Ndaisaba: Itungwe sheria ya kuzuia watu kunywa pombe muda wa kazi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,501
9,279
Mbunge wa Ngara (CCM), Ndaisaba Ruhoro amelitaka Bunge kutunga sheria itakayopiga marufuku matumizi ya vileo hadharani.

Ruhoro alitoa kauli hiyo wakati akichangia Mpango wa Serikali jana bungeni mjini Dodoma akibainisha kuwa kunywa pombe hadharani kunasimamisha shughuli za maendeleo kwa kuwa linashusha ufanisi wa kazi, kutaka watu wasinywe wakati wa kazi.

"Iletwe sheria hapa bungeni itakayopiga marufuku vileo kuuzwa muda wa kazi ili tuipitishe maana haisaidii watu wanashindwa kutimiza majukumu yao wakikimbilia kulewa," amehoji Ruhoro.

Ametaja kundi la vijana kuathirika na kudai wafanyakazi wengi wanatumia saa ya kazi kunywa pombe kwa kuwa muda wa kazi baa huwa zimefunguliwa.
 
Mimi kwa akili zangu ndogo ningeshauri watu wanywe pombe wekend tu, kuanzia Ijumaa jioni mpaka jumapili tu, weekdays ni kazi kwenda mbele, tumechelewa sana kwenye hii nchi.
 
Watu wanasubiri hoja nzito mtu anakuja na hoja nyepesi kuliko karatasi.Unawezaje kuzuia kitu halali kwa mujibu wa sheria kisitumike hadharani sasa.

Angalau angesema kuwepo kwa msisitizo wa elimu bora ya matumizi ya hivyo vileo. Sio kila mtu anayekunywa pombe hafanya kazi na si kila mtu ambaye hanywi pombe anapenda kufanya kazi.
 
Pombe ipigwe marufuku mtaendeshaje nchi?
Tanzania bila wafuta sigara na walevi imekwisha
Huyu Mbunge ana mambo ya kitoto sana. Kwanza wananchi wake hawajamtuma akaongelee mambo ya watu wanaokunywa pombe. Mambo ya barabara, maji, madarasa, na umeme jimboni kwake hajayaongelea anarukia mambo ya sisi wanywa pombe. Ana matatizo huyu siyo bure
 
Kunywa pombe nayo ni kazi. Aache uboya huyu mbunge. Au anadhani tunakunywa bure? Kwanza wanaokunywa pombe ndiyo wanaofanya sana kazi ndiyo maana wana hadi hela za kunywa hizo pombe
Hajui stress za kazi na zile za ujira mdogo, zinapunguzwa , kama sii kuondoshwa na hayo maji pendwa .
 
Pombe ipigwe marufuku mtaendeshaje nchi?
Tanzania bila wafuta sigara na walevi imekwisha
Hajui angalao viwanda vinavyotengeneza hiyo mambo yaweza kuwa angalao ndio vinavyoweza onafaidi wakati huu japo kidogo.
 
Kwa hiyo mlikuwa mnaapply hiyo sheria kabla ya kuitunga?maana huku street watu wanakamatwa kila siku kwenye mabaa sababu ya the so called mda wa kazi na bar zinauza pombe jioni.

Hivi hizi kazi mnazotaka watu wafanye ni zipi ilhali siku hizi kila mtu anapambana ili mikonon uende kinywani sababu maisha magum.
Kweli kuna watu wa kuwahamasisha kazi siku hizi au mmekosa la kuongea?

Hao vijana gani mnaowasema wakati vijana wa kibongo siku hizi wako bize wanajua kuitafta hela zaidi yenu nyinyi mnaolipwa posho tu hapo bungeni?hivi kuna kundi linapiga mzigo siku hizi kama vijana?uyu mbunge anaongelea nchi gani?hivi hawa viongozi kama bungeni wanareflect watanzania wenyewe au wao wana ulimwengu wao unaowafanya hawajui mambo huku chini?

kweli dunia ya leo vijana wanavyopambana mtu unasimama unasema vijana hawafanyi kazi?mnatutafuta nini?mss!Na hilo jina la huyo mbunge huyo......jumlisha ni Ngara.napata ukakasi.
 
Back
Top Bottom