Ndoa ya serikali V/s ndoa ya kanisani

Ndoa ya serikali V/s ndoa ya kanisani

nyonga nyonga

Member
Joined
Oct 2, 2013
Posts
27
Reaction score
4
Habari !

Mie ni mkristo, ninataka kufunga ndoa. Ila taratibu za ufungaji wa ndoa zetu ni ndefu. Naomba kuelimishwa ama kujuzwa uhalali wa ndo za kiserikali kuhusiana na imani ya ki kristo.

Namaanisha, unapokua umefunga ndoa kanisani, unakua hauzini ila inakua halali kwako kukutana na mkeo au mumeo.

Nikifunga serikalini, kwasababu sio ya kidini nitakua nazini ama nayo inapokelewa na Mungu na kua halali kama hiyo ya kanisani?

Jioni njema.
 
Mimi ni mkristo tena RC, ninachojua mimi ni kuwa kuna aina tatu za ndoa 1. Ndoa ya kanisani 2. Ndoa ya serikalini 3. Ndoa ya kimila na aina zote zinakubalika. Aina ya kwanza na ya pili wanakupa cheti kile kile cha ndoa isipokuwa cha kanisani kina mihuri ya kanisa na cha bomani kina mihuri ya bomani. Kama utaamua kufunga ya serikalini endelea tu ila ukitaka kuibariki kanisani watatumia cheti kile kile ulichopewa bomani ila kitagongwa mihuri ya kanisa na sahihi za alieibariki. Mwisho hongera sana kwa uamuzi wa kuachana na kambi ya ukapera.
 
Kwangu pia ni utata je kwetu wakatoliki hata kukomunika endapo umefunga hyo ndoa ya ser.hapo pakoje?
 
Mkuu naomba usome haya maelezo kwa kina.... Nimeyatoa mahali...

UFAHAMU KUHUSU NDOA
Ndoa ni nini?
Ndoa inaweza kutafsiriwa kwa namna nyingi kulingana na kusudi la mhusika na lengo la tafsiri hiyo. Katika tafsiri za kisheria Ndoa inatambulika kama mkataba wa kisheria ambao unaweza kuvunjwa wakati wowote. Kwa sheria za Tanzania Ndoa ni mkataba unaofungwa kwa hiari baina ya Mwanamume na Mwanamke ambao wanakusudia kuambatana na kuishi pamoja kama mke na mume.

Kwa kuwa si kusudi letu kutafakari sheria za nchi zinasema nini kuhusu Ndoa, tungependa kujikita zaidi katika maana ya Ndoa kwa imani ya kikristo ambayo msingi wake unajengwa katika neno la Mungu. Hata hivyo tunapenda kuweka wazi kwamba Ndoa ni suala la kisheria, na ni muhimu sana kwa wanandoa kutambua kwamba zipo taratibu za kisheria zilizowekwa na serikali zinazosimamia masuala ya Ndoa. Kwa kuwa tumefanyika wana wa Mungu, mwenendo wetu na maisha yetu ya Ndoa yanaongozwa na imani yetu kwa Mungu na si sheria za kibinadamu.

Katika imani ya kikristo, Ndoa inaweza kutafsiriwa kama “AGANO KATI YA MWANAMKE NA MWANAMUME AMBAO WAMEKUSUDIA KWA HIARI KUAMBATANA NA KUISHI PAMOJA KAMA MKE NA MUME KWA SIKU ZOTE ZA MAISHA YAO.” Jambo la msingi kulitambua hapa ni kwamba Ndoa ya kikristo ni AGANO. Kuna tofauti kubwa kati ya kile kinachoitwa “AGANO” na “MKATABA” kimsingi agano ni zaidi ya mkataba kwa namna nyingi. Zifuatazo ni baadhi ya tofauti za msingi kati ya agano na mkataba;
AGANO
• Hufungwa katika msingi wa kuaminiana, kuheshimiana na kuthamini uhusiano uliopo baina ya pande mbili. Wanaoingia agano wanaaminiana kuamua kwa dhati kujitoa kuishi katika agano siku zote za maisha yao.
• Agano linaunganisha utu wa ndani wa mtu katika mahusiano, hupelekea kuunganisha watu katika mahusiano yenye uwajibikaji usio na kikomo.
• Agano hushuhudiwa na Mungu ambaye pia ndiye mdhamini wa agano la Ndoa. Hii ndiyo sababu baadhi ya watu katika tamaduni zao wanapoingia agano huapa kwa jina la Mungu wanayemwamini. (Mfano agano la urafiki wa damu katika mila za kiafrika na tamaduni nyingine)
• Agano hudhihirisha, kuweka wazi na kuimarisha mambo ya msingi yanayojenga uhusiano wa kudumu/usiovunjika mpaka kifo kiwatenganishe.
MKATABA
• Mkataba hufungwa katika hali ya kutokuaminiana, na hivyo wanaoingia mkataba huweka bayana taratibu zitakazoongoza na kusimamia mahusiano yao ikiwemo majukumu ya kila upande unaoingia katika mkataba.
• Mkataba unaunganisha huduma inayotolewa na mtu na si utu wake wa ndani. Kwa lugha nyingine, mkataba huainisha na kuweka wazi mipaka ya uwajibikaji baina ya watu wanaohusika.
• Mkataba hushuhudiwa na wanadamu na ndio wanaokuwa mashahidi wa mkataba uliofungwa.
• Mkataba huainisha na kuweka wazi njia halali za kuvunja uhusiano baina ya watu wanaohusika na mkataba huo.
 
