Ndoa na kazi ipi bora?

Ndoa na kazi ipi bora?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
37,112
Reaction score
55,529
Kumekuwa na malalamiko ya wanandoa wengi walioajiriwa kuwa mbali na wapenzi wao, ambapo mke/mume anakuwa mbali na mwenzie kutokana na mazingira ya kazi.

Mmoja anaweza kuwa mbali ki wilaya, mkoa au nchi tofauti na mwenzie na kupelekea ugumu wa kuonana mara mara na mwenzake.

Hii imekuwa ikiathiri taasisi ya ndoa na kupelekea upendo kupungua na kuongeza dhambi ya uchepukaji ndani ya ndoa.

Waume wamekuwa wakimaliza hamu zao na kuzaa nje huku pia wake zao nao wakimaliza hamu zao pamoja nakuzaa watoto nje.

Mwisho wa siku ndoa inakuwa na doa.

Sasa tuchague, ndoa ama kazi ipi ni bora?

dna.jpg
 
Kama hakuna umuhimu,Mke awe Mama wa Nyumbani tu,
Aangalie Nyumba,Mumewe na watoto wake,

Kama kuna umuhimu wa Mke kufanya kazi,basi iwe ni kazi ya kwenda asubuhi na kurudi home mchana au jioni.

Muhimu;Mume ajitahidi kutimiza majukumu ya nyumbani na kumtimizia mkewe ili mke asione umuhimu au ulazima wa kufanya kazi.
 
Kama hakuna umuhimu,Mke awe Mama wa Nyumbani tu,
Aangalie Nyumba,Mumewe na watoto wake,

Kama kuna umuhimu wa Mke kufanya kazi,basi iwe ni kazi ya kwenda asubuhi na kurudi home mchana au jioni.

Muhimu;Mume ajitahidi kutimiza majukumu ya nyumbani na kumtimizia mkewe ili mke asione umuhimu au ulazima wa kufanya kazi.
Mfano, umemkuta tayari mkeo ana kazi mkoa mwingine kabla ya kuoana, je utamuachisha kazi?​
 
Inategemea na uchumi wako. Na pia wategemezi alionao mkeo.

Maana wanawake wengine wamebeshwa majukumu ya kutunza wazazi wao na wadogo zake
Kwa mazingira hayo, utakuwa uko tayari kubeba 'risk' yoyote itakayo sababishwa na umbali?​
 
Kwa mimi siwezi kubeba risk ndio maana naishi nyumba moja na mke wangu.

Sina ujinga wa kufunga ndoa za bluetooth, ndoa hewa
Ikitokea akapata uteuzi wa kwenda huko mbali, utamzuia?
 
Kama hakuna umuhimu,Mke awe Mama wa Nyumbani tu,
Aangalie Nyumba,Mumewe na watoto wake,

Kama kuna umuhimu wa Mke kufanya kazi,basi iwe ni kazi ya kwenda asubuhi na kurudi home mchana au jioni.

Muhimu;Mume ajitahidi kutimiza majukumu ya nyumbani na kumtimizia mkewe ili mke asione umuhimu au ulazima wa kufanya kazi.
Hivi mke akiwa mama wa nyumbani tu mara paaap, baba ambaye ndio provider akafariki huyo mama anaanzia wapi kutunza familia?? Au ndio ile unaona mume kafariki leo mke wiki ijayo anaanza kudanga,.
 
Ushauri upo hivi ni vizuri mke akiwa mbali kwa maana unaepushwa na madharau napia kwasababu akiwa nakazi kuombwa pesa ni kidogo sana kwanini umuachishe kazi awe anakusumbua
Na je kama unachepuka, hapo itakuwaje?
 
Hivi mke akiwa mama wa nyumbani tu mara paaap, baba ambaye ndio provider akafariki huyo mama anaanzia wapi kutunza familia?? Au ndio ile unaona mume kafariki leo mke wiki ijayo anaanza kudanga,.
Kudanga ni tabia ya mtu,wala haihusiani na shida ya maisha,kudanga ni sawa na tabia ya wizi,mtu mwizi hata akiwa na hela ila ataiba tu,

Kufa ni jambo la siri,ukiwaza kifo tu basi huwezi kufanya jambo lolote lile hapa Duniani,

What if Mke atangulie kufa? What if wafe kwa pamoja kwa ajali?

Kwanini Wanawake wengi huamini kua Mume ndio atatangulia kufa?

Anyway kila mtu ana utashi wake katika familia yake,maoni yangu sio formula.
 
Unafiki ni mwingi sana ,kama utaoa mtumishi mambo ya ndoa sahau ...Maisha ya kazi yanajulikana ,kazi zina majukumu kila siku .

Ukweli ni kwamba ,mke na mume wakiwa wanafanya kazi basi wanakuwa na malengo tofauti ,tena malengo binafsi ,kila mtu anataka kupanda cheo na kufanya vizuri kazini kwake .

By the way ,fanye kile unachoona kinafaa ,ukweli utabaki pale pale ; mke anayefanya kazi sio mke ,tena akiwa mkoa wa mbali ,inakuwaje mke anaishi mkoa tofauti na wewe?

Hayo mengine ,sijui kusaidiana ,mme akifa Watoto watapata tabu ni mambo ya kufikirisha ,hayana uhusiano kabisa na mke kutofanya kazi.
 
Unafiki ni mwingi sana ,kama utaoa mtumishi mambo ya ndoa sahau ...Maisha ya kazi yanajulikana ,kazi zina majukumu kila siku .

Ukweli ni kwamba ,mke na mume wakiwa wanafanya kazi basi wanakuwa na malengo tofauti ,tena malengo binafsi ,kila mtu anataka kupanda cheo na kufanya vizuri kazini kwake .

By the way ,fanye kile unachoona kinafaa ,ukweli utabaki pale pale ; mke anayefanya kazi sio mke ,tena akiwa mkoa wa mbali ,inakuwaje mke anaishi mkoa tofauti na wewe?

Hayo mengine ,sijui kusaidiana ,mme akifa Watoto watapata tabu ni mambo ya kufikirisha ,hayana uhusiano kabisa na mke kutofanya kazi.
Kwa hiyo, mke aliyesomeshwa na wazazi wake unataka awe mama wa nyumbani?
 
Kwa hiyo, mke aliyesomeshwa na wazazi wake unataka awe mama wa nyumbani?
Ninachokuambia kusoma hakuna uhusiano na kufanya kazi ,haya mambo zamani waliwezaji basi katika ulimwengu wa sasa ,wote wanafanya kazi ni ubatili kufunga ndoa.

Ukweli utabaki pale pale , zamani mke na mume walikuwa wanaandaliwa mapema sio kukurupuka ...Kwa huu umagharib basi na ndoa hakuna.
 
Back
Top Bottom