Nchi ya Ajabu: Nimewaona Wafanyabiashara wa Tanzania wamekuja Kampala kununua Bidhaa za China

Naunga mkono hoja, hata mimi, bi mdogo ni mfanyabiashara wa nguo, alianzia kwenda South, nguo za kule ghali, akaenda Uturuki, nguo ni quality lakini overheads kubwa. Akaja kwenda China, ili ilipe lazima ulete mzigo mkubwa, sasa anakwenda Uganda, aki fly Jumatano, Jumamosi yuko hapa, mzigo wote ni wa Mchina, uliopitia bandari yetu!. Anasema Kariakoo is full of the cheapest Chinese stuff, Uganda has a better quality.
P
TRA lazima wajipange sana Mkuu. Hawa watu bado wanatumia ule mfumo wa tangu tumepata Uhuru. Hawataki kabisa kubadilika kwenda na mfumo wa uchumi wa ushindani wa Dunia ya sasa. Wenzetu Kenya na Uganda wamebadilika sana. Pamoja na sheria za kodi za East Africa lakini nakuhakikishia hii sheria ni kiini macho tu. Kenya na Uganda hawafuati kabisa hizi sheria. Wao wanafata matakwa ya wafanyabiashara wao.

Ndiyo maana unaona k,koo imekufa. Wateja wote wa Zambia Malawi Zaire wamehamia Nairobi. Kampala Nenda utawakuta wamejaa Mahotellini usiku. Mchana wanafungasha tu mizigo. Shida waliyonayo hawa TRA wa Tanzania ni kubwa kuliko Raisi anavyofikiria.
 
Juzi nilikuwa TRA. Katika watu 10 tuliokuwa kwenye line, 7 walikuwa wapo pale “kufunga au kusimamisha biashara zao kwa muda”. Wengi sasa hivi wapo radhi wastopishe biashara zao rasmi na waanze kufanya upya kimyakimya bila kutoa taarifa TRA na Manispaa.

Kuna haja TRA kuangalia wapi tunakosea na kurekebisha baadhi ya sheria mbovu za kodi zisizo na tija
Tatizo la hawa TRA ni kubwa sana Mkuu, kwanza Dharau. Mtu akishafanya kazi TRA anajiona Kama Mungu. Wao wanajiona ndiyo Wasomi Pekee ktk Nchi Hii, Stupid. Watakuja kumletea Raisi magonjwa yasiyoambukiza kwa Upuuzi na kujiona kwao. Huwa hawashauriki. Ni Dharau kwenda Mbele.
 
Juzi Alhamisi nimeshuhudia mwenyewe. Mwanzoni nilikuwa siamini nikijua ni siasa tu, nikiwa katikati ya Jiji la Kampala wakati wa lunch time ktk mgahawa mmoja nilikutana na Wafanyabiashara watatu Watanzania. Nilikuwa nimekaa meza ya jirani na wao, niliposikia Kiswahili chao fasaha nikagundua hawa ni ndugu zangu wa Home, nikasogea tukakaa pamoja, hapo ndipo Mazungumzo yakaanza.

Ktk maongezi kila mmoja wetu alijitambulisha ni nani na amefata nini Kampala, wao walisema kuna bidhaa huwa wanazichukua Kampala na kuzipeleka Tanzania. Aina ya bidhaa sitazitaja. Lakini ni bidhaa hizi hizi za kawaida zinazotoka China na Zimepitia bandari ya Dar kuja Kampala. Nilijaribu kuwadadisi ya kwamba kwanini wasinunue Dar wakati pia zipo, walijibu bei ni kubwa sana na haiwezi kuwalipa.

Tuliongea mengi sana. Lakini nilichogundua ni kwamba, aidha kuna mkakati wa Makusudi wa baadhi ya watendaji wa TRA wa kuhakikisha kwamba hakuna mfanyabiashara wa Tanzania atakayefanikiwa kibiashara. Kwa sababu haiwezekani Bidhaa inayotoka China kupitia bandari yetu halafu iuzwe kwa bei ya chini Kampala kuliko Dar.halafu wafanyabiashara wetu waifate Kampala na kuirudisha Dar na waiuze Dar na kupata faida kuliko Yule Mtanzania aliyenunua bidhaa hiyo hiyo China na akaipitisha bandarini dar na akaiuza Dar.

Madhara yanayosababishwa na Hawa Majini TRA ni makubwa sana tofauti na wenye akili ndogo wanavyofikiria. Nitayataja baadhi.

1 Wafanyabiashara majirani zetu ambao hawana bandari wamekoma kuja Tanzania

1 Wafanyabiasha wetu haswa wa Soko letu kubwa la Kimataifa k,koo wako hoi kiuchumi

3 Wenye Mahotel ambao target Yao ilikuwa ni kuwapokea wageni kutoka Zaire, Malawi, Zambia,
Burundi, Rwanda, lazima watafilisika kwa kukosa wateja.

4 Wenye Restaurant wengi watafunga kwa kukosa wateja. Na hivyo wafanyakazi wengi
Watapoteza ajira.

5 Wabeba mizigo Ajira zao zitakufa rasmi hawa ni kuanzia wale Vibega, matoroli, bajaji, kirikuu, Canter
Fuso malori nk, hii cheni ni kubwa

6 Mama lishe biashara sitadoda.

7 TRA wenyewe hawatoweza kukusanya tena kodi kwa sababu biashara wameua wenyewe.

Maoni yangu,

Pamoja na Raisi kukaa na wafanyabiashara wachache, pia ni lazima TRA wenyewe wakae na Wafanyabiashara haswa wale wanao import bidhaa toka Nchi mbali mbali Duniani. Ili kupanga namna na viwango bora vya kulipa kodi.

TRA ni lazima iwe inawapeleka baadhi ya wafanyakazi wake nje kujifunza ktk Nchi Kama Dubai , Hong Kong, China Uganda South Africa, kuona wao wamewezaje kufanikiwa ktk Suala la kodi kwa kiasi hicho na Kufanya hizo Nchi Wafanyabiashara wakawa na furaha.
Umezunguak sana lakini lengo lako ni kulaumu TRA na huenda wewe ni mkwepa kodi mzoefu uliyekumbwa na kimbunga. Kama unabisha toa info zifuatazo ku-justfy ulichoandika.
1. Walifuata bidhaa gani na huko zinauzwa bei gani. Ukitoa detail tutaweza kweli ku-compare bai ya hapa kwetu na ya Kampala. Na unajua kabisa umeacha kuzitaja hizo bidhaa makusudi kwa sababu unaumbuliwa!
 
Yeye mwenyewe linamkera sana, ndiyo maana kila Siku anawatumbua, bahati mbaya kila anayemuweka ni bomu
Sidhani kama yana mkera, kama anawatumbua kila siku na hakuna mabadiliko angekundua ishu si watu ni mfumo.
 
Hawa mambuzi ndio wanaomkwamisha mheshimiwa
Si kweli kabisa msikimbie kivuri chenu. Nani anapitisha sheria? Nani kila siku anawaambia TRA wakusanye kodi yote? Nani anasema watu lazma walipe kodi?
Jamaa nyie ,msitubambikie kabisa..ukinunua kitu omba risiti na ukiuza kitu toa risiti
 
Hizo Dharau zao zinawafanya wafanyabiashara wawaone Kama maadui. Matokeo yake ndiyo haya tunayoyaona Leo. Wao hawajui kuwa wafanyabiashara wanajua mambo mengi kuliko wao na hivyo walitakiwa kuwa marafiki wao wakubwa ili kupanga mbinu namna ya kuisaidia Nchi.

Binafsi nakiri kwamba ktk mkakati wa kuhakikisha Bandari ya Tanga inakufa kiuchumi Mimi nilishiriki Kama kinara namba moja. Master plan. Na kilichosababosha ni dharau ya kamishna mmoja tu aliyekuwa pale wakati ule. Na nilimtaarifu wazi wazi kwamba, kwa kuwa amenidharau kwa kiwango kile nilitaka kumwonyesha kuwa najua mambo mengi kuliko yeye. Na baada ya miezi 6 tu bandari ilikufa. Mpaka Leo, ananiita Kamanda . Na sasa hivi kazi Hana. Anatia huruma. Na mpaka Leo bandari ya Tanga iko hoi. Kifupi sipendi dharau!. Na nikiamua iamke pia itaamka. Ni Suala la ushirikiano tu.
 
Mkuu hili jambo siyo la kumwachia Raisi peke yake. Yeye mwenyewe linamkera sana, ndiyo maana kila Siku anawatumbua, bahati mbaya kila anayemuweka ni bomu
Kwahiyo wasikusanye kodi kama anavyotaka?
 
TRA lazima wajipange sana Mkuu. Hawa watu bado wanatumia ule mfumo wa tangu tumepata Uhuru. Hawataki kabisa kubadilika kwenda na mfumo wa uchumi wa ushindani wa Dunia ya sasa. Wenzetu Kenya na Uganda wamebadilika sana. Pamoja na sheria za kodi za East Africa lakini nakuhakikishia hii sheria ni kiini macho tu. Kenya na Uganda hawafuati kabisa hizi sheria. Wao wanafata matakwa ya wafanyabiashara wao.

