elvee
JF-Expert Member
- Jan 27, 2017
- 1,110
- 1,629
HahahaaHahaha unataka ujioe aisee
HahahaaHahaha unataka ujioe aisee
Hehe eti mkuu umemuelewa huyo?Hahahaa
Nashukuru kwa kupigilia msumariMtoa hoja Mungu wetu si wa michanganyo. Kama mtu amekuwa mwaminifu kwa Mungu hilo suala la mchepuko mstarabu halipo, huo ni uzinzi tu kama ilivyo kahaba/mzinzi yeyote hakuna cha ustarabu, atendaye dhambi ni wa ibilisi
Si kweli pengine huyo uliyenaye ndio yuko hivyo haimaanishi wote wako hivyo wapo wanaofurahia huo mwisho wa mwezi na familia zao, kaa na mwenzio chini tumia kila namna mpaka amekuweka ndani ujue una nafasi yako kwake itumie hiyoMwanaume ni mbaya sana katika ndoa hasa kila ikifika mwisho wa mwezi,atakamuliwa njee zikiisha ndo anarudi ndani anakuita baby, ovyooooooo,wanaume mungu anawaona,yaani mwanaume akishapata hela anawaza kuchepuka tu!!!!
Nimemuelewa kama alivyomaanisha, bahati mbaya haiwezekani.Hehe eti mkuu umemuelewa huyo?
Atakuwa na utaratibu wa kutumia viganja hahahaNimemuelewa kama alivyomaanisha, bahati mbaya haiwezekani.
Hahahahahahah hatari lakini salamaMatatizo yetu haya ya kiuchumi bakuli la nyama mnashare watu sita ugali mlima, baada ya watoto wawili una kukuta tumbo kule, unatupia madera, mkitoka mume anakwambia tangulia ninakuja. Kama ni restaurant atahakikisha umekula umemaliza wewe na wanao akija analipa bill mnarudi nyumbani.
Huwezi kulalamika hunitoi
Ndoa tamu na hasa umpate mwanaume Mwenye kujua nini maana ya ndoa.
Hongera...kama mimi
Hongera
Safi sana, kwa maana nyingine tusiwe wepesi kusema matatizo yetu kwa watu kila mtu anayo ya kwakekatika vitabu vyenye kufunza historia ya hekima kuna kisa kirefu cha mtu aliekwenda kwa kiongozi mkuu wa kiroho wa wakati huo kutaka mashauri, alipokaribia mlango wa nyumba ya kiongozi yule alisikia sauti ya mke wa kiongozi analalamika sana, analalamika kwa maneno makali mno, jamaa akashangaa na kuamua kurudi anakotoka, kabla hajafika mbali kiongozi akamuona na kumuuliza kulikoni mbona anarudi anakotoka bila ya kueleza chochote, jamaa akamjibu nimekuja unishauri kuhusu mke wangu yeye analalamika na maneno mengi kila wakati lakini nimefika hapa naona ni afadhali wa kwangu kuliko wa kwako, kiongozi akamjibu rudi kakae na mke wako, nikikuuliza fadhila wanazotufanyia hawa unaweza kuzihesanbu? ndivyo walivyo. Tuwavumilie na tukae nao kwa wema.
Tatizo lipo kwenye malezi tunayoyapata cku hizi. Unakuta mwanamke hamuheshim hata mama yake mzazi, atakuheshim wew mliyekutana chuoni na kuoana?Habari wanakijiji wenzangu, matumaini mko salama kabisa, bila kupoteza muda nielekee kwenye mada
Kumekuwa na wimbi la watu wengi hasa wanandoa kueleza negatives za ndoa kiasi kupelekea wengine kukata tamaa ama kuogopa lakini ngoja niwaelezeni kitu
Ndoa ni tamu sana hasa kama umepata mtu sahihi, kwanza mfanye mke au mume kuwa rafiki yao ambaye unaweza kushare mambo yote yawe ya Furaha au huzuni hii itamfanya mwenzako kuwa huru kushauri lolote kwa kauli nzuri, ikumbukwe hakuna binadamu mkamilifu hivyo mapungufu ya mwenzio chukulia kama kilema sio ndio fimbo ya kumchapia, unaweza kupata mwanamke mrembo lakn kitandani hajui chukulia hiyo ni changamoto na usimuumize kwa sababu ya udhaifu huo utafurahia ndoa yako.
Mwanamke akijua majukumu yake na akaweza kuyatimiza licha ya kuajiriwa, kuheshimiana licha ya kuwa na utofauti wa kipato, kuwe na mipaka mambo ya kazini yaishie kazini uwapo nyumbani lazima familia iwe imara na ndoa itafurahiwa na kila mmoja.
Makwazo hayakosekani, mkikaa pamoja na kuelezana kwa upendo mkiepuka maneno makali ya kuumiza lakini pia kuachilia kwa kusamehe yaliyopita, mtafurahia
Michepuko kwa wanaume husababishwa na mwanamke kutokaa kaa katika nafasi au tamaa tu, kama mwanamke atakaa katika nafasi yake, kupunguza gubu kuna nafasi kubwa kwa mwanaume kutulia au kupata mchepuko mstaarabu ambaye hatavuruga ndoa.
Mungu ni kiongozi mkuu wa ndoa ukiambatana naye katika kila hatua lazima ufurahie ndoa yako wengine watalalamika kuhusu ndoa zao wewe utakuwa unashangaa mambo ya naenda
Mwisho vijana msiogope ndoa, ni tamu sana kama utapata mtu sahihi kama nilivyoeleza hapo juu, usikubali kukatishwa tamaa kwa sababu et ndoa ya fulani inasumbua ukajua na yako itakuwa hivyo nooo, kila mtu amezaliwa kivyake ingekuwa hivyo tungeogopa kusoma eti kisa Fulani amefeli mtihani, Muwe na siku njema.