Ndege zinamsaidia nini bibi yangu kule kijijini?

Ndege zinamsaidia nini bibi yangu kule kijijini?

Nimekuwa najiskia vibaya sana pale naposafiri kwenda nchi ndogo kama Seashels/Mauritious/Rwanda/Cape verde/Guinea iquotoria/ ni viinchi vidogo vidogo sana ila wana ndege za nchi zao Air sichels/Mauritious airways/Rwanda air/Swatzi airways/ ni inchi ndogo hata mkoa wa Arusha mkubwa!
Alafu najiambia ivi mbona sie hatuna hata kandege kamoja kalichoandikwa air Tanzania?
Zaidi nlijiskia vibaya pale ndege ya Kenya airways ilipoenda mpaka Rio d janairo kupeleka wana michezo tokea Kenya! Dah ukiangalia Ethiopian airlines ndo ndege kongwe zaidi barani Africa na ndo Ethiopia wanaitegemea kwa uchumi wa nchi yao!
Alafu ukiangalia kwa Rasilimali Africa nzima tanazo ni ndio vyanzo va mapato makubwa! Ambapo ndo tungetakiwa tuwe the South Africa ya East Africa

ukweli nashindwa elewa wanaobeza mafanikio makubwa na yaa ajabu anayo yafanya kwa mda mfupi amekuwa madarakani, mueshimiwa Rais! anachofanya tena kwa manufaa ya Watanzania mijitu inaponda? Kweli alie tuloga watanzania sijui alitulogea kwa mganga gani? Bora tumtafte uyo mganga awague baadhi ya Watanzani!
VIVA MY PRESIDENT VIVA!
 
Muamishie mjin.....na ww fnya kaz upate hela itakusaidia na co unaandka hpa.....kwn umelazmishwa kupnda??
 
anza kumsaidia bibi yako wewe kabla mapato ya ndege hayajamsaidia

utakuta bibi yako ana watoto 7 ila wameshindwa msaidia wote lawana inapewa ndege ya jpm
 
Uliza pia hostel zinazojengwa chuo kikuu cha Dar es salaam zinamsaidiaje bibi yako. go Magufuli maneno ya watu yasikurudishe nyuma na jitihada zako za kweli kweli...
ww utakuwa ulikula 10% ununuzi wa cash kwani bei halisi ya ndege ni ndogo kuliko hiyo cash mliyotoa
 
Hakuna lami na hajawahi na wala hategemei kupanda ndege,

Je zitamsaidia nini yeye hizi??hata mimi binafsi sielewi zinanisaidia nini maana sina pesa ya kulipia kwenye ndege.

Wataalamu msaada wenu.
Waliokula 10% mgao ganji la ununuzi wa hizo ndege watakushambulia sana .
 
Tatizo si ndege bali ni bei kubwa ya ndege wakati bei halisi si hiyo pia ununuzi wa cash mara nyingi huwa na magumashi ikiwemo kununua ndege Mtumba ambao umekarabatiwa vizuri kiasa kwamba unaonekana ni mpya, 10% hutawala manunuzi ya cash, waliopewa Dhanana za manunuzi TZ huwa miaka yote wanapiga lakini siri hujulikana baadae wakiwa wameshastaafu, hata hizo ndege lazima zitaibua skendo baadae.
 
Hospitalini hakuna dawa....ila sie tunataka Jet nyingine....nchi ya ajabu sana hii....
 
Hakuna lami na hajawahi na wala hategemei kupanda ndege,

Je zitamsaidia nini yeye hizi??hata mimi binafsi sielewi zinanisaidia nini maana sina pesa ya kulipia kwenye ndege.

Wataalamu msaada wenu.
Kwa akili kama hizi sishangai mnachagua jiwe.
 
You are very myopic! haijawahi kutokea kitu fulani kikawa na faida kwa kila mtu, wala haitokaa iwe hivyo.
 
