-Niweke Sawa hapo kwanza.
Chogo hupenda kuita mtu yoyote wa Bara,ukisikia Chogo ujue ni wa Bara,wakina na maana kwamba Asili ya Watu wa bara vichwa vyao ni Vichogo.
-Kuhusu Guest inategemea ulienda Vipi,wakiona umekaa kihatari hatari hata Dar hawawezi kukupa
Pale Adams Inn kwanza sio watu wa kuhoji Saana,maana Pale ni Bandarini,ila usalama wa kila mgeni ni juu yao.Na ndio maana inabidi wakuulize kama mgeni wa kawaida wakati wa kucheck in na kama wana daubt basi watakuuliza masuali ya Ziada
Utakumbuka kwamba pale Adams Inn kuna Guest inaitwa Malindi inaelekezana na Adams Inn,kuna jamaa alikuja haeleweki,akakodi chumba,na chumba chake alilocate chumba kilichopo juu ya Duka la Sim,basi ailipofika usiku,akaja na wageni wake,wakaingia room kumbe walienda kutoboa zege na kudongokea kwenye duka la sim na kuiba simu kibaooo.Sasa hadhari ni muhim mkuu
Ila Guests Houses na sehem zote za kulaza wageni hazina ubaguzi,na ifahamike kwamba ubaguzi mwingine ni wewe baada ya kujishuku.Watakubagua vipi wakati wana Room`s Rates za Foreigners na Resident.
ATM ya Umoja,kwanza kama unauliza bila kusalimia hatamie sikujibu.
Ila vijana wa Pale forodhani ni Wastaarabu wengi wao,wewe ungeuliza hata Driver Tax angekuelekeza,sasa kama umeenda na mbwembwe zako kama Bill Gate na kuuliza tu watakuzingua tu lazima,na unabahati wanatabia ya kuku locate mbaliii kama ukifanya madharau.
Kuhusu kumuuliza huyo Mama,ni kwamba hata vijana wa kawaida wangpata tabu kukujibu ilipo ATM ya UMOJA,wewe mama anauza maandazi unategemea mambo hayo ya Bank.Huyo mama hata neno ATM halijui maana yake,anajua,usilaumu kila kitu mkuu,lazima uendane na uhalisia,ni ATM Chache sana za Umoja na almost kama zote zipo chini ya PBZ(People`s Bank of Zanzibar)
Kuhusu kuambiwa Camera haizwi,hii ni umetia chumvi nyingi saana,inawezekana ikawa hauzwi kweli,maana sio kila kitu ukiona dukani kinauzwa,na Wafanyabiashara wanaangalie sana hela,sio salam yako,sasa Suala la Kusalimia ni kuonyesha uungwana tu,ila sio kwamba linafanya mtu asikuuzie Bidhaa
Overall
Inaonekana hata wewe mwenyewe ni Mtata,kwanini yote yatokee kwako?