Ndiyo maana unaona k,koo imekufa. Wateja wote wa Zambia Malawi Zaire wamehamia Nairobi. Kampala Nenda utawakuta wamejaa Mahotellini usiku. Mchana wanafungasha tu mizigo. Shida waliyonayo hawa TRA wa Tanzania ni kubwa kuliko Raisi anavyofikiria.
Ila unajua kuwa kuwa tra wao wanafuata na wanasimamia sheria ya Kodi.... Sheria inatungwa na serikali kupitia wizara ya fedha na uchumi na zingine shirikishi kisha inapelekwa bungeni Kama mswada huko inajadiliwa(kuongezewa/kupunguzwa nyama) kisha baada ya kulidhiwa kuwa sheria inapelekwa kwa Raisi isainiwe kuwa sheria rasmi, tra ndo inaanza kuifuta na kuhakikishwa Ina tekelezwa....

Kwahiyo kuwawekea lawama zote TRA
 
Juzi Alhamisi nimeshuhudia mwenyewe. Mwanzoni nilikuwa siamini nikijua ni siasa tu, nikiwa katikati ya Jiji la Kampala wakati wa lunch time ktk mgahawa mmoja nilikutana na Wafanyabiashara watatu Watanzania. Nilikuwa nimekaa meza ya jirani na wao, niliposikia Kiswahili chao fasaha nikagundua hawa ni ndugu zangu wa Home, nikasogea tukakaa pamoja, hapo ndipo Mazungumzo yakaanza.

Ktk maongezi kila mmoja wetu alijitambulisha ni nani na amefata nini Kampala, wao walisema kuna bidhaa huwa wanazichukua Kampala na kuzipeleka Tanzania. Aina ya bidhaa sitazitaja. Lakini ni bidhaa hizi hizi za kawaida zinazotoka China na Zimepitia bandari ya Dar kuja Kampala. Nilijaribu kuwadadisi ya kwamba kwanini wasinunue Dar wakati pia zipo, walijibu bei ni kubwa sana na haiwezi kuwalipa.

Tuliongea mengi sana. Lakini nilichogundua ni kwamba, aidha kuna mkakati wa Makusudi wa baadhi ya watendaji wa TRA wa kuhakikisha kwamba hakuna mfanyabiashara wa Tanzania atakayefanikiwa kibiashara. Kwa sababu haiwezekani Bidhaa inayotoka China kupitia bandari yetu halafu iuzwe kwa bei ya chini Kampala kuliko Dar.halafu wafanyabiashara wetu waifate Kampala na kuirudisha Dar na waiuze Dar na kupata faida kuliko Yule Mtanzania aliyenunua bidhaa hiyo hiyo China na akaipitisha bandarini dar na akaiuza Dar.

Madhara yanayosababishwa na Hawa Majini TRA ni makubwa sana tofauti na wenye akili ndogo wanavyofikiria. Nitayataja baadhi.

1 Wafanyabiashara majirani zetu ambao hawana bandari wamekoma kuja Tanzania

1 Wafanyabiasha wetu haswa wa Soko letu kubwa la Kimataifa k,koo wako hoi kiuchumi

3 Wenye Mahotel ambao target Yao ilikuwa ni kuwapokea wageni kutoka Zaire, Malawi, Zambia,
Burundi, Rwanda, lazima watafilisika kwa kukosa wateja.

4 Wenye Restaurant wengi watafunga kwa kukosa wateja. Na hivyo wafanyakazi wengi
Watapoteza ajira.

5 Wabeba mizigo Ajira zao zitakufa rasmi hawa ni kuanzia wale Vibega, matoroli, bajaji, kirikuu, Canter
Fuso malori nk, hii cheni ni kubwa

6 Mama lishe biashara sitadoda.

7 TRA wenyewe hawatoweza kukusanya tena kodi kwa sababu biashara wameua wenyewe.

Maoni yangu,

Pamoja na Raisi kukaa na wafanyabiashara wachache, pia ni lazima TRA wenyewe wakae na Wafanyabiashara haswa wale wanao import bidhaa toka Nchi mbali mbali Duniani. Ili kupanga namna na viwango bora vya kulipa kodi.

