Nchi 10 zinazoongoza kwa ubaguzi duniani

Nchi 10 zinazoongoza kwa ubaguzi duniani

Iran sio nchi ya kiislamu na hata uislamu wao ni wa kishia umesema sio nchi ya kiislamu then unasema uislamu wao wa kishia sasa hapo huoni kama huo ni ubaguzi???je uislamu halisi ni uislamu upi??mwisho uache itikadi kali
Uislaam wa Kishia hauwezi kuwa Uislaam sawa na Uislaam wa Kibohora !
 
Sasa hapo huoni kama tunabaguana waislamu kwa waislamu???je itakuwaje kuhusu wale wasio waislamu???
Sio kubaguana bali hayo ni madhehebu tuu,kama vile Shia,Sunni,Ibadhi etc, hata kwenye Christianity kuna madhehebu pia,

Sasa kama alivyokwambia Mkuu Bandiwe naamini lengo lake ni kua yaani kuna tofauti kiasi fulani kama ukifananisha mashia na mabohora na ndio maana ni madhehebu tofauti coz yanatofautiana kiasi fulani,

Mfano adhana inayotolewa na Mashia ina utofauti wa maneno fulani ukilinganisha na Adhana ya Dhehebu la Ibadhi,

Hivyo ndivyo nijuavyo mimi,
 
Zanzibar haimo ?.
Babalao kwa UBAGUZI !!
images

Mchana kweupee peee..ilisomeka hivi.. " Machotara "
Last emperor vipi hapo !!
 
Nawasalimia wakuu wangu,

Ningependa tuangalie nchi 10 duniani zinazoongoza kwa ubaguzi wa hali ya juu dhidi ya binadamu wenzao kwa misingi ya rangi za ngozi zao,hali ya kiuchumi,dini,jinsia na asili (nationality).

1) MAREKANI
Marekani ndio kinara wa nchi inayoongoza kwa ubaguzi katika vigezo mbalimbali. Ubaguzi wa kwanza ulianza kwa wamarekani wageni walipookuwa wakiwaua kwa wingi kama nyani wenyeji wenye nchi ambao ni wahindi wekundu (Red Indians),ambapo waliendesha vita mbalimbali za kuwafuta katika nchi ya marekani.
Ubaguzi mwingine mkubwa ni ubaguzi wa rangi kwa watu weusi,kwasababu weusi wengi babu zao walipelekwa huko kama watumwa kwenda kufanya kazi kwenye mashamba ya wazungu na majumbani.Toka enzi hizo mtu mweusi ameonekana kama sio binadamu kamili.Japo ubaguzi wa rangi ulipigwa marufuku miaka mingi iliyopita lakini mpaka sasa kumekuwa na ubaguzi mkubwa ukiendelea.Kuna ubaguzi mwingine ambao ni wa kisiasa..nafasi nyingi za nchi kama mahakama kuu,jeshini,CIA,serikalini kumekuwa na ubaguzi nafasi hizo zishikiliwe na watu weupe ilikudumisha (white supremacy),pia ubaguzi umekuwepo wa kijamii,kidini,kiuchumi na mfumo wa kumiliki nyumba.Mpaka sasa kuna watu weupe wanathamini mbwa na farasi wao kuliko binadamu wenzao.

2) SAUDI ARABIA
Hii ndo nchi inayosemekana inaongoza kwa ubaguzi duniani kwa hali ya juu, ule wa wazi wazi na wa moja kwa moja bila hata kujaribu kufichaficha. Wenyeji wa Saudi Arabia hawapo tayari kuona mgeni akiwa anamiliki vitu vya kifahari kuliko wao kama magari,nyumba nk..uvumilivu huo hawana. Wanawake wa Kisaudia wamekatazwa wasiolewe na mgeni wa kutoka mataifa mengine,wakati wanaume wa Kisaudi wapo huru kuoa yoyote wanaetaka.Wanawake wa saudia hawaruhusiwi kuendesha magari na kama anatakiwa kutoa ushahidi mahakamani inatakiwa atafute mwanaume amuwakilishe,na akilazimika sana,ushahidi wa wanawake wawili ndo unalinganishwa wa mwanaume mmoja. Mgeni haruhusiwi kununua mali yoyote hata kama ni nyumba bila kumshirikisha mgeni. Mgeni hafikiriwi kupata kazi nzuri yoyote zaidi ya Msaudi,haijalishi ana vigezo na elimu kiasi gani. Ni ngumu kupata uraia wa nchi hii hata kama umeishi muda mrefu kiasi gani,mgeni katika nchi hii unachukuliwa kama mtumwa tu. Raia wake wanadharau kubwa sana kwa binadamu wengine.

