X_INTELLIGENCE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2014
- 9,677
- 12,244
Ndugu zangu nawasalimu Kwa Jina la jamhuri ya Tanganyika. Mimi ni muumini wa dini ya kiislam Ambae Kwa kiasi Fulani naweza kusema Imani yangu imeteteleka kutokana na baadhi ya matendo ya watu wa Imani ambao nilikuwa na waamini sana ila mwisho wa siku wanafanya mambo kinyume na maelekezo ya Dini.
Katika dini zote tunaamlishwa kufanya mema na kukatazwa kufanya mabaya hivyo sipingani na Imani ya mtu wowote hata kama Hana dini kama afanyi mabaya huyo ni mtu wa Mungu.
Kwenye dini yetu ya kiislam Kuna maamrisho mengi sana mema Ikiwemo.
√ Kusaidia Yatima
√ kuwasaidia wazazi
✓ kusaidia wenye huitaji
√ kutoa sadaka
✓ kufuturisha kwa waliofunga mwezi mtukufu.
Hizo ni baadhi. matendo mema ya sisi waislam yamegawanyika kwenye makundi mawili.
1. Faradhi
2. Sunna
Ili swala la kuoa lipo kwenye kundi la kwanza la faradhi. Ila ili ndoa iwe ndoa Kuna misingi ya kuzingatiwa.
Muhtadha wa andiko langu upo kwenye hizi ndoa za wake Zaidi ya mmoja. Ambayo Mimi naiweka kwenye kundi la sunna maana imeandikwa kuwa "muoe wake Hadi wanne kama mna uwezo".
Hivyo usipo oa wake wengi sio dhambi ila kikubwa ni lazima uwe na uwezo.
Ndoa za wake wengi Kwa nchi yetu changa kiimani, changa kimaendeleo na changa ki uelewa HAZIFAI.
Wenzetu WAarabu wanaouweza wa kuoa Zaidi ya wake mpaka wa 4 kwasababu wanao uwezo kipesa na dini imeanzia Kwao hivyo wanauelewa mpana sana wa Hilo swala.
Watanzania wengi vipato vyetu ni vya kawaida sana hivyo kuoa wake wengi ni sawa na kuipa familia UMASIKINI wa kujitakia.
Kwenye andiko langu hili
Najuta kumtia umasikini Mama yangu
Wachangiaji wengi walinilalamikia kuwa kwanini andiko lote hakuna sehemu nimemtaja baba😭🙆😭🙆
Mimi nimelelewa na wazazi wote wawili baba na mama na Nina mshukuru Mungu sana wazazi wangu wote Bado wapo hai na wanaishi pamoja.
Kitu kilichopelekea nisimgusie mzazi wangu wa kiume kwenye andiko langu la awali ni ile hali ya yeye kuwa na wanawake wengi. Najua nakosea Kwa Mila zetu kuzungumza hivi ila mtanisamehe sizungumzi Kwa Nia mbaya.
Kwa uwezo wa kiTanzania kuanzia cheo cha mkuu wa mkoa kushuka chini awana uwezo wa kumudu kuhudumia wanawake Zaidi ya mmoja.
Hizi ndoa zinaleta mateso makubwa sana Kwa watoto na Huwa zinaleta matabaka sana. Kuna familia Moja kati ya hizo itajaaliwa. Harafu itaona kama inapendelewa.
Kuishi bila kupendelea haiwezekani hivyo Kuna mke atapendelewa yeye na watoto Wake. Hapo ndipo balaa litapoanza kujitokeza.
Baba yangu Kwa nafasi aliyokuwa nayo alikuwa na uwezo wa kuhakikisha watoto Wake wote wanasoma na kupata kazi endapo angekuwa na familia Moja.
Ila Hilo ameshindwa kulifanya kwasababu ya kuhusudu ndoa za wake wengi kitu kilichopelekea baadhi ya watoto kutelekezwa. 😭😭😭
Waliosema ndugu zako wa kweli ni watoto wako wa kuwazaa hawakukosea ila sio watoto wawe wengi kupita kiasi.
Kibinaadam ukiwa na watoto 3 au 4 hivi wanatosha sana. Sasa unakuta mfanyakazi analipwa milioni 1. Ana wake Zaidi ya 4 ana watoto 16. Huku ndugu zake dada, kaka na wadogo zake wote wanamtegemea mtu kama huyu anaweza kweli kuwasaidia watoto Wake.
