KERO Nchi hii Dharau zimezidi! Watumishi wa serikali Vyeo sio Misifa, ni Dhamana

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mwadu Nkuva 2

Member
Mar 1, 2024
6
4
Dhahiri shahiri bila kupepesa macho nanyoosha malalamiko yangu Ofisi ya halmashauri Njombe mjini Kuwa Cheo ni Dhamana sio sifa na lawama hizi ziende moja kwa moja kwenye kitengo cha NIDA, Mjue tumeteseka Mashambani na makazini na viwandani, mikono yetu ikapasuka pasuka kwa kazi ngumu tukajituma kwa kila hali sasa ninapokuja ofisini unanisubirisha bila kujali Kuwa unanichelewesha hakuna unachofanya ila kuzurula kwenye korido, na Mwendo wa madaha ama kweli ukipata basi matako hulia bwata . Sio mbaya nakusubiria haya sasa huishi kunirusha kalenda njoo kesho, nilikua kwenye kikao, oh sijui kuna....

Sababu haziiishi Loooh! Vikao Gani kila siku hatariiiiiii Hii haya ukichoka Kukiona sura yangu sasa niweke kidole kwenye mashine Naambulia matusi Futa majasho Yako kwenye vidole, huna hata lugha ya staha nimefuta sawa! Gandamiza kidole chako kama umekula! Harafu mnaishia kuchekeshana kitakua kina magaga! Sijapenda hata kidogo! Uhuru wenu kufanya chochote kwenye kazi Vyeo taaluma na nyadhifa zenu usiwe msalaba kwetu! Inakera Sana!

Lawama hizi ziende kwenye Ofisi za Vyeti vya kuzaliwa Njombe mjini ! Mchezo wenu tumeujua hizo Nenda rudi tushazichoka kwa mujibu wa Utaratibu cheti Lazima kukamilike Ndani ya siku saba. Malipo nimekamilisha haitoshi na Risiti nimekata , Eti pesa imepotea kwenye Mfumo , pesa Gani inayopotea kwenye Mfumo inanisikitisha kwa kweli iko wazi huu ni mchezo wa kutafuta chai au kuwafanya watu wazunguke mbuyu!

TAKUKURU nchi hii Ingekuwa yenu hamna mnachofanya! KAZI kutufundisha kwenye Club tuache Rushwa mnamkanya perege kuacha usumbufu Huku mkisifia usumbufu wa mapapa mapapa au mnasubiri mko kama Mkia wa n'gombe popote penye maziwa mko nyuma hata ni Karibu na harufu mbaya ya kinyesi sisemi zaidi ? Ila hamfanyi kazi Sijui mnasubiri maagizo toka Juu , au ziara za Makonda zije Ndo mshtuke kutoka usingizini mnaota Ndoto Gani! Nchi inapigwa na Rushwa Juu chini!

Ole wenu! Badilikeni mapema kabla kiama chenu hakijafika Nawaonya! iiiiiiiiih!
 
Back
Top Bottom