Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 464
- 687
Ukweli waweza kuwa mchungu, lakini ndio ukweli hata kama hatuupendi. Na ukweli mchungu mojawapo kwa Balozi Polepole na wenzake, ni kuwa Dr. Samia ndio mgombea wetu wa urais.
Mwalimu alituasa wana CCM, kuwa akishapatikana mgombea wa CCM, wana CCM wote lazima tumtetee. Katiba ya CCM imeenda mbali zaidi kwakutamka kuwa, mwana CCM, kumpinga mgombea wa CCM ni USALITI.
Vitendo au maneno ya kumbomoa Dr. Samia wakati huu, vinaibomoa CCM pia. Tafakari, kama tukimpaka matope Dr. Samia sasa, nani atampigia kura October 29? Na akikosa hizo kura, Je, CCM itaendelea kuwepo?
Historia ni mwalimu mzuri sana. Katika Afrika, Historia inatufundisha kuwa, chama tawala kikishindwa uchaguzi tu kinakufa. Kwa maneno mengine ni kuwa, kumpinga mgombea Rais wa CCM, ni kama kuitakia kifo CCM. Rai yangu ni kuwa, hata kama hatujaridhika vipi, ni mwiko mambo ya chumbani kuyaweka hadharani.
CCM ni urithi wa watanzania, ndio maana pamoja na matatizo yake yote, hitimisho la baba wa Taifa lilikuwa, "Bila CCM madhubuti, Tanzania itayumba"
Mwalimu alituasa wana CCM, kuwa akishapatikana mgombea wa CCM, wana CCM wote lazima tumtetee. Katiba ya CCM imeenda mbali zaidi kwakutamka kuwa, mwana CCM, kumpinga mgombea wa CCM ni USALITI.
Vitendo au maneno ya kumbomoa Dr. Samia wakati huu, vinaibomoa CCM pia. Tafakari, kama tukimpaka matope Dr. Samia sasa, nani atampigia kura October 29? Na akikosa hizo kura, Je, CCM itaendelea kuwepo?
Historia ni mwalimu mzuri sana. Katika Afrika, Historia inatufundisha kuwa, chama tawala kikishindwa uchaguzi tu kinakufa. Kwa maneno mengine ni kuwa, kumpinga mgombea Rais wa CCM, ni kama kuitakia kifo CCM. Rai yangu ni kuwa, hata kama hatujaridhika vipi, ni mwiko mambo ya chumbani kuyaweka hadharani.
CCM ni urithi wa watanzania, ndio maana pamoja na matatizo yake yote, hitimisho la baba wa Taifa lilikuwa, "Bila CCM madhubuti, Tanzania itayumba"