kwaiyo ya serikalini haina baraka?

Mimi ni mkristo tena RC, ninachojua mimi ni kuwa kuna aina tatu za ndoa 1. Ndoa ya kanisani 2. Ndoa ya serikalini 3. Ndoa ya kimila na aina zote zinakubalika. Aina ya kwanza na ya pili wanakupa cheti kile kile cha ndoa isipokuwa cha kanisani kina mihuri ya kanisa na cha bomani kina mihuri ya bomani. Kama utaamua kufunga ya serikalini endelea tu ila ukitaka kuibariki kanisani watatumia cheti kile kile ulichopewa bomani ila kitagongwa mihuri ya kanisa na sahihi za alieibariki. Mwisho hongera sana kwa uamuzi wa kuachana na kambi ya ukapera.
 
charminglady , asante kwa mchango wako. Hasa nataka kujua ya Kiserikali ukifunga (sitaki kuuita ya mkataba kwasababu kuna watu wameanza na hiyo hadi umauti ukawatenganisha) unakua mbele za Macho ya Mungu unahesabika kama mzinzi ama? na kama kwa RC nitaruhusiwa hata kukomunika?
 
Last edited by a moderator:
Sio kwamba ndoa ya serikalini haina baraka. Kama ingekuwa hivyo basi wasingeweza kutumia cheti kile kile wangekupa kingine, pia vyeti vya ndoa vinavyotumika kanisani vimetolewa na serikali kanisa halina vyeti vyake vya ndoa.
 
Maelezo yote yaliyotolewa ni sahihi ndugu mtoa hoja inabakia wewe kuamua wapi ukafunge ndoa. Kama kweli wewe ni mkristo na mwenzako pia ni mkristo fungeni kanisani japo cheti ni 1 kwa ndoa zote za bomani, kanisani na msikitini.

Tofauti ni mihuri na ila zaidi imani inayoambatana na ndoa kwa Mujibu wa kila dini. Japo hujaweka wazi kwanini unauliza hilo nataka nikupe mifano kadhaa inayofanya watu wafunge ndoa za bomani.

Huenda ikakusaidia hicho ulichosita kueleza na pia itasaidia wengine.

1 Tofauti za imani kati ya waoaji

Unakuta binti mkristo na mwanaume muislamu ila wamependana na kila mtu anataka kubaki na imani yake. Hapo inabidi muende bomani.

2.misimamo ya wazazi.

Unakuta binti amekubali kubadili dini yake kumfuata mumewe au Mume kakubali kumfuata mchumba na wapo tayari kuwa imani moja, lakini wazazi wanaingilia kati kuanza vitisho na laana. Hapo sasa cha kufanya ili mtoke salama ni kufunga bomani ili wote waridhike.

Baada ya hapo wahusika inawapasa mkabariki ndoa yenu kanisani maana sasa mpo wenyewe. Kama ni msikitini nendeni mfuate imani zenu mlivyokubaliana kwakuwa hapo uamuzi ni wenu.

Hiyo inasaidia kufunga ndoa kwa amani bila kukwaza wengine japo wengine pia hawapendi ndo za bomani. Ila haya maisha tusishurutishwe sana na imani. Wakati mwingine tunashuhudia mtu ndoa imefungwa kanisani lakini ndo ndoa mbovu kila siku vurugu.

Hapa nataka kusema kwamba kinachodumisha ndoa ni hekima, busara na mapenzi ya dhati kati ya wanandoa wala si imani za dini zetu. Si unaona ndoa ya Emmanuel mbasha na mkewe. Japo si vizuri kutolea mfano wakati huu.

Ndoa ni maelewano kati ya wawili. Note: Tanzania kwasababu ya misingi ya Taifa letu kuwa si nchi ya dini bali kila mtu ana imai yake, imefanya wengi tuchangamane sana, tumeoana wakristo na waislamu na tunaishi kwa amani bila kubaguana.

