Wasalaam,
Mwenyezi Mungu ametuamsha salama kabisa wakuu.
Nina changamoto ya ndoto zinazonisumbua sana, zipo za aina tofauti 5 isipokuja hii itakuja hii. Zipo hivi:
Naota nafanya mapenzi na jitu nisiloifahamu. Hapa linaweza nibadilisha niwe mwanaume lenyewe linakuwa la kike au linakuwa la kiume linaniingilia.
Naota nakimbizwa na N'gombe mkuubwa mweusi mwenye pembe Kali sana.. Huwa nakimbia sana na linaponikosa ghafla hubadilika na kuwa binadamu na kuanza kunirushia mishale mingi kwa haraka ila mungu mwema halijawahi kunichoma na mshale.
Naota nataka kung'atwa na nyuki...! Lakini pia naota kuna majoka yananikimbiza ila moja ya majoka haya hujificha sehemu/ kama kujibanza ili lisionekane.
Naota nimetekwa..hii ndio niliyoiota hata leo! Hapa huwa nakuwa na wakati mgumu sana wa kukabiliana na mtekaji.. Nimekimbia sana nimeomba wapita njia msaada lakini Mzee mmoja alisema nastahili kutekwa, .. Nilijaribu kumkimbia mtekaji na pikipiki ila kabla sijapanda pikipiki nae alichukua yake akaanza kumfukuza bodaboda niliyemkodi.. Tumesumbuana sana ila mwisho kuna wanaume nilikutana nao na mmoja wao akanishika mkono yule mtekaji akakubali kushindwa.
Wakuu hii ni hali y kawaida au ni mini... Hiizi ndoto zimekuwa na muda mrefu kama miaka minne .. Ila miaka ya hivi karibuni linakuwa sugu.
Je wewe unaota ndoto za aina moja tu? Nakaribisha maoni na ushauri nifanyeje ili nisiote tena?
Mwenyezi Mungu ametuamsha salama kabisa wakuu.
Nina changamoto ya ndoto zinazonisumbua sana, zipo za aina tofauti 5 isipokuja hii itakuja hii. Zipo hivi:
Naota nafanya mapenzi na jitu nisiloifahamu. Hapa linaweza nibadilisha niwe mwanaume lenyewe linakuwa la kike au linakuwa la kiume linaniingilia.
Naota nakimbizwa na N'gombe mkuubwa mweusi mwenye pembe Kali sana.. Huwa nakimbia sana na linaponikosa ghafla hubadilika na kuwa binadamu na kuanza kunirushia mishale mingi kwa haraka ila mungu mwema halijawahi kunichoma na mshale.
Naota nataka kung'atwa na nyuki...! Lakini pia naota kuna majoka yananikimbiza ila moja ya majoka haya hujificha sehemu/ kama kujibanza ili lisionekane.
Naota nimetekwa..hii ndio niliyoiota hata leo! Hapa huwa nakuwa na wakati mgumu sana wa kukabiliana na mtekaji.. Nimekimbia sana nimeomba wapita njia msaada lakini Mzee mmoja alisema nastahili kutekwa, .. Nilijaribu kumkimbia mtekaji na pikipiki ila kabla sijapanda pikipiki nae alichukua yake akaanza kumfukuza bodaboda niliyemkodi.. Tumesumbuana sana ila mwisho kuna wanaume nilikutana nao na mmoja wao akanishika mkono yule mtekaji akakubali kushindwa.
Wakuu hii ni hali y kawaida au ni mini... Hiizi ndoto zimekuwa na muda mrefu kama miaka minne .. Ila miaka ya hivi karibuni linakuwa sugu.
Je wewe unaota ndoto za aina moja tu? Nakaribisha maoni na ushauri nifanyeje ili nisiote tena?
