NEC ya dharura Dodoma kishindo gani?

Leo kinaanza kikao cha kamati kuu ya CCM. Kikao yaonekana kitakuwa moto kwa taarifa kuwa baadhi ya wajumbe NEC hawataki mabadiliko kwa hofu ya vyeo vyao kupunguzwa maana wengine wana vyeo zaidi ya vitano.

Mwenye zaidi atujuze
Moto utoke CCM?

Nowadays no one cares anymore about them hata wakikesha usiku kucha coz nothing significant will come from the same old stuff.
 
Haya ni miongoni mwa mamambo yanayojadiliwa. Kufanya marekebisho ambayo Wastaafu watakua na nafasi ya pekee na ya juu na si kukesha katika vikao ambavyo kwa sasa vimekua na fadhaa isiyowastahili wazee hawa na kwamba kwa mujibu wa CCM wenyewe ndani ya uongozi, haina maana kuwang'oa bali watakua na nguvu zaidi na hapa JK anajiandalia kuwa na nguvu hata baada ya kustaafu kwake kwa hiyo hawezi kufanya jambo ambalo na yeye litamgharimu.

Turejee tu na hii habari iliyozua tafsiri tofauti kati ya magazeti na Nape;

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...rume-kung%92olewa-kamati-kuu.html#post2915411
 
Ccm hawana jipya la kujadli nimewachoka hakuna cha moto matokeo ya mgomo wa walimu yameleta madhara makubwa kuliko ule wa madaktari oneni matokeo wakiweza wajadili hilo je ni vema kubeza taaluma za walimu kwakutowalipa mishahara itakayowawezesha kukabili changamoto za maisha kwa sababu raia wengine huwafagilia ******* sasa watafute kwakupeleka watoto wao walio feli ho eti kilimo kwanza pembejeo zenye ruzuku hazija fika kwa wakulima mpaka leo fika kilombero ujionee ndo utaona kama ******* wanajipya picha kamili ******* waliipata wilayani kilombero wakati wa mazishi ya aliekuwa mbunge wa viti maalumu r.mtema nakwenye vyombo vya habari hawaja onyesha uhalisia hali ilivyo kuwa mkulu mwenyewe tulishtukiwa ameshafika makaburini na mbunge wakugushi /kuchakachua alikuwa anafichama kama mwizi nilifurahi kuona hali hiyo kwa wilaya ya kilombero sasa inaonyesha hawataki ujinga wanachotaka ni mtetetezi wa wanyonge
 
KIKAO kinaendelea lakini ni Mabadiliko ya Katiba katika kubadilisha muundo wa chama katika maeneo yafuatayo



1-NEC kutoka mikoa ufutwe badala yake watoke wilayani ili kuwaweka karibu na wanachama

2-Kundi la wajumbe 85 NEC kupunguzwa

3-Kuundwa kwa chombo cha ushauri kwa Taifa kwa Wenyeviti wastaafu na Makamu Wastaafu, ambao sasa hawatakua wajumbe wa Kamati Kuu na NEC

4-Kura za maoni kufanyika Mei mwaka wa uchaguzi kupata muda kushughulikia malalamiko
5-Chombo kipya Udhibiti na nidhamu.. Ndio kile chombo kilichosemwa kwamba kitakua na mamlaka ya kuchukua maamuzi bila kusibiri vikao na kitakua na nguvu ya kuchunguza na kuhukumu.


Kwa maoni yangu ni kwamba sasa Wastaafu na Kamati ya Usalama na Maadili watalua na nguvu kubwa za ajabu katika mkakati wa kudhibiri rishwa katika uchaguzi. Je, haitakua tundu lingine la rushwa? UMAKINI WA HALI YA JUU UNAHITAJIKA KATIKA HILI.
 
Chichiemu hawana lolote wanaweweseka weweseka kutokana na ukweli kwamba Watanzania wamewagundua kwamba ni majambazi ya mchana ambayo yanakwepa kwenda jela hivyo wanajiweka sawa ili kuona hawaishii lupango kama yule jamaa wa el Masri.
 