TRA ni lazima iwe inawapeleka baadhi ya wafanyakazi wake nje kujifunza ktk Nchi Kama Dubai , Hong Kong, China Uganda South Africa, kuona wao wamewezaje kufanikiwa ktk Suala la kodi kwa kiasi hicho na Kufanya hizo Nchi Wafanyabiashara wakawa na furaha.
Tatizo siyo TRA tatizo lipo kwa rais wako na waziri wa fedha. TRA hawajitungii kodi, ila wanapata pressure kutoka kwa Magufuli. Magufuli anatumia pesa za watanzania bila kufuata kanuni za matumizi ndio maana kodi hata TRA wakusanye VP hazitoshi. Vile vile ujue kwamba nchi za magharibi wamesitisha kutoa misaada kutokana na utawala wa Magufuli ya kuua na kuwafunga watanzania. Na uchaguzi wa Zanzibar 2015 nayo imechangia kwani walimnyang'anya Maalim Seif urais. Hivyo usiwalaumu sana TRA chanzo ya matatizo ni Magufuli. Na bado 2020 kama atarudi madarakani mtakula madaraja kuanza na ya salender
 
Nakubaliana na wewe mkuu, Dawa ni kupanga safu mpya kabisa. Hawa waliokuwepo ni mtandao wa Kishetani. Ni watu wenye Choyo wivu na Roho za kwanini kwa wafanyabiashara wa Nchi Hii. Pls, Mheshimiwa Raisi. Fukuza haraka hawa watu, hawana wanachokusaidia, wameshakujengea uadui mkubwa na Wafanyabiasha.
Yeye anasema kodi,anasema hivyo sasa sisi tufanyeje?
 
Kwenye Korosho, Mimi nilishakuja na Mada hapa. Kwamba. Waliomshauri Raisi, wanatakiwa kuwa Gerezani na Viboko Juu. Kumbuka Raisi siyo mfanyabiashara, ila Ana washauri wa biashara na mishahara wanalipwa. Hawa hawana tofauti yoyote na Wahujumu uchumi.
Huu ni unafiki wa juu sana,wakati anasema yeye anajua kila kitu na ataki ushauri ulikua bado ujazaliwa?
 
Mimi hapo napishana na wewe Mkuu, kwa sababu Kama ni juhudi za kuwatumbua Mbona anafanya kila Siku? Angekuwa anafurahia wala asingepata Muda wa kukaa na wafanyabiashara . Tatizo lipo hapo hapo TRA tu.
Kuna kitu kinaitwa earning of political credibility. Kwani mkuu hujasikia atakutana na wadau wa korosho Mtwara? Lets wait and observe what will happen alafu tutakutana tena hapa
 
Umezunguak sana lakini lengo lako ni kulaumu TRA na huenda wewe ni mkwepa kodi mzoefu uliyekumbwa na kimbunga. Kama unabisha toa info zifuatazo ku-justfy ulichoandika.
1. Walifuata bidhaa gani na huko zinauzwa bei gani. Ukitoa detail tutaweza kweli ku-compare bai ya hapa kwetu na ya Kampala. Na unajua kabisa umeacha kuzitaja hizo bidhaa makusudi kwa sababu unaumbuliwa!
Hizi ndiyo naziitaga dharau.na watu dizain hii ndiyo wanaokwamisha mambo. Kama ninachosema ni uongo au ni mkwepa kodi, basi hata Raisi asingemfukuza kamishna wa kodi. Kifupi ni kwamba ukimuona Raisi anachukua action kubwa namna ile, jua hajakurupuka.
 
Umezunguak sana lakini lengo lako ni kulaumu TRA na huenda wewe ni mkwepa kodi mzoefu uliyekumbwa na kimbunga. Kama unabisha toa info zifuatazo ku-justfy ulichoandika.
1. Walifuata bidhaa gani na huko zinauzwa bei gani. Ukitoa detail tutaweza kweli ku-compare bai ya hapa kwetu na ya Kampala. Na unajua kabisa umeacha kuzitaja hizo bidhaa makusudi kwa sababu unaumbuliwa!
Mkuu sema nawe unataka ukijua basi uanze kwenda Kampala kuleta hiyo mitonyo
 
Wenzetu wanatengeneza pesa sisi tumebaki na maneno tu ya kila Siku, Tanzania Nchi ya Amani.Mh!
 
Ni kweli mkuu, yeye ndiye anayetoa target. Lakini kumbuka hata huyu anayepewa target ni lazima awe na akili ya kukusanya kodi na kuiboresha hali ya huyo anayemlipa kodi. Ili mwakani akusanye zaidi. Sasa Kama unakusanya kodi na huyu anayekupa kodi unamwacha hoi masikini, unategemea nini mwakani? Bado kuna tatizo kubwa.
Usihamishe goli mzee, chukulia mfano mimi ni boss wako nimeakuambia kesho asubui andikia flan na flan barua ya kuwaachisha kazi, utaitikia alafu usiandike na badala yake uanze kutafuta sababu za mm kuwasimamisha kazi?? Mbona wakt wa jk hatukuyaona haya.
 
Back
Top Bottom