pediatric neurosurgeon mweusi ambaye amefanikiwa sana marekani (ameandika vitabu the gifted hands na the big picture). Yeye na kaka yake walilelewa na single mother ambaye anasema alifanya kazi mbili ili kuhakikisha watoto wake wanapata elimu na alikuwa mkali kabisa na kuwaambia wanae @'no son of mine will be hopeless'.

Je, ni wazazi wangapi, pamoja na umaskini wako tayari kuhakikisha hawalali usiku kucha kuhakikisha watoto wao wanafanikiwa na kubadilisha fate yao?
 
Maggid should know that Ujamaa ni kwa kulinda maslahi ya wananchi na sio kulinda maslahi ya nchi. Katika ulimwengu na Tanzania ya sasa, maslahi ya nchi na maslahi ya wananchi ni maji na mafuta.....inahitaji utaalamu wa hali ya juu na gharama kubwa kuweza kuchanganya

Omary,

Ahsante kwa kuchangia mada hii. Kwangu mimi, maslahi ya nchi ni maslahi ya mwananchi, sioni utata katika hilo.
 
Maggid nimekuona,nadhani bado umo jamvini.kweli unapenda mno bamia.umewahi kuniambia zamani.
Neno lako la leo zuri mno.niko bkb,mbunge wa hapa ameweka gari nje ya hospitali ya mkoa anabeba maiti.lakini ndani ya hospitalini hakuna dawa. Kungekuwa na mfumo dawa zingepatikana na kungekuwa na magari ya halmashauri kwa ajili ya maiti.ilivyo sasa ni mradi wa kuombea kura.
 
Omary,

Ahsante kwa kuchangia mada hii. Kwangu mimi, maslahi ya nchi ni maslahi ya mwananchi, sioni utata katika hilo.

Kaka katika maslahi ya nchi kuna maslahi ya WELA NCHI kwanza kabla ya WANANCHI. Yaani maslahi ya wadau wakuu wa mfumo wa utawala zaidi na ujamaa ulikuja maalumu kwa ajili ya kupambana nalo hilo kutokana na kukua kwa Ubenzi ulikokuwa ukijengwa kwa jina la maslahi ya nchi
 
Ndugu yangu Maggid kama umetambua tatizo ni la kimfumo pia utakubali kwamba inabidi tuubadili mfumo huu uliopo.
Kila Mtnzania anawajibika katika hili.
Utawla wa nchi huu ambao ni kama wa kifalme sasa mi naona ndio chanzo.
Tuanze juhudi za kuubadili.
Anza wewe Maggid kwa kuondoa 'rangi za kijani' za mafisadi ziliyojaa kwenye blog yako.
Hapo utakuwa umeonyesha mfano.
 
"Ujamaa ni kwa kulinda maslahi ya wananchi na sio kulinda maslahi ya nchi."

Nashindwa kabisa kuelewa mantiki ya "Ujamaa ...sio kulinda maslahi ya nchi."

Je, corollary (deduction or an inference) yake inaweza kuleta mantiki ya "Ubepari ni kwa kulinda maslahi ya nchi na sio maslahi ya wananchi."

Haya mawazo yanatoka wapi?

Naomba kuelemishwa; nina uwezo wa kuelemika!
 
Ndugu yangu Maggid kama umetambua tatizo ni la kimfumo pia utakubali kwamba inabidi tuubadili mfumo huu uliopo.
Kila Mtnzania anawajibika katika hili.
Utawla wa nchi huu ambao ni kama wa kifalme sasa mi naona ndio chanzo.
Tuanze juhudi za kuubadili.
Anza wewe Maggid kwa kuondoa 'rangi za kijani' za mafisadi ziliyojaa kwenye blog yako.
Hapo utakuwa umeonyesha mfano.

Ndibalema,

Ahsante sana. Tatizo sio rangi za kijani blogini. Tunahitaji umakini zaidi. Nimewahi hata kuandika blogini kuwahimiza vyama na wagombea wa vyama vingine walete taarifa na picha za matukio yao. Blogu hizi zinatembelewa na wengi na CCM ni mahodari wa kutuma taarifa na picha za matukio yao. Mwingine akaniambia nizitafute mwenyewe taarifa na picha hizo! Mimi si mwandishi wa habari. Ni mwandishi wa makala na mwenye hobby ya kupiga picha. Nina kazi nyingine inayonifanya niishi.

