NEC ya dharura Dodoma kishindo gani?

hahaahhh.hachelewi huyo kubadili mawazo yake tena!!!.......
 
CCM inafanya uchaguzi wake wa ndani mwaka huu, kuingalia katiba ya chama wakati huu na kuifanyaia marekebisho ni hatua muhimu sana ili watakaochaguliwa waende sambamba na mabadiliko ya katiba ya chama mpya. Katika hili lilikuwepo pia suala la namna ya kuteua wajumbe wa NEC- CCM kutoka mikoani
 
Kiukweli lengo la kikao hicho sio kujadili katiba ya CCM, hoja ya kujadili katiba ya CCM sio hoja ya kidharura kihivyo!.

Lengo la kikao hicho ni ku practice Party Supremacy over the government!. Baada ya ile kanuni ya chama kushika hatamu kufutwa, kwa sasa taifa liko katika hali tete ya mgomo wa madaktari, JK ambaye ndiye mkuu wa the executive alitakiwa awe amesha intervene tangu hajaenda Davos!. Akiwa Dovos akatoa maelekezo kwa Pinda kufanya alichokifanya, aliporudi tuu hii ndio ingekuwa priority no.1 kudeal nayo ikiwemo kufanya maamuzi magumu lakini due to his weakness hakufanya lolote!.

The weak are always scared, hivyo anaitisha NEC ya CCM ili kupata baraka za maamuzi makubwa anayopanga kuyafanya ikiwemo kulivunja baraza la mawaziri au kufanya mabadiliko makubwa!.
Dah! Ni wewe mkuu!!!?
 
unategemea nini kwa rais aliyepata GPA ya 2.4 !!! very mediocre...

kama kweli wewe una elimu ya chuo kikuu utakubaliana nami kwamba GPA haina mahusiano makubwa na mafanikio katika utendaji. Zipo GPA za kweli, za chupi, za kuiba mtihani, za kuchungulia karatasi ya mtihani kwa mtahiniwa mwingine. Ni heri ukapata GPA ya 2.4 lakini ikawa halali. Wangapi wana GPA nzuri lakini wameshindwa pia kuonyesha ufanisi katika maeneo ya kazi zao?
 
kama kweli wewe una elimu ya chuo kikuu utakubaliana nami kwamba GPA haina mahusiano makubwa na mafanikio katika utendaji. Zipo GPA za kweli, za chupi, za kuiba mtihani, za kuchungulia karatasi ya mtihani kwa mtahiniwa mwingine. Ni heri ukapata GPA ya 2.4 lakini ikawa halali. Wangapi wana GPA nzuri lakini wameshindwa pia kuonyesha ufanisi katika maeneo ya kazi zao?
Naona mnapeana zamu ya kuingia humu kumwaga kinyesi siku hizi!!1
 
unategemea nini kwa rais aliyepata GPA ya 2.4 !!! very mediocre...

Mkuu Uongozi haupimwi kwa GPA ndio maana mnaibiwa na Kila kiongozi anataka kuwa na Phd. wananchi wameshaaminishwa wakishasikia Dr na Pofr fulani basi anafaa kuwa mbunge au waziri kuliko ndugu fulani..............

Unaweza kuwa na GPA nzuri usiwe na UBUNIFU na VISION ya kuzitumia hizo GPA kwa manufaa ya jamii.

Kama vijisenti msomi wa HAVARD chuo nachosifka duniani anakula dili za KIFISADI unadhani GPA inaweza kuwa na maana. Iwe ya OXFORD,UDSM au IFM GPA ni vipimo vya nadharia tu.

Ndio maana kuna watu kama bilgates hawana GPA na ni drop out yaani hawkumaliza chuo lakini wao ndiyo wanawaaaijri hao wenye GPA nzuri. Jiulize kwa nini
 
tetesi zimezidi hapa JF mods peleka thread hii hoja mchanganyiko hapa inatuchanganya tu.

Pipijojo,
Habari niliyoileta mie kuhusu JK kuahirisha ziara ya Ulaya sio tetesi, ni habari ya ndani kabisa katika ngazi ya maamuzi. Nashangaa mods wameunganisha na hii ya vikao vya sisiemu.
 
Yaani anaitisha kikao cha zarura cha nec badala ya kuitisha na serikali yake kujadili swala la madaktari kwani watanzani ndio wanaangamia..... hivi washauri wake huwa wanafikiria kweli ama wapo wapo tuu yaani inaniuma sana maswala ya muhimu watu wanaona ni mambo ya mchezomchezo tuu...

Ewe mola tunurusuru na janga hili......
 
Jk na serikali yake wako hoi,so wanachofanya ni kutapatapa.Wabunge wa CCM hawana msimamo walichofanya ni kujishushia heshima hivi sijui watarudi majimboni wakiwa na sera gani?
 
Mabadiliko haya yalenge kuirudishia CCM na vikao vyake nguvu zote zilizoporwa na baadhi ya wanachama ambao sasa wanaonekana kama miungu watu. Tunakoelekea tunataka TAASISI zenye nguvu sio watu.
 
Jamani kwanini mnaojiita Great thinkers mnapenda kubuni mambo au kuwa wataalamu wa kupiga ramli.

JK na wana CCM wana kikao chao cha dharula na ni vizuri kuwa na subra kupata agenda za kikao chao na sio kupiga ramli kujua wanataka kuongea nini.

Kumbukeni nao ni wasomi na wana mengi sana ya kuzungumza hususan usalama na hali ya nchi yenu, mikakati na maendeleo ya kampeni za ubunge arumeru na uwakilishi uzini na mengi mengineyo.

Wapeni pumzi wajinafasi na chama chaokatika vikao vyao sio kuwabanabana kwa kila kitu.
 
Back
Top Bottom