KIKAO kinaendelea lakini ni Mabadiliko ya Katiba katika kubadilisha muundo wa chama katika maeneo yafuatayo



1-NEC kutoka mikoa ufutwe badala yake watoke wilayani ili kuwaweka karibu na wanachama

2-Kundi la wajumbe 85 NEC kupunguzwa

3-Kuundwa kwa chombo cha ushauri kwa Taifa kwa Wenyeviti wastaafu na Makamu Wastaafu, ambao sasa hawatakua wajumbe wa Kamati Kuu na NEC

4-Kura za maoni kufanyika Mei mwaka wa uchaguzi kupata muda kushughulikia malalamiko
5-Chombo kipya Udhibiti na nidhamu.. Ndio kile chombo kilichosemwa kwamba kitakua na mamlaka ya kuchukua maamuzi bila kusibiri vikao na kitakua na nguvu ya kuchunguza na kuhukumu.


Kwa maoni yangu ni kwamba sasa Wastaafu na Kamati ya Usalama na Maadili watalua na nguvu kubwa za ajabu katika mkakati wa kudhibiri rishwa katika uchaguzi. Je, haitakua tundu lingine la rushwa? UMAKINI WA HALI YA JUU UNAHITAJIKA KATIKA HILI.

Taarifa kwa vyombo vya habari

Utangulizi:
Halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi imefanya kikao chake maalum chini ya mwenyekiti wake wa taifa dr. Jakaya mrisho kikwete tarehe 12.02.2012. Katika kikao hicho halmashauri kuu ya taifa pamoja na mambo mengine imeamua;

Kufanya marekebisho ya katiba ya ccm ya 1977, toleo la 2010 na kanuni zake.

Halmashauri kuu ya taifa imeridhia marekebisho ya katiba ya CCM ya 1977, toleo la 2010 hivyo kubadili namna ambavyo wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM taifa inavyopatikana.

Kwa mujibu wa mabadiliko hayo wajumbe wa halmashauri kuu ya taifa ya CCM watakuwa katika makundi yafuatayo:-
(a) ngazi ya taifa
wajumbe 10 kutoka tanzania bara
wajumbe 10 kutoka tanzania visiwani
(b) wajumbe 10 wa kuteuliwa na mwenyekiti wa CCM taifa
(c) wajumbe wanaoingia kwa nafasi zao.
(d). Wajumbe wanaotoka kwenye vyombo vya uwakilishi
i. Wanaochaguliwa na bunge 10 (bara 8, zanzibar 2)
ii. Wanaochaguliwa na blw 5 (zanzibar 5)
(e). Wajumbe wanaochaguliwa kutoka wilayani.-221
wajumbe wa halmashauri kuu ya taifa waliochaguliwa kupitia wilaya watakuwa ni viongozi wa kazi za muda wote ili kuweka wazi zaidi wajibu wa wajumbe hao wa kuwa karibu na wanachama na kushughulikia shida zao.
(f). Wajumbe toka kwenye jumuiya za chama
i. Wanaochaguliwa na uwt 15 (bara 9, zanzibar 6)
ii. Wanaochaguliwa na uvccm 10 (bara 6, zanzibar 4)
iii.wanaotokana na wazazi 5 (bara 3, zanzibar 2)

Aidha halmashauri kuu ya taifa imeamua kuwa viongozi wakuu wastaafu ngazi ya taifa waundiwe baraza la ushauri.
Baraza hilo litakuwa na wajumbe wafuatao:-
• marais wastaafu wa jamhuri ya muungano wa tanzania ambao walikuwa wenyeviti wa ccm taifa.
• marais wastaafu wa zanzibar ambao pia walikuwa makamu wenyeviti wa ccm taifa.
• makamu wa mwenyekiti wa ccm taifa wastaafu.

