Daudi1
JF-Expert Member
- Dec 14, 2013
- 8,758
- 8,631
Habari wanakijiji wenzangu, matumaini mko salama kabisa, bila kupoteza muda nielekee kwenye mada
Kumekuwa na wimbi la watu wengi hasa wanandoa kueleza negatives za ndoa kiasi kupelekea wengine kukata tamaa ama kuogopa lakini ngoja niwaelezeni kitu
Ndoa ni tamu sana hasa kama umepata mtu sahihi, kwanza mfanye mke au mume kuwa rafiki yao ambaye unaweza kushare mambo yote yawe ya Furaha au huzuni hii itamfanya mwenzako kuwa huru kushauri lolote kwa kauli nzuri, ikumbukwe hakuna binadamu mkamilifu hivyo mapungufu ya mwenzio chukulia kama kilema sio ndio fimbo ya kumchapia, unaweza kupata mwanamke mrembo lakn kitandani hajui chukulia hiyo ni changamoto na usimuumize kwa sababu ya udhaifu huo utafurahia ndoa yako.
Mwanamke akijua majukumu yake na akaweza kuyatimiza licha ya kuajiriwa, kuheshimiana licha ya kuwa na utofauti wa kipato, kuwe na mipaka mambo ya kazini yaishie kazini uwapo nyumbani lazima familia iwe imara na ndoa itafurahiwa na kila mmoja.
Makwazo hayakosekani, mkikaa pamoja na kuelezana kwa upendo mkiepuka maneno makali ya kuumiza lakini pia kuachilia kwa kusamehe yaliyopita, mtafurahia
Michepuko kwa wanaume husababishwa na mwanamke kutokaa kaa katika nafasi au tamaa tu, kama mwanamke atakaa katika nafasi yake, kupunguza gubu kuna nafasi kubwa kwa mwanaume kutulia au kupata mchepuko mstaarabu ambaye hatavuruga ndoa.
Mungu ni kiongozi mkuu wa ndoa ukiambatana naye katika kila hatua lazima ufurahie ndoa yako wengine watalalamika kuhusu ndoa zao wewe utakuwa unashangaa mambo ya naenda
Mwisho vijana msiogope ndoa, ni tamu sana kama utapata mtu sahihi kama nilivyoeleza hapo juu, usikubali kukatishwa tamaa kwa sababu et ndoa ya fulani inasumbua ukajua na yako itakuwa hivyo nooo, kila mtu amezaliwa kivyake ingekuwa hivyo tungeogopa kusoma eti kisa Fulani amefeli mtihani, Muwe na siku njema.
Kumekuwa na wimbi la watu wengi hasa wanandoa kueleza negatives za ndoa kiasi kupelekea wengine kukata tamaa ama kuogopa lakini ngoja niwaelezeni kitu
Ndoa ni tamu sana hasa kama umepata mtu sahihi, kwanza mfanye mke au mume kuwa rafiki yao ambaye unaweza kushare mambo yote yawe ya Furaha au huzuni hii itamfanya mwenzako kuwa huru kushauri lolote kwa kauli nzuri, ikumbukwe hakuna binadamu mkamilifu hivyo mapungufu ya mwenzio chukulia kama kilema sio ndio fimbo ya kumchapia, unaweza kupata mwanamke mrembo lakn kitandani hajui chukulia hiyo ni changamoto na usimuumize kwa sababu ya udhaifu huo utafurahia ndoa yako.
Mwanamke akijua majukumu yake na akaweza kuyatimiza licha ya kuajiriwa, kuheshimiana licha ya kuwa na utofauti wa kipato, kuwe na mipaka mambo ya kazini yaishie kazini uwapo nyumbani lazima familia iwe imara na ndoa itafurahiwa na kila mmoja.
Makwazo hayakosekani, mkikaa pamoja na kuelezana kwa upendo mkiepuka maneno makali ya kuumiza lakini pia kuachilia kwa kusamehe yaliyopita, mtafurahia
Michepuko kwa wanaume husababishwa na mwanamke kutokaa kaa katika nafasi au tamaa tu, kama mwanamke atakaa katika nafasi yake, kupunguza gubu kuna nafasi kubwa kwa mwanaume kutulia au kupata mchepuko mstaarabu ambaye hatavuruga ndoa.
Mungu ni kiongozi mkuu wa ndoa ukiambatana naye katika kila hatua lazima ufurahie ndoa yako wengine watalalamika kuhusu ndoa zao wewe utakuwa unashangaa mambo ya naenda
Mwisho vijana msiogope ndoa, ni tamu sana kama utapata mtu sahihi kama nilivyoeleza hapo juu, usikubali kukatishwa tamaa kwa sababu et ndoa ya fulani inasumbua ukajua na yako itakuwa hivyo nooo, kila mtu amezaliwa kivyake ingekuwa hivyo tungeogopa kusoma eti kisa Fulani amefeli mtihani, Muwe na siku njema.