Ifike kipindi serikali itoe tamko baadhi ya maandiko ya Dini yazingatiwe yasifuatwe kwani yanadhalisha kizazi chenye chuki na visasi na kulirudisha Taifa nyuma😭😭😭
NAPINGA NDOA ZA WAKE WENGI.
Katika dini zote tunaamlishwa kufanya mema na kukatazwa kufanya mabaya hivyo sipingani na Imani ya mtu wowote hata kama Hana dini kama afanyi mabaya huyo ni mtu wa Mungu.
Kwenye dini yetu ya kiislam Kuna maamrisho mengi sana mema Ikiwemo.
√ Kusaidia Yatima
√ kuwasaidia wazazi
✓ kusaidia wenye huitaji
√ kutoa sadaka
✓ kufuturisha kwa waliofunga mwezi mtukufu.
Hizo ni baadhi. matendo mema ya sisi waislam yamegawanyika kwenye makundi mawili.
1. Faradhi
2. Sunna
Ili swala la kuoa lipo kwenye kundi la kwanza la faradhi. Ila ili ndoa iwe ndoa Kuna misingi ya kuzingatiwa.
Muhtadha wa andiko langu upo kwenye hizi ndoa za wake Zaidi ya mmoja. Ambayo Mimi naiweka kwenye kundi la sunna maana imeandikwa kuwa "muoe wake Hadi wanne kama mna uwezo".
Hivyo usipo oa wake wengi sio dhambi ila kikubwa ni lazima uwe na uwezo.
Ndoa za wake wengi Kwa nchi yetu changa kiimani, changa kimaendeleo na changa ki uelewa HAZIFAI.
Wenzetu WAarabu wanaouweza wa kuoa Zaidi ya wake mpaka wa 4 kwasababu wanao uwezo kipesa na dini imeanzia Kwao hivyo wanauelewa mpana sana wa Hilo swala.
Watanzania wengi vipato vyetu ni vya kawaida sana hivyo kuoa wake wengi ni sawa na kuipa familia UMASIKINI wa kujitakia.
Kwenye andiko langu hili
Najuta kumtia umasikini Mama yangu
Wachangiaji wengi walinilalamikia kuwa kwanini andiko lote hakuna sehemu nimemtaja baba😭🙆😭🙆
Mimi nimelelewa na wazazi wote wawili baba na mama na Nina mshukuru Mungu sana wazazi wangu wote Bado wapo hai na wanaishi pamoja.
Kitu kilichopelekea nisimgusie mzazi wangu wa kiume kwenye andiko langu la awali ni ile hali ya yeye kuwa na wanawake wengi. Najua nakosea Kwa Mila zetu kuzungumza hivi ila mtanisamehe sizungumzi Kwa Nia mbaya.
Kwa uwezo wa kiTanzania kuanzia cheo cha mkuu wa mkoa kushuka chini awana uwezo wa kumudu kuhudumia wanawake Zaidi ya mmoja.
Hizi ndoa zinaleta mateso makubwa sana Kwa watoto na Huwa zinaleta matabaka sana. Kuna familia Moja kati ya hizo itajaaliwa. Harafu itaona kama inapendelewa.
Kuishi bila kupendelea haiwezekani hivyo Kuna mke atapendelewa yeye na watoto Wake. Hapo ndipo balaa litapoanza kujitokeza.
Baba yangu Kwa nafasi aliyokuwa nayo alikuwa na uwezo wa kuhakikisha watoto Wake wote wanasoma na kupata kazi endapo angekuwa na familia Moja.
Ila Hilo ameshindwa kulifanya kwasababu ya kuhusudu ndoa za wake wengi kitu kilichopelekea baadhi ya watoto kutelekezwa. 😭😭😭
Waliosema ndugu zako wa kweli ni watoto wako wa kuwazaa hawakukosea ila sio watoto wawe wengi kupita kiasi.
Kibinaadam ukiwa na watoto 3 au 4 hivi wanatosha sana. Sasa unakuta mfanyakazi analipwa milioni 1. Ana wake Zaidi ya 4 ana watoto 16. Huku ndugu zake dada, kaka na wadogo zake wote wanamtegemea mtu kama huyu anaweza kweli kuwasaidia watoto Wake.
Ifike kipindi serikali itoe tamko baadhi ya maandiko ya Dini yazingatiwe yasifuatwe kwani yanadhalisha kizazi chenye chuki na visasi na kulirudisha Taifa nyuma😭😭😭
NAPINGA NDOA ZA WAKE WENGI.