3) INDIA
Wahindi wanaanza 'kwa kumalizana' kubaguana wao kwa wao kabla hawajaanza na mgeni.Wanaanza kubaguana kwa tofauti ya dini zao(muslim,buddha,sikh,hindu etc)..hii husababisha mauaji makubwa ya halaiki kwa kubaguana tu.Halafu wanaanza kubaguana kwa ukanda..wahindi waliotoka kusini ni masikini sanakuliko wa kaskazini,kusini ni eneo linaloongoza kwa watu kujiua (suicide) kwaajili ya njaa,dhiki na madeni. Halaf wanafata kubaguana kwa sababu ya rangi,mhindi mwenye ngozi nyeusi anabaguliwa sana na wahindi wenzake,kuna baadhi ya wahindi weupe kutoka kwenye matabaka ya juu hawako tayari kuongea na mhindi mwenye rangi nyeusi.
Wahindi pia wanabaguana kwa kufuata madaraja matatu ya binadamu (caste),ambayo raia yoyote anayeangukia katika madaraja hayo sio rahisi kuchomoka,maana yamewekwa katika mfumo wa miaka maelfu na maelfu na watu wanajuana.Madaraja hayo ni
i) Daraja la juu(Brahamans)- Hawa ndio wale ambao ni matajiri vizazi na vizazi,wafanyabiashara wa dhahabu,chuma na wamilki wa utajiri wa aina mbalimbali (Hawa nao wamo katika makabila 12 na kila kabila limespecialize katika biashara fulani toka dahari)
ii) Daraja la kati- Hawa ni wale wamilki wa uchumi wa kati (mabucha,saloni,garage,seremala nk)
iii) Daraja la chini-Hawa ni wale kajamba nani ambao ni masikini na wanafanya kazi za chini kama kushona viatu,kubeba mizigo,kuosha vyoo nk..
Sasa hao ambao ni daraja la chini 'low caste' au 'untouchable' kama wanavyoitwa,wananyanyapaliwa kiasi kuna mtu anaona hata kuwapa mkono tu ni kujitafutia mikosi..na ndio kundi kubwa kuliko hayo mengine.

4) ISRAEL
Wayahudi wana sera yao ya kibaguzi ya kizayuni(zionism),ambayo Fuadmondeo anakaririwa akisema "Uzayuni ni mfumo mbaya na wa ubaguzi kuliko wote duniani".Wazayuni wanaamini wao ndio watoto wa Mungu na ni bora kuliko binadamu wengine wote.Wayahudi Waisrael wanawabagua waisrael wenzao kutoka Ethiopia,ambao ni kizazi cha nabii Suleiman na Malkia wa Sheba.Wamekuwa pia wakiwabagua majirani zao na watu mbalimbali kutokana na imani yao ya kizayuni.

5) AUSTRALIA
Waustralia ni wabaguzi kwa wenyeji wao waliowakuta katika ardhi ya Australia ambao wanaitwa Aborigines.Mpaka kufikia mwaka 1969 waustralia walikuwa hawawatambui wenyeji wao na walikuwa wakifanya vita na kuwaua.Pia hata sasa kumekuwa na ubaguzi kwa watu wanaotoka Asia na Afrika, kuna maeneo kama beach na maduka hawawahudumii watu weusi.

6) Serbia
Nchi nyingi za ulaya mashariki zimekuwa zina ubaguzi wa hali ya juu kwa watu weusi,ajabu ni nchi masikini tu lakini Serbia nayo ni kinara wa ubaguzi duniani.

7) UJERUMANI
Wajerumani ni wabaguzi wakubwa, huwa wanajitapa waziwazi kuwa Mungu alivyoanza kuumba binadamu alianza kwa kuwaumba wao wadachi kwanza (Aryan race).Wanaamini wao ndio uzao bora zaidi duniani,ni watu wenye superiority complex. Kitendo cha dunia nzima 'kuwachangia kuwapiga' katika vita kuu mbili za dunia na bado wakajijenga tena mpaka kuwa taifa tajiri lenye nguvu ya uchumi kuliko nchi yoyote ya ulaya, inawafanya wajione wao ni superior race.Hii huwafanya kuwadharau watu wa mataifa mengine.

8) KOREA KASKAZINI
Nchi hii ina ubaguzi mkubwa..hii inaweza kuwa ni kwa sababu ya itikadi na propaganda za serikali yao na pia kwaajili ya kukosa mwingiliano na mataifa mengine.Inawabagua watu wa Korea kusini na watu wa mataifa mengine ya Asia na Afrika.

9) ARGENTINA
Katika nchi ya Argentina kuna ubaguzi mkubwa kwa misingi ya dini,rangi,jinsia nk.Pia wanawabagua walatini wenzao vibaya na watu weusi.

10) URUSI
Urusi pia inaingia kwenye orodha ya nchi yenye ubaguzi kwa watu weusi na hata wazungu wenzao wa mataifa mengine.
MKUU TUNAOMBA MAREJEO YA HABARI YAKO
 
Nini maana ya ubaguzi? Mtu akisema ukweli ni mbaguzi? Ni kweli waarabu ni uncevilised na watu wa mavurugu yasiyo na sababu za msingi
.........kuna Muarabu mwenye mabomu ya Nuclear !? ....au una chuki nao tuu !??
 
Kuna wamerekani weusi,walizaliwa huko.Mbona hatuoni waarabu weusi kule kwao uarabuni wakati nao walijihusha vizuri na biashara ya watumwa?
Waarabu weusi wapo wengi tu, ila ujue Muarabu alikuwa mchuuzi wa Watumwa na Mzungu ndiye mnunuaji na Kanisa linakula commission, kwa ajili ya nguvu kazi ya kulima mashamba ya tumbaku kule Virginia na mashamba ya miwa. Muarabu hakuwa na shamba wala kiwanda.
Kwa taarifa yako, kwa taratibu za Dini ya Kiislaam, Mtumwa akisilimu, anatoka utumwani moja kwa moja na anakuwa na haki sawa na Tajiri yake. Ndio Maana nchi zote zenye asilia ya Uislaam hakukuwa na struggle ya Blacks kulilia haki. LOTH HEMA
 
List na huo utafiti ni fake, utafiti ungeenda kisayansi na ukusanyaji bira wa data Kenya isingekosekana kwenye hiyo liist
Tuwe na hofu ya Mungu. Kabla ya kutoa kilichomo machoni mwa wengine tutoe kwanza boriti machoni mwetu. Hata Tanzania kuna ubaguzi wa aina nyingi sana, udini, ukabila, walionacho dhidi wa wasionacho.
 
Back
Top Bottom