Yeye alichokuwa anasema vipaumbele vingefuatwa kwanza huduma za jamii kwanza baadaye hiyo midege yenu!!!
Conclusion hapo ni kama umemsemea, umuhimu wa ndege utaufahamu kama unakaa mikoa ya pembezoni kama Mwanza, Kigoma, Bukoba na Musoma sema sasa hivi barabara ndio zinatutoa ufahamu

Nikirudi kwenye mada, hizo huduma za jamii zinatakiwa zitegemeane yaani ndege inaweza ikaonekana haina impact ya moja kwa moja kwa bibi yake wa kijijini lakini kupitia ndege hiyo hiyo zile ela ambazo zingelipwa kwenye mashirika ya ndege ya nje zinabaki kwenye mzunguuko wa ndani kwa kusafiri kwenye usafiri wa Tanzania na ela inabaki Tanzania tofauti kama unasafiri na kampuni nyingine kwenda.

Pia ni rahisi pia ku-promote utalii wa ndani kwa kuwa ukiwa na ndege zako kama Taifa hata logistics za routes kwenye sehemu za utalii na mbuga zetu utaweka ili unapofanya promotion tayari una suruhisho la usafiri. (kila mtu au taasisi ina umuhimu kwa ukuaji wa kiuchumi kama sekta zote zitakuwa linked vizuri)

Kwahiyo kitu kinaweza kikawa hakina faida kwa bibi yako lakini kikawa na faida kwa bibi ya mwingine na kinyume chake pia. Na nchi ingekuwa inaendeshwa kwa mawazo kama yako mikoa kama Dodoma, Singida na mingine isingepewa miundombinu badala yake ela ingewekezwa Dar, Mwanza na Arusha ambapo watu wake wana mchango mkubwa kwa maendeleo ya Taifa (mfano tu hapa ila kuna mikoa mingine pia kutokana na rasilimali zinazopatikana kule)

Mdau major mwendwa ameeleza kiurefu
 
Hakuna lami na hajawahi na wala hategemei kupanda ndege,

Je zitamsaidia nini yeye hizi??hata mimi binafsi sielewi zinanisaidia nini maana sina pesa ya kulipia kwenye ndege.

Wataalamu msaada wenu.
Hutaelewa umuhimu wa ndege hadi kifo chako ukizingatia una ugonjwa kichwani.
 
Hakuna lami na hajawahi na wala hategemei kupanda ndege,

Je zitamsaidia nini yeye hizi??hata mimi binafsi sielewi zinanisaidia nini maana sina pesa ya kulipia kwenye ndege.

Wataalamu msaada wenu.
Pesa si kisingizio... Sema hujui wenzako wanachojua. Kupanda ndege hakuna tofauti na kupanda basi sema unatakiwa ufanye booking mapema sana.
Ndugu yangu alikua anataka kusafiri tokea Dar kwenda Mbeya kwa fastjet... Akakata ticket mwezi mmoja kabla na ikawa elfu 90 kwenda na kurudi. Mda wa kusafiri ukafika mdogo ake akataka ambatane nae ila yeye akaenda kwa basi na nauli ilikua elfu 45 kwa kwenda tu.
Ko ukijipanga vizuri unaweza panda ndege kwa bei rahisi tu.
 
Hakuna lami na hajawahi na wala hategemei kupanda ndege,

Je zitamsaidia nini yeye hizi??hata mimi binafsi sielewi zinanisaidia nini maana sina pesa ya kulipia kwenye ndege.

Wataalamu msaada wenu.
Wewe na bibi yako mmewasaidia nini watanzania?
 
Hakuna lami na hajawahi na wala hategemei kupanda ndege,

Je zitamsaidia nini yeye hizi??hata mimi binafsi sielewi zinanisaidia nini maana sina pesa ya kulipia kwenye ndege.