Bado nakaribisha picha na taarifa za matukio kutoka kwa wagombea na vyama vingine mbali ya CCM. Nitazirusha bila malipo wala hiyana. Leo ni kuifikia jamii taarifa na picha hizo. Si haki kuwanyima CCM fursa hiyo kwa vile wengine hawanitumii.

Ni mtazamo wangu, tunaweza kutofautiana. Ni kawaida.
 
Ndibalema,

Ahsante sana. Tatizo sio rangi za kijani blogini. Tunahitaji umakini zaidi. Nimewahi hata kuandika blogini kuwahimiza vyama na wagombea wa vyama vingine walete taarifa na picha za matukio yao. Blogu hizi zinatembelewa na wengi na CCM ni mahodari wa kutuma taarifa na picha za matukio yao. Mwingine akaniambia nizitafute mwenyewe taarifa na picha hizo! Mimi si mwandishi wa habari. Ni mwandishi wa makala na mwenye hobby ya kupiga picha. Nina kazi nyingine inayonifanya niishi.

Bado nakaribisha picha na taarifa za matukio kutoka kwa wagombea na vyama vingine mbali ya CCM. Nitazirusha bila malipo wala hiyana. Leo ni kuifikia jamii taarifa na picha hizo. Si haki kuwanyima CCM fursa hiyo kwa vile wengine hawanitumii.

Ni mtazamo wangu, tunaweza kutofautiana. Ni kawaida.
Ndugu Maggid umenifungua masikio sasa.

Sikujua kama wapinzani wanaweza kuachia nafasi muhimu ya kujitangaza kam hii uliyoitoa wewe lakini nadhani tatizo linaweza likawa ni taarifa.

Pengine hawana habari kuwa wanaweza wakakutumia tu picha za matukio yao na wewe ukazirusha blogini bila hiyana.

Good.
 
Ndugu yangu Ndibalema,

Ahsante kwa kunielewa. Leo asubuhi nimepitia blogu kadhaa kuona kama walau nitaazima latest pictures kutoka kampeni za Prof. Lipumba, Dr Slaa na wengine. Sikupata. Kama kuna walio katika campaign teams za wahusika wenye kusoma post hii basi, email yangu ni; mjengwamaggid@gmail.com. Huu si wakati wa kuendesha kampeni 'gizani'.

Kujitangaza ni muhimu, na kuna akina sisi tulio tayari kurusha taarifa na picha bila malipo, iwe kwa vyama au wagombea.
 
Kaka,

Usiende mbali. Waliotufikisha hapa wote tunawajua. Hatujaona umuhimu wa kuwaondoa madarakani, waje wengine wenye uchungu na uzalendo kwa nchi yao, wafanye mabadiliko ya uhakika? Kama ni suala la wizi wa kura, tunao uwezo wa kulinda kura hizo zisiibiwe. Tuwapigie kura ya HAPANA mafisadi hawa, na kura ya NDIO kwa wazalendo, wakombozi wetu, watakaoleta mabadiliko. Mchuzi ukikaa jikoni zaidi ya siku tatu unachacha. Mchuzi uliopo jikoni leo una miaka hamsini, umeoza tiii, hauliki! MIE SIKUBALI!

-> Mwana wa Haki

KURA YANGU KWA CHADEMA - Diwani (Kawe), Mbunge (Kawe) na Rais! Ni HAKI YANGU!
 
Maggid,
Mkuu shukran sana kwa mchango wako na hakika sisi wepesi sana wa kuzilaumu familia zaidi hata katika majukumu makubwa ya serikali. Hii habari yako sii mpya, sote hapa kijiweni tumekutana na watoto kama huyu Rehema kila siku ya maisha yetu..

Nachokuomba mkuu wangu nenda tena kwa mtoto Rehema omba ukutane na wazazi wake uwahoji ndipo utagundua kwamba inachukua familia nzima kutafuta mlo mmoja kwa siku na bahati mbaya ni kwamba familia kama hizo hufikiria kuwa ni Mungu alowapa Umaskini huo. Kwao maisha bora ni baina yao na mwenyezi Mungu.. kidogo wanachokipata humshukuru Mungu - imetoka.
 
Back
Top Bottom