Nchi haina NDEGE ila Rais ana NDEGE

Nchi haina NDEGE ila Rais ana NDEGE

harafu kenya airways wanatangaza humu jamii forums angalieni chini, kule ndo kuona viongozi huku kuna vioo ndozi.
 
Elewa hapa hoja ni 'nchi haina ndege za kibiashara bali ndege ya rais' alafu kwa swali lako Botswana haina ndege ya rais ila wana ndege za taifa lao japo pato lao ni kubwa kuliko letu.
...Tatizo hapa ni la kisemantic. Kinachoitwa 'ndege ya rais' si chengine bali ni ndege ya serikali maalum kwa ajili ya safari za viongozi wa juu. Nchi karibu nyingi zinazojijali zina ndege maalum kwa ajili ya viongozi wake ambazo ni alama za taifa hilo! ndoo maana Ben aliyenunua ndege ya sasa hakuondokanayo baada ya kumaliza muda wake! na JK hataondokanayo atakapohitimisha awamu yake... suala la msingi ni jinsi inavyotumika!
 
I do not mean to be rude but Mwandishi alipaswa kutumia jina zima la huyo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji throughout the article kwa sababu anapoandika 'Chizi' peke yake ananikwaza.
Tukumbuke tunaongelea ATCL kubaki shirika la ndege bila kuwa na vitendea kazi vya kufanikisha utolewaji wa huduma ya usafiri wa anga ambayo ndiyo core b'ness.
Halafu unasoma maelezo ya utetezi yanatolewa na 'Chizi'.I've failed to tame my sense of humor.

Nautakia kila la kheri uongozi wa ATCL katika kuendelea kuitia serikali gharama ya kukodi ndege kutoka kwa mashirika binafsi kwa kodi za watanzania ili kujionyesha kwamba wako hai ilhali ni maiti.
Pia ukarabati mwema wa hiyo scrap moja iliyobakia.

Miaka 50 ya uhuru.Wamethubutu kufilisi ATCL kwa ufisadi na hujuma,wanaweza kuendelea kuwabebesha mzigo walipa kodi na wanasonga mbele bila ya kuwa na ndege.
CCM Oyeee!!

Ushauri wangu kwa nini isichukuliwe ndege ya Rais ikawa inatumika kitaifa badala ya
kutokuwa na ndege hata moja,kwani yaonekana kurusha ndege hadi Brazil kwa rais na wapambe wachache haina tija.
ukizingatia amekwenda na mke wake wa nini wakati ameenda kikazi.ni vizuri akafeel pinch naye kwamba tumefika mahali pabaya kama nchi. akapanda ndege na watu wengine na wakimuuliza yeye nani akiri na kusema ni Rais wa Tanzania na nchi
yake haina ndege inabidi apande kama raia wa kawaida.
 
Labda mwenye kufahamu zaidi atujuze ni nchi gani aina ndege ya Rais tuinge mfano
Nchini za Ulaya hazina ndege za raisi isipokuwa Marekeni ina AIRFORCE1 na ziko mbili
zina ndege ya raisi. China, India, Uk viongozi wa nchi hukodisha national carrier kwenye ziara za Kimataifa
 
Obama kama maraisi wengine wana ndege inaitwa Airforce one ndo hiyo nayoitumia kwenye avata yangu.Na marekani kama marekani wana shirika la ndege strong linaitwa America Airline
hakuna kitu kinaitwa "America Airline"!!!

America hawana ndege. Nini ndege, hawana hata basi la serikali la biashara.

Hawana dhana za zama za kale za kisoshalisti za serikali kumiliki njia kuu za uchumi.
 
Back
Top Bottom