Wataalamu msaada wenu.
Nina mashaka na elimu yako na akili ya uchambuzi wa mambo !!!...
Kweli ndo maana lowasa alisema
1.Elimu 2.Elimu 3.Elimu
S mnaona wenyewe watanzania tulionao
Kesho hukawii kuja kusema..."umeme tanesko unamsaidia nn bab yangu na ww mwenyewe maana hamna uwezo wa kulipa bili
 
Yeye alichokuwa anasema vipaumbele vingefuatwa kwanza huduma za jamii kwanza baadaye hiyo midege yenu!!!
Vipaumbele vinategemeana. Hakuna kipaumbele ambacho Ni complete and perfect by itself. Ndege watapanda wenye uwezo, Serikali itapata faida ambayo itatumika kupanua huduma za jamii hadi huko kijijini Kwa mtoa mada
 
ama kweli kuna watu na viatu, mtoa mada ni kiatu tena cheusi, kwani bibi yako ni nani hasa mpaka kila lifanyikalo nchini afaidike?
Huyu mleta mada hajafikiria yeye anamsaidiaje bibi yake wa kijijini anakimbilia ndege ambazo zimenunuliwa na serikali na hajafikiria fastjet wanamsaidiaje bibi yake. Kuna mambo mengi ambayo serikali inafanya mfano uhakiki wa vyeti feki ina maana bibi yake ana cheti halali?
 
Kwenye uchumi kuna kitu kinaitwa multiplier effect, kwanini iwe ndege na sio bandari, hoteli za kitalii, treni, kampuni ya TTCL nk. kwa mfano serikali imechukua asilimia 35 zilizokuwa zinamilikiwa na Bhatti ambao ni wamiliki wa Airtel waliokuwa wakiwa sehemu ya umiliki wa TTCL je ununuzi wa hizo hisa uliogharimu zaidi ya billioni 15 unakusaidiaje,
Kwa kesi ya ATCL pamoja na ukweli kuwa si watanzaniawengi wenye uwezo wa kupanda ndege hii haiondoi ukweli kuna faida kama wananchi tutaipata kwa mfano faida ya moja kwa moja miezi 2 kabla ya hizi ndege kuja shirika la ATCL lilitangaza nafasi za ajira takribani 18. japo sio wewe au bibi yako tayari kuna watanzania takribani 18 ambao watanufaika moja kwa moja, hawa watu watapata vipato ambavyo vitaendesha maisha yao yao ya kila siku na jamaa zao, fedha zao zotakuwa chanzo kwa wengine kupata riziki hiyo moja.

Kwa kuwa shirika ni la serikali, tunatarajia kupata kodi ambayo hulipwa na kila abiria anayesafiri, na kila ndege inapotua katika uwanja wa ndege kuna ada inalipia, kupitia hiyo serikali itapata fedha ambazo zitatumika kuagiza dawana bidhaa muhimu kama mafuta ambayo yanaleta bidhaa kwako na bibi yako. hiyo mbili

ya tatu kupitia sekta ya anga kuimarika kutapelekea sekta nyengine kama ya utalii kukuwa na hivyo kuongeza mapato ya kuja kujenga hiyo barabara, badala ya watalii kushukia nchini kenya na kupanda usafiri mwengine sasa watakuwa wanakuja moja kwa moja jambo litakalowapunguzia usumbufu na kuwavutia kuja kwa wingi, lakini pia sekta ya biashara za kimataifa itaimarika kwa kuwa na usafiri wa uhakika ambao wafanyabiashara wengi huzingatia katika kuhakikisha wanafanya biashara kwa wakati ili kuokoa gharama zinazoweza kuongezeka kwa kuwa na mfumo mbovu wa usafiri wa anga. hili litatupelekea kuongeza akiba ya kutosha ya fedha za kigeni ambazo zitasaidia katika manunuzi ya bidhaa na huduma nje ya nchi na kuimarisha shilingi yetu
Unafikiri hawajui haya unayoeleza? Wanajitoa ufahamu tu kwasababu ya siasa uchwara!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom