kwamtoro
JF-Expert Member
- Nov 15, 2010
- 4,922
- 3,244
Naitaji maombi yenu dhidi ya huyu shetani. Nimeokoka jana nikapokelewa kwa fujo na nderemo toka katika familia yangu pamoja na majirani. Saa saba usiku nimerudi tilalila vibaya sana. Kisa kilikuwa hivi, jamaa yangu moja nilikuwa namdai laki sita. Ilipofika muda wa jioni akanipigia simu. Njoo uchukuwe pesa yako nipo sehemu fulani akanielekeza. Nikasema kweli Yesu atukuzwe, mdaiwa sugu kaniita akanilipe!!!
Nikachukuwa bodoboda huyo mpaka sehemu husika. Huwa bodaboda nikipanda lazima iwe na kiti cha kuegemea sababu nikimkumbuka Kayumba huwa nakithamini sana kichogo changu. Punde nikafika kiwanja, eee bwana ehee nikamkuta jamaa kazungukwa na wadada viwango wanakata maji. Akaniagizia nikamwambia ushidwe nimeokaka. Akaniambia kama aunywi ----- wewe nakulipa laki tatu tu na matusi kibao. Nikasema kimoyomoyo ngoja nizifakamie, kwanza sijasimama kiimani.
Nikaanza kupiga bia mara valuu baada ya kuchangamka tu nikadai pesa zangu. Tukaenda chobingo jamaa akanihesabia changu na kwa bahati nzuri alikuwa pombe sana, alinipa laki sita sabini badala ya laki sita kamili. Mishale ya saa sita na nusu nikachukuwa cab mpaka nyumbani nikagonga geti kipombe pombe nikafunguliwa then nikaingia sebuleni hapo ndipo nilipo zima mazima. Saa tatu asubuhi kustuka nimezungukwa na wale walionipongeza pamoja na yule aliye niongoza sala ya toba.
Nikachukuwa bodoboda huyo mpaka sehemu husika. Huwa bodaboda nikipanda lazima iwe na kiti cha kuegemea sababu nikimkumbuka Kayumba huwa nakithamini sana kichogo changu. Punde nikafika kiwanja, eee bwana ehee nikamkuta jamaa kazungukwa na wadada viwango wanakata maji. Akaniagizia nikamwambia ushidwe nimeokaka. Akaniambia kama aunywi ----- wewe nakulipa laki tatu tu na matusi kibao. Nikasema kimoyomoyo ngoja nizifakamie, kwanza sijasimama kiimani.
Nikaanza kupiga bia mara valuu baada ya kuchangamka tu nikadai pesa zangu. Tukaenda chobingo jamaa akanihesabia changu na kwa bahati nzuri alikuwa pombe sana, alinipa laki sita sabini badala ya laki sita kamili. Mishale ya saa sita na nusu nikachukuwa cab mpaka nyumbani nikagonga geti kipombe pombe nikafunguliwa then nikaingia sebuleni hapo ndipo nilipo zima mazima. Saa tatu asubuhi kustuka nimezungukwa na wale walionipongeza pamoja na yule aliye niongoza sala ya toba.