Caroline Danzi
JF-Expert Member
- Dec 19, 2008
- 3,713
- 1,263
Asalam aleykum Jamii,
Nimatumaini yangu amjambo wote ningeomba kuchua wasaa huu kuelezea machache yaliyopo moyoni mwangu!
Ni majuzi tangu nilipoondokewa na mke wangu kipenzi , Subira Alfred Mwamasso mnamo wa saa 09:27hrs tarehe 31.Katika Hosptali ya Taifa Muhimbili
Napenda kutoa shukurani zangu za dhati kwa wote ambao walikuwa na mimi katika kipindi hiki kigumu na bado wanaoendelea kushirikiana na mimi kwa njia moja au nyingine ningewaomba ni wambie sina chakuwalipa kwa wema mkubwa waliouonyesha kwangu!!Ninawaomba wapokee hii shukurani yangu ya dhati kutoka kwangu kwani nimefarijika kwakiasi kikubwa kwa wale walio bahatika kufika msibani waliona nilikutana na mtu na kujitambulishas yeye ni mwana JF kwa jinsi nilivyo badrika na kuwa nafuraha naye kwakusema ukweli hii ilinifariji sana!!.
Kwakweli nikitu ambacho sikukitegemea mimi binafsi kuwa nitakuja kuwa na marafiki ambo siwakuwai kuwafahamu!Nilidhani rafiki niyule unayekutana naye barabarani,mgahawani,kwenye basi,Baa na sehemu za maofisini na hata kwenye misiba na harusi!!Kumbe la hasha!!
Hata nyuma ya keyboard kuna dunia nyingine inayoishi na inayoweza kuwa msaada mkubwa kwako bila wewe kujitambua!! hasa wewe mhusika utaitumia keyboard kwa uangalifu na kwa umakinai zaidi!!
Ninamengi sana ya kueleza lakini naona siwezi kuyamaliza!!
Hivyo ngoja nifupishe maneno nirudi kule nilikokusudia hapo awali!
********************************************************************************
Napenda niongozwe na utashi wa mwenyezi mungu kwakuwa ndiye amenipa huu uwezo nilionao kwa sasa.
Napenda kutoa shukurani njia moja au nyingine kwa wale wote ambao mliweza kunipa faraja kwenye hiki kipindi kigumu kwangu kwa walenitakao wa sahau nitawaombeni mniwie radhi sana kwani na mimi ni binadamu naweza kughafirika ila na wahaidi kuwa nitakuwa nana UPDATE pale nitakapo kuwa nimekumbuka!
Napenda kutoa shukurani kwa JF Management.
Napenda kutoa shukurani kwa mmoja mmoja kama ifuatavyo:-
(Special Thanks),
Maxence Melo Invisible Kiresua Mtambuzi mamamia YNNAH The Finest Preta Caroline Danzi RR Nicas Mtei TANMO BelindaJacob Dark City Gedeli Mr Rocky FirstLady1 Gaijin Liverpool Chauro Swts The secretary AshaDii afrodenzi tete'a'tete Fixed Point
Kwa wale ambao sijawataja naomba waniwie radhi nikikumbuka nitawaweka hapa!Nimesahau kwa bahati mbaya!
Kila siku ninawaombea wote mlioshirikiana na mimi katika kipindi hiki kizito kwangu napenda kusema
SINA CHA KUWALIPA MUNGU AWAZIDISHIE BARAKA NA HEKIMA
Asanteni wote muendelee na moyo huo!na mungu awabariki awahepushe nakila lilobaya awanyoshee njia.AMAN.
Tuko pamoja kaka. Mungu akutie nguvu. AMEN