Baraza litakuwa na kazi ya kutoa ushauri kwa chama cha mapinduzi na serikali zinazoongozwa na ccm, kwa madhumuni hayo hayo katika jambo mahsusi. Wajumbe wa baraza hilo wanaweza pia kualikwa ama wote au mwakilishi wao kuhudhuria vikao vya chama ngazi ya taifa.
Imetolewa na:

Nape M. Nnauye.
Katibu wa NEC wa itikadi na uenezi
 
Ndugu zangu watanzania,

Nadhani imefikia wakati tuukubali ukweli na kuuishi. Tunavyomuita Rais wetu majina ya ajabu ajabu na kumpa majina yashushayo, ndivyo hivyo atakavyokuwa.

As long As hatuwezi kumuondoa hapo alipokuwa kwa mujibu wa katiba, basi inatupasa Kutii Mamlaka iliyopo (kama maandiko yanavyotuambia).

Hebu tuache kumshusha na kumsemea mabaya siku zote, Hebu tuanze Kumuinua, Na kumpa Baraka ili abarikiwe na kuliongoza taifa letu.

Hivi unajua kama maneno yanaumba?

Hebu angalia mzazi ambaye anamuita ajina mabaya mtoto wake na kumuwazia mabaya, e.g hili toto jinga sana, wewe mbwa, litazame kwanza sura kama ng'ombe, we mtoto ndio maana hauna akili, Asilimia 95 ya watoto hao wanaishia kuwa na tabia za mbwa, majinga na yote ambayo watoto wao wamewawazia na kuwanenea.

Hebu tuache kumsema vibaya raisi wetu na kutoa mawazo ya kuendeleza nchi kuliko kulaumu, Mungu atasikia huko aliko na kutusaidia, kulaumu hakutosaidia chochote zaidi ya kuwa na hasira vichwani mwetu zinazopunguza siku za kuishi.

Ee Mungu, Tunaomba mkono wako wenye nguvu umguse Rais wetu na kuweza kuliongoza taifa letu katika nchi ya asali na maziwa.
 
Jamani jamani jamani....sijawahiona nchi hovyo kama hii.
Kigezo gani kinatumika hapo...iwenje zenj wachukue 45% ya wajumbe wote?
Ndio maana ccm maamuzi yake yamejaa vilaza wengi, full mipashoo.
 
Ndugu zangu watanzania,

Nadhani imefikia wakati tuukubali ukweli na kuuishi. Tunavyomuita Rais wetu majina ya ajabu ajabu na kumpa majina yashushayo, ndivyo hivyo atakavyokuwa.

As long As hatuwezi kumuondoa hapo alipokuwa kwa mujibu wa katiba, basi inatupasa Kutii Mamlaka iliyopo (kama maandiko yanavyotuambia).

Hebu tuache kumshusha na kumsemea mabaya siku zote, Hebu tuanze Kumuinua, Na kumpa Baraka ili abarikiwe na kuliongoza taifa letu.

Hivi unajua kama maneno yanaumba?

Hebu angalia mzazi ambaye anamuita ajina mabaya mtoto wake na kumuwazia mabaya, e.g hili toto jinga sana, wewe mbwa, litazame kwanza sura kama ng'ombe, we mtoto ndio maana hauna akili, Asilimia 95 ya watoto hao wanaishia kuwa na tabia za mbwa, majinga na yote ambayo watoto wao wamewawazia na kuwanenea.

Hebu tuache kumsema vibaya raisi wetu na kutoa mawazo ya kuendeleza nchi kuliko kulaumu, Mungu atasikia huko aliko na kutusaidia, kulaumu hakutosaidia chochote zaidi ya kuwa na hasira vichwani mwetu zinazopunguza siku za kuishi.

Ee Mungu, Tunaomba mkono wako wenye nguvu umguse Rais wetu na kuweza kuliongoza taifa letu katika nchi ya asali na maziwa.

Mkuu umesahau kuwa watu walianzia mahali tofauti kabuisa na hapo unapoongelea wewe? Wa-Tanzania mwanzoni walimwita chaguo la nani? Leo watu wanakufa Hospitalini ovyo ovyo hakuna huduma! Wanakaa vikao vya kurekebisha chama na kuunda kamati za ushauri. Katika siku zote ni leo? Hicho kikao kingelifanyika pale Muhimbili Mkuu.
 
Back
Top Bottom