Beberu Mwitu
JF-Expert Member
- Mar 31, 2019
- 491
- 692
Habari za muda huu ndugu wana jukwaa.
Niende moja kwa moja kwenye mada; nilihitimu kidato cha sita mwaka 2014 mchepuo wa PCM na kupata alama zifuatazo;
Physics- D
Chemistry- E
Advanced Mathematics-E
General Studies- D ( japo haina maana).
Baada ya matokeo hayo yasiyoridhisha nikajikatia tamaa mpaka mwaka 2019 nilipoamua kusomea ualimu wa shule ya msingi daraja la III A na mwaka huu nimeajiriwa Serikalini.
Niwe mkweli tu; hii kazi siifurahii hata kidogo. Natamani sana kuwa mtaalamu wa masuala ya sayansi kama vile mambo ya mazingira, maliasili na Uhandisi lakini si ualimu. Kikwazo kilichopo ni hizo alama za mtihani hapo juu.
Ningependa kujua kama alama nilizozipata A’level zinaweza kunisaidia kusomea Stashahada za Sayansi nilizozitaja hapo juu huku nikiendelea na kazi hasa nyakati za jioni au blended mode. Nafahamu ufaulu wangu wa O’level unaniwezesha kusoma stashahada ya kozi hizo kwa muda wa miaka mitatu(Full time), kitu ambacho ni kigumu kwangu kwa sababu muda wa asubuhi mpaka mchana nitakuwa kazini . Ufaulu wangu wa O’level ulikuwa kama ifuatavyo kwa masomo ya Sayansi;
Engineering Science- C
Basic Mathematics- C
Chemistry- B
na masomo ya ufundi ufaulu wake ulikuwa hivi;
Building Construction-C
Surveying- B
Architectural Draughting- C
NB: Biology sikusoma na badala yake nilisoma Geography ambayo nilipata alama D kwa O’ level.
Na kwa sasa nimepata selection pale Open University kusomea Diploma in Primary Teacher Education ingawa sioni hii ikinipeleka kwenye Science Courses hapo baadaye.
Naomba ushauri tafadhali kabla sijachelewa kutoka kwenu wanajukwaa. Naamini kuna wataalamu wengi sana humu ndani na wengine ni wakufunzi kabisa. Je, naweza kupata kozi ya sayansi na kuisoma nyakati za jioni au kwa mfumo wa elimu ya masafa?,
Vipi kuhusu Foundation course?
Shukrani sana.
Niende moja kwa moja kwenye mada; nilihitimu kidato cha sita mwaka 2014 mchepuo wa PCM na kupata alama zifuatazo;
Physics- D
Chemistry- E
Advanced Mathematics-E
General Studies- D ( japo haina maana).
Baada ya matokeo hayo yasiyoridhisha nikajikatia tamaa mpaka mwaka 2019 nilipoamua kusomea ualimu wa shule ya msingi daraja la III A na mwaka huu nimeajiriwa Serikalini.
Niwe mkweli tu; hii kazi siifurahii hata kidogo. Natamani sana kuwa mtaalamu wa masuala ya sayansi kama vile mambo ya mazingira, maliasili na Uhandisi lakini si ualimu. Kikwazo kilichopo ni hizo alama za mtihani hapo juu.
Ningependa kujua kama alama nilizozipata A’level zinaweza kunisaidia kusomea Stashahada za Sayansi nilizozitaja hapo juu huku nikiendelea na kazi hasa nyakati za jioni au blended mode. Nafahamu ufaulu wangu wa O’level unaniwezesha kusoma stashahada ya kozi hizo kwa muda wa miaka mitatu(Full time), kitu ambacho ni kigumu kwangu kwa sababu muda wa asubuhi mpaka mchana nitakuwa kazini . Ufaulu wangu wa O’level ulikuwa kama ifuatavyo kwa masomo ya Sayansi;
Engineering Science- C
Basic Mathematics- C
Chemistry- B
na masomo ya ufundi ufaulu wake ulikuwa hivi;
Building Construction-C
Surveying- B
Architectural Draughting- C
NB: Biology sikusoma na badala yake nilisoma Geography ambayo nilipata alama D kwa O’ level.
Na kwa sasa nimepata selection pale Open University kusomea Diploma in Primary Teacher Education ingawa sioni hii ikinipeleka kwenye Science Courses hapo baadaye.
Naomba ushauri tafadhali kabla sijachelewa kutoka kwenu wanajukwaa. Naamini kuna wataalamu wengi sana humu ndani na wengine ni wakufunzi kabisa. Je, naweza kupata kozi ya sayansi na kuisoma nyakati za jioni au kwa mfumo wa elimu ya masafa?,
Vipi kuhusu Foundation course?
Shukrani sana.