Ndoa ni tamu sana

Ndoa ni tamu sana

Mtoa hoja Mungu wetu si wa michanganyo. Kama mtu amekuwa mwaminifu kwa Mungu hilo suala la mchepuko mstarabu halipo, huo ni uzinzi tu kama ilivyo kahaba/mzinzi yeyote hakuna cha ustarabu, atendaye dhambi ni wa ibilisi
Nashukuru kwa kupigilia msumari
 
Mwanaume ni mbaya sana katika ndoa hasa kila ikifika mwisho wa mwezi,atakamuliwa njee zikiisha ndo anarudi ndani anakuita baby, ovyooooooo,wanaume mungu anawaona,yaani mwanaume akishapata hela anawaza kuchepuka tu!!!!
Si kweli pengine huyo uliyenaye ndio yuko hivyo haimaanishi wote wako hivyo wapo wanaofurahia huo mwisho wa mwezi na familia zao, kaa na mwenzio chini tumia kila namna mpaka amekuweka ndani ujue una nafasi yako kwake itumie hiyo
 
Matatizo yetu haya ya kiuchumi bakuli la nyama mnashare watu sita ugali mlima, baada ya watoto wawili una kukuta tumbo kule, unatupia madera, mkitoka mume anakwambia tangulia ninakuja. Kama ni restaurant atahakikisha umekula umemaliza wewe na wanao akija analipa bill mnarudi nyumbani.

Huwezi kulalamika hunitoi
Hahahahahahah hatari lakini salama
 
katika vitabu vyenye kufunza historia ya hekima kuna kisa kirefu cha mtu aliekwenda kwa kiongozi mkuu wa kiroho wa wakati huo kutaka mashauri, alipokaribia mlango wa nyumba ya kiongozi yule alisikia sauti ya mke wa kiongozi analalamika sana, analalamika kwa maneno makali mno, jamaa akashangaa na kuamua kurudi anakotoka, kabla hajafika mbali kiongozi akamuona na kumuuliza kulikoni mbona anarudi anakotoka bila ya kueleza chochote, jamaa akamjibu nimekuja unishauri kuhusu mke wangu yeye analalamika na maneno mengi kila wakati lakini nimefika hapa naona ni afadhali wa kwangu kuliko wa kwako, kiongozi akamjibu rudi kakae na mke wako, nikikuuliza fadhila wanazotufanyia hawa unaweza kuzihesanbu? ndivyo walivyo. Tuwavumilie na tukae nao kwa wema.
 
katika vitabu vyenye kufunza historia ya hekima kuna kisa kirefu cha mtu aliekwenda kwa kiongozi mkuu wa kiroho wa wakati huo kutaka mashauri, alipokaribia mlango wa nyumba ya kiongozi yule alisikia sauti ya mke wa kiongozi analalamika sana, analalamika kwa maneno makali mno, jamaa akashangaa na kuamua kurudi anakotoka, kabla hajafika mbali kiongozi akamuona na kumuuliza kulikoni mbona anarudi anakotoka bila ya kueleza chochote, jamaa akamjibu nimekuja unishauri kuhusu mke wangu yeye analalamika na maneno mengi kila wakati lakini nimefika hapa naona ni afadhali wa kwangu kuliko wa kwako, kiongozi akamjibu rudi kakae na mke wako, nikikuuliza fadhila wanazotufanyia hawa unaweza kuzihesanbu? ndivyo walivyo. Tuwavumilie na tukae nao kwa wema.
Safi sana, kwa maana nyingine tusiwe wepesi kusema matatizo yetu kwa watu kila mtu anayo ya kwake
 
Habari wanakijiji wenzangu, matumaini mko salama kabisa, bila kupoteza muda nielekee kwenye mada

Kumekuwa na wimbi la watu wengi hasa wanandoa kueleza negatives za ndoa kiasi kupelekea wengine kukata tamaa ama kuogopa lakini ngoja niwaelezeni kitu

Ndoa ni tamu sana hasa kama umepata mtu sahihi, kwanza mfanye mke au mume kuwa rafiki yao ambaye unaweza kushare mambo yote yawe ya Furaha au huzuni hii itamfanya mwenzako kuwa huru kushauri lolote kwa kauli nzuri, ikumbukwe hakuna binadamu mkamilifu hivyo mapungufu ya mwenzio chukulia kama kilema sio ndio fimbo ya kumchapia, unaweza kupata mwanamke mrembo lakn kitandani hajui chukulia hiyo ni changamoto na usimuumize kwa sababu ya udhaifu huo utafurahia ndoa yako.

Mwanamke akijua majukumu yake na akaweza kuyatimiza licha ya kuajiriwa, kuheshimiana licha ya kuwa na utofauti wa kipato, kuwe na mipaka mambo ya kazini yaishie kazini uwapo nyumbani lazima familia iwe imara na ndoa itafurahiwa na kila mmoja.

Makwazo hayakosekani, mkikaa pamoja na kuelezana kwa upendo mkiepuka maneno makali ya kuumiza lakini pia kuachilia kwa kusamehe yaliyopita, mtafurahia

Michepuko kwa wanaume husababishwa na mwanamke kutokaa kaa katika nafasi au tamaa tu, kama mwanamke atakaa katika nafasi yake, kupunguza gubu kuna nafasi kubwa kwa mwanaume kutulia au kupata mchepuko mstaarabu ambaye hatavuruga ndoa.

Mungu ni kiongozi mkuu wa ndoa ukiambatana naye katika kila hatua lazima ufurahie ndoa yako wengine watalalamika kuhusu ndoa zao wewe utakuwa unashangaa mambo ya naenda

Mwisho vijana msiogope ndoa, ni tamu sana kama utapata mtu sahihi kama nilivyoeleza hapo juu, usikubali kukatishwa tamaa kwa sababu et ndoa ya fulani inasumbua ukajua na yako itakuwa hivyo nooo, kila mtu amezaliwa kivyake ingekuwa hivyo tungeogopa kusoma eti kisa Fulani amefeli mtihani, Muwe na siku njema.
Tatizo lipo kwenye malezi tunayoyapata cku hizi. Unakuta mwanamke hamuheshim hata mama yake mzazi, atakuheshim wew mliyekutana chuoni na kuoana?

Bongo saiv kama ulaya. Ndoa magumashi!!
 
Back
Top Bottom