Lakini mkuu hapa tunaongelea ubaguzi wa rangi, wewe unasema Afrika tunaogoza kwa ubaguzi. Unamaanisha m-Kenya na m-Tanzania wanabaguana? Kisa rangi zao?
Au Mchaga na Msukuma?
Balotelli alirushiwa ndizi akiwa uwanjani Italia, Etoo alioneshwa ishara ya nyani akiwa Uingereza.
India kuna binti wa Kitanzania alivuliwa nguo na wahindi hadharani shambulio ambalo limetokana na ubaguzi wa rangi. Watanzania wanaoishi au kufanya kazi kwa wahindi watakua washasikia neno "Goro" ambalo hutumika kumuita Mtanzania, unajua maana yake?
Kuna mwafrika/ mtu yeyote aliyewahi kumrushia kitu mchezaji asiye na asili ya Afrika akiwa analenga ubaguzi wa rangi?
Mkuu nahisi haupo informed ipasavyo.