Hivyo mtu asikukwaze na wala usimbague mtu kwa imani yake au usimwache mchumba uliyempenda kwasababu ya dini yake. Safari ya mbinguni ni ya kila Mtu na nafsi yake siku ya mwisho! Kila la kheri katika maamuzi yako!
 
Na ndio maana ukishafunga ndoa ya serikalini haitafungishwa ndoa nyingine ten kanisani ila tu utapeleka vyeti vyako vya ndoa kanisani.
 
Asante mkuu, nimekupata.

Sio kwamba ndoa ya serikalini haina baraka. Kama ingekuwa hivyo basi wasingeweza kutumia cheti kile kile wangekupa kingine, pia vyeti vya ndoa vinavyotumika kanisani vimetolewa na serikali kanisa halina vyeti vyake vya ndoa.
 
Nachojua Nikwamba Serikali Haina Dini,sasa Wewe Km Unadini Iweje Uende Ukafunge Ndoa Sehemu Ambayo Haina Dini?Nenda Kafuate Maandiko Ya Din Yako Ndugu
 
Nachojua Nikwamba Serikali Haina Dini,sasa Wewe Km Unadini Iweje Uende Ukafunge Ndoa Sehemu Ambayo Haina Dini?Nenda Kafuate Maandiko Ya Din Yako Ndugu

kabla hizi dini zilizoletwa na meli hazijaja je babu zako na mabibi zako walikuwa wanazini?
 
charminglady , asante kwa mchango wako. Hasa nataka kujua ya Kiserikali ukifunga (sitaki kuuita ya mkataba kwasababu kuna watu wameanza na hiyo hadi umauti ukawatenganisha) unakua mbele za Macho ya Mungu unahesabika kama mzinzi ama? na kama kwa RC nitaruhusiwa hata kukomunika?

Mkuu hapana kabisa, make NDOA kama ilivyotafsiri yake ni Muunganiko kwa wtu wawili waliopata baraka toka pande zote mbili. Yaani wazazi, na wazazi wanamwakiliza Mungu hapa duniani make wazazi ni kielelezo cha Mungu. Kama umepata baraka za wazazi pande zote hata kwa Mungu baraka pia zimetoka na ni halali kabisa. Ndio maana wazazi huwa wanatoa baraka ambazo kwako ni maneno yanayomwakilisha Mungu.

kama Biblia inavyosema waheshimu baba yako na mama yako upate heri duniani. Ina maana yale ni maneno ya Mungu mwenyewe! Kuwa na amani kabisa mkuu ndio maana hata Ndoa ya Serikali inakubalika kanisani.
 
kwaiyo ya serikalini haina baraka?

Kwa kanisani jibu ni 'NDIYO' Kanisa halitambui ndoa ya bomani wala ya kimila. Lazima mkifika kanisani muibariki hiyo ndoa ya bomani ili itambulike kiroho. Hope nimesomeka
 
daaaah, wadau nimejaribu kufuatilia majadiliano kimsingi naeza nikasema yote hivi, ila nazidi kupata kigugumizi hasa kwa aliyeleta mada hii kwamba kuna wanaomsapoti na pia kuna wanamhepa wakisisitiza ndoa ya kanisani, ila mimi kwa maoni yangu ni kwamba, hili jambo ni la watu wawili yaani wanaotaka kuingia ktk maisha ya mume na mke, na sasa kwa kuwa ni la watu wawili yan kama kilingana na maridhiano yao wawili ni kufunga cjui ya kidini wafunge tuu, kama ni ya kiserikali au kimila its ok wafunge tuu ilimradi wote wawili wameridhia huku Mungu wakimtanguliza mbele kwani Mungu sisi sote ni watoto wa kwake yeye na habagui na hata hivo mkisharidhia na kufunga ndoa na kuwa mke na mume, anayependa na asiyependa wote watabadilika na kuwa kitu kimoja yaan wanie mamoja iwe ni wazazi au ndugu wengine mana hakuna jinc tena kwan walioana cjui kidn , kiserikali au kimila wote wana ndoa tena halali na wao kama wao gurudumu la maisha liko mikononi mwao na si vinginevyo. niwapongeze wote kwa mjadala mzuri na wenye hekima na busara ndani yake na nimpongeze pia mwenye kuleta mada nimejifunza mengi. pamoja sana.
 
kabla hizi dini zilizoletwa na meli hazijaja je babu zako na mabibi zako walikuwa wanazini?


na kweli ni swali nzur ila mm nina iman hawakuwa wakizini tena ndoa zao ziliduma mamiaka nenda rudi na syo kama hz za kidijitali za leo ndoa tjen kesho habari ya mjini unasikia wameshatalakiana.
kaaaaah ni thidaaaaaaa.
 
Back
Top Bottom