Mimi nimewahi fika Kenya, Marekani na Qatar, lakini sijawahi kubaguliwa huko. Mara pekee niliyowahi kubaguliwa maishani, nilienda Zanzibar.....sitaraji kwenda tena.
Waliniita chogo, sijui maana yake kwa kiswahili lkn nafikiri wanamaanisha kafiri. Kila guest house nilikoenda waliniambia vyumba vimejaa, mpk teja mmoja pale ferry akanipeleka Adams Inn, ndio nikalala hapo baada ya yeye kunisaidia kujieleza.
Asubuhi nilitafuta ATM ya UMOJA, nikamuuliza kijana mmoja pale Forodhani, akaniambia yeye sio kazi yake kuelekeza watu. Nilifanikiwa kusogea maeneo ya karibu na lilipokuwa soko la watumwa, kuna benki pale ya FBME, nikamuuliza mama mmoja akasema haijui na hajapata kuisikia. Baadaye FFU mmoja alinielekeza, kwa maajabu...ni jengo hilo hilo alilokaa huyo mama akiuza vitafunio.
Kama haitoshi, pale darajani niliona video camera ya mtumba inauzwa, nilipouliza bei nikaambiwa haiuzwi. Dalali aliniambia siku nyingine nijifunze kusalimia kistaarabu kama nataka kuhudumiwa.
Jamani, Waarabu wa Qatar ni wakarimu sijapata kuona. Americans hawana time na mtu. Usimuulize kitu Black America, atakujibu huku anaenda hata hutaelewa alichosema.