Nchi gani hii?

Nchi gani hii?

Tuanzishe soko la konokono tanzania tuwauze nje hii itasaidia kupunguza tatizo la ajira huku si hatuwatumii
 
hiyi kitu west africa wanakula matajiri tu, maskini hawezi kumudu gharama yake. hata akikamata bora akauze apate mpunga wa kutosha kutimiza mahitaji ya lazima kwake. Wenyewe wanaita ni delicacy food
 
288f69d0d3d6a08bd0b6f938eb08fea0.jpg
Hiki kitakuwa ni kilimo cha konokono..
 
Hiyo ni fursa nzuri sana kwa sasa ambayo haihitaji mtaji mkubwa. Kenya wanaitumia vizuri sana.
 
China hawezi ikusanya kwa kutumia vyombo kama hivyo, yaani China ukibahatika kupewa chakula cha hiyo kitu, ufahamu kuwa wewe wamekuheshimu sana, kumbuka hiyo ni sea food ambayo ni ghali sana. Kuna kipindi nilifanya internship katika mji fulani unaitwa Jiian, siku ya kutukaribisha wakatwambia wataandaa sea food kwa heshima yetu, tulipoenda mezani hiyo kitu ilikuwa ni miongoni mwa chakula, meza ilikuwa ya kuzungusha na kupakua kile unapenda, niliepuka hiyo kitu. Hata hivyo, sikuwa na mood ya kula na nilikuwa nahisi kichefu chefu, mpaka leo sijawahi sahau ile siku.

Mkuu una uhakika hiyo ni sea food? Hembu angalia vyema jombaa
 
Tatizo sisi tumewazoea kuwaona konokono katika hali yao ya utelezi fulani. Lkn hakuna mboga nzuri kama iyo kitu. Hapo Kenya umekua mradi mzuri sana kwa watu walioiona fursa. Mshana ukibahatika kula hii mboga,mbuzi na ndugu zake utawasahau.....
 
Tatizo sisi tumewazoea kuwaona konokono katika hali yao ya utelezi fulani. Lkn hakuna mboga nzuri kama iyo kitu. Hapo Kenya umekua mradi mzuri sana kwa watu walioiona fursa. Mshana ukibahatika kula hii mboga,mbuzi na ndugu zake utawasahau.....
Never on earth
 
Ha ha ha! Kwakua neema ya mboga saba kujisevia ipo una haki kuendelea kuchagua.
 
nahisi ujenzi wa barabara unaendelea hapo kwa hisani ya wale wale wa feki
 
Mkuu una uhakika hiyo ni sea food? Hembu angalia vyema jombaa
Mkuu, kwani hiyo kitu ikipikwa inawekwa kwenye kundi gani la chakula. Mimi huko nilikoikuta ilikuwa iko kwenye kundi la sea food na kilikuwa chakula gali sana, wanakula watu wenye pesa au unaandaliwa kwa heshima kama Mgeni, kiliandaliwa kwenye ajili yetu kama wageni, tulikuwa wanane kutoka nchi za Afrika tuliokuwa masomoni (internship) nchini nchina. Jamaa kutoka Morocco ndo alikifurahia, kesho yake tulimwambia Mratibu (Mwenyeji) kuwa hiyo kitu baadhi yetu sio utamaduni wetu. Walikuwa wanamwandalia Jamaa kutoka Morocco.
 
daah ila kila sehemu na utamaduni wake,kuna mzungu mmoja mmarekani yaani yeye dagaa alikuwa anaona kinyaa kwelikweli na alikuwa anatuona waajabu kula dagaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom