Ndege hutumia mafuta gani?

Ndege hutumia mafuta gani?

Nyamongo kwao

Member
Joined
Jan 1, 2013
Posts
48
Reaction score
4
Naombeni kujuzwa ndege hutumia mafuta gani? Hi ni kutokana na kuishi kwangu mbali na mazingira hayo.
 
Ndege yupi? Mbauyau au njiwa? Lakini kama ni hizi za abiria hutumia Jet A1
 
Umenikumbusha wakati tupo kijijini zamani tulikua tunadanganyana ndege inatumia mafuta ya korosho.
 
Ndege yupi? Mbauyau au njiwa? Lakini kama ni hizi za abiria hutumia Jet A1

Huko kwenu manyara mbayuwayu na njiwa hutumia mafuta? Nilimaanisha hizi ndege za akina fastjet &Tanzania Airways.
 
yapo ya aina 2...(1) Avgass 100LL na Jet-A1.....Avgass( Aviation gassoline) hii ni aina ya mafuta yenye tabia kama ya petroli bt ni very pure na yana rangi ya bluu ambapo ndege nyingi zinazotumia hayo ni Cessna ndogo na baadhi ya helcopta...ila Jet ndio the main leading Aircraft fuel kwa mdge zote kubwa unazozijua na kuziskia hapa duniani zikiwemo na Caravan..kwa kifupi Jet-A1 ni mafuta ya taa tu...
 
Zamani tulikuwa tunaambiwa ni mafuta ya taa
 
Nakumbuka pale Nzovwe Mbeya gari kubwa aina ya semitrailer tanker lenye namba za Zambia lilianguka likalalia ubavu lilikuwa limesheheni mafuta ya A1 jet fuel raia wakapasua moja ya mifuniko waliweza kukinga mafuta mengi sana wakitumia ndoo na masufuria.nilistaajabu kujua kwamba kumbe mafuta ya ndege yanafaa kuwashia taa na majiko yenye tambi.
.
 
NA YA MELI Je?

yapo ya aina 2...(1) Avgass 100LL na Jet-A1.....Avgass( Aviation gassoline) hii ni aina ya mafuta yenye tabia kama ya petroli bt ni very pure na yana rangi ya bluu ambapo ndege nyingi zinazotumia hayo ni Cessna ndogo na baadhi ya helcopta...ila Jet ndio the main leading Aircraft fuel kwa mdge zote kubwa unazozijua na kuziskia hapa duniani zikiwemo na Caravan..kwa kifupi Jet-A1 ni mafuta ya taa tu...
 
Mafuta ya ubuyu.. kama umeweza kupost hii kitu basi hata kugoogle unaweza
 
Back
Top Bottom