UKWELIYAKINIFU
Member
- Oct 6, 2020
- 27
- 50
Na Thadei Ole Mushi.
Kipindi hiki Cha uchaguzi mkuu niuhimu kuwakumbusha watu Mambo muhimu ambayo yanaweza kuwaletea shida wasipoyajua. Kuna baadhi ya wanasiasa wameaacha kunadi sera wao wanasema tusiposhinda tutaandamana na kuleta vurugu. Ni vizuri vijana kufahamu kuwa kuandamana bila ruhusa ni Kujaribu kumpindua Rais aliyepo madarakani na kwa mujibu wa Sheria zetu huo ni uhaini na adhabu yake ni kifo. Vijana wafahamu pia kwamba kumshawishi au Kuchochea vurugu ni uhaini.
Sheria za nchi zinasemaje?
Sheria ya jeshi la Polisi ya mwaka 1961 na marekebisho yake ya mwaka 1995 ambayo kwayo ndio tunayoifuata hadi sasa inatoa njia na namna ya kuendesha maandamano nchini. Inasema nanukuu:-..
(1) Mtu yeyote ambaye ana mpango wa kufanya, kukusanya, kuunda au kupanga mkusanyiko au maandamano ya hadhara , kwa muda usiopungua saa 48 kabla ya mkusanyiko au maandamano kwa muda uliopangwa kuanza, atawasilisha kwa maandishi notisi kuhusu kufanyika kwa mkusanyiko au maandamano hayo kwa afisa polisi msimamizi wa eneo hilo akianisha:-
(a) Sehemu na muda ambao mkutano utafanyika;
(b) Dhumuni kwa ujumla kuhusu mkutano huo; na
(c) Maelezo mengine kama Waziri atakavyotangaza kwa notisi, mara kwa mara kwenye gazeti la Serikali, kuainisha.
(2) Pale ambapo mtu anawasilisha taarifa kulingana na kifungu kidogo cha (1), anaweza kuendelea kuitisha, kukusanya, kuunda au kuandaa mkusanyiko au maandamano hayo kama yalivyopangwa isipokuwa na mpaka atakapopokea amri kutoka kwa afisa polisi msimamizi wa eneo ikielekeza kwamba mkusanyiko au maandamano hayo hayatafanyika kama ilivyotaarifiwa.
(3) Afisa polisi ambaye taarifa imewasilishwa kwake kulingana na kifungu kidogo cha (1), hatatoa amri ya kusitisha chini ya kifungu kidogo cha(2) kulingana na taarifa isipokuwa ameridhika kwamba kufanyika kwa mkusanyiko au maandamano hayo kuna uwezekano wa kusababisha kuvunjika kwa amani au kuathiri usalama wa taifa au kudumisha amri kwa umma au kutumika kwa dhumuni lolote lisilokuwa halali."
Hiyo ndio sheria inayoliongoza jeshi letu la polisi.Kwa maana rahisi maandamano ni mpaka jeshi la polisi likubali na litoe kibali baada ya waandamanaji kuomba kibali hicho.
Kwa vyovyote vile maandamano hayo yanapaswa jeshi la Polisi lijiridhishe pasipo na Shaka kuwa hayatasababisha madhara yoyote na hayata ingilia haki za watu wengine ambao hawataki kuandamana. Huu ni mtego niliokuwa nawaambia...
NINI KINAWEZA KUTOKEA?
Kinachoweza kutokea baada ya katazo la jeshi la Polisi ni watu wenye nia ya kuandamana kutaka kuandamana kwa nguvu. Ukifanya hivyo moja kwa moja utakuwa unatenda kosa la UHAIN ambalo ndio kosa kubwa kuliko yote nchini kwa mujibu wa ibara ya 28 ya katiba yetu.
Sheria inatuambia kwamba kama ukifanya yafuatayo utakuwa umefanya uhaini katika nchi yako.
( a ) Kifungu cha 39 ( 1 ) cha kanuni za adhabu kinasema kuwa mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri ya muungano au popote akajaribu kumuua rais atakuwa ametenda uhaini.
( b ) Pia mtu yeyote aliye ndani ya Jamhuri ya muungano au popote na akaanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya muungano atakuwa naye ametenda kosa la uhaini.
( c ) Mtu yeyote ambaye yuko ndani ya Jamhuri ya muungano au popote ambaye atajenga, kusababisha au kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri, kuhusu kifo, kumlemaza, kumzuia, au kufungwa kwa rais atakuwa ametenda uhaini.
( d ) Mtu yeyote ambaye yuko ndani ya Jamhuri ya muungano au popote ambaye atajenga, kusababisha au kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kumwondoa rais madarakani visivyo halali atakuwa ametenda uhaini.
( e ) Mtu yeyote ambaye yuko ndani ya Jamhuri ya muungano au popote ambaye atajenga, kusababisha au kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kumwondolea rais heshima na jina la mkuu wa nchi, amiri jeshi mkuu, au kiongozi wa serikali atakuwa ametenda kosa la uhaini.
( f ) Mtu yeyote ambaye yuko ndani ya Jamhuri ya muungano ambaye atajenga, kusababisha au kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kupindua serikiali iliyo madarakani, kutishia serikali, bunge au mahakama atakuwa ametenda kosa la uhaini.
Rudia kusoma kipengele D Hadi ukielewe ukishindwa mwite na Mwenzako mkisome kwa pamoja.
Aidha ifahamike kuwa kwa mtu yeyote atakayekutwa na hatia ya kutenda kosa la uhaini adhabu yake ni kifo na sheria hiyo ya kifo imeelezwa katika kifungu cha sheria namba 39 na 40 cha kanuni za adhabu.
Hivyo watanzania kwa umoja wetu tunapaswa kuzijua sheria za nchi yetu ili kuweza kujiepusha kutenda makosa ya jinai dhidi ya nchi yetu.
Wale wanaowachochea kwenye kampeni waambieni Siku hiyo wanayotaka kuandamana waje na familia zao wake Mbele kabisa maana Hao wakishapata Vyeo hulia kivulini, wanasoma shule Bora kabisa, Wana Mali mpaka nje ya nchi, wakiumwa wanatibiwa hospital Bora kabisa. Ukiona familia zao zipo Mbele waungeni mkono.
Ole Mushi.
0712702602
Kipindi hiki Cha uchaguzi mkuu niuhimu kuwakumbusha watu Mambo muhimu ambayo yanaweza kuwaletea shida wasipoyajua. Kuna baadhi ya wanasiasa wameaacha kunadi sera wao wanasema tusiposhinda tutaandamana na kuleta vurugu. Ni vizuri vijana kufahamu kuwa kuandamana bila ruhusa ni Kujaribu kumpindua Rais aliyepo madarakani na kwa mujibu wa Sheria zetu huo ni uhaini na adhabu yake ni kifo. Vijana wafahamu pia kwamba kumshawishi au Kuchochea vurugu ni uhaini.
Sheria za nchi zinasemaje?
Sheria ya jeshi la Polisi ya mwaka 1961 na marekebisho yake ya mwaka 1995 ambayo kwayo ndio tunayoifuata hadi sasa inatoa njia na namna ya kuendesha maandamano nchini. Inasema nanukuu:-..
(1) Mtu yeyote ambaye ana mpango wa kufanya, kukusanya, kuunda au kupanga mkusanyiko au maandamano ya hadhara , kwa muda usiopungua saa 48 kabla ya mkusanyiko au maandamano kwa muda uliopangwa kuanza, atawasilisha kwa maandishi notisi kuhusu kufanyika kwa mkusanyiko au maandamano hayo kwa afisa polisi msimamizi wa eneo hilo akianisha:-
(a) Sehemu na muda ambao mkutano utafanyika;
(b) Dhumuni kwa ujumla kuhusu mkutano huo; na
(c) Maelezo mengine kama Waziri atakavyotangaza kwa notisi, mara kwa mara kwenye gazeti la Serikali, kuainisha.
(2) Pale ambapo mtu anawasilisha taarifa kulingana na kifungu kidogo cha (1), anaweza kuendelea kuitisha, kukusanya, kuunda au kuandaa mkusanyiko au maandamano hayo kama yalivyopangwa isipokuwa na mpaka atakapopokea amri kutoka kwa afisa polisi msimamizi wa eneo ikielekeza kwamba mkusanyiko au maandamano hayo hayatafanyika kama ilivyotaarifiwa.
(3) Afisa polisi ambaye taarifa imewasilishwa kwake kulingana na kifungu kidogo cha (1), hatatoa amri ya kusitisha chini ya kifungu kidogo cha(2) kulingana na taarifa isipokuwa ameridhika kwamba kufanyika kwa mkusanyiko au maandamano hayo kuna uwezekano wa kusababisha kuvunjika kwa amani au kuathiri usalama wa taifa au kudumisha amri kwa umma au kutumika kwa dhumuni lolote lisilokuwa halali."
Hiyo ndio sheria inayoliongoza jeshi letu la polisi.Kwa maana rahisi maandamano ni mpaka jeshi la polisi likubali na litoe kibali baada ya waandamanaji kuomba kibali hicho.
Kwa vyovyote vile maandamano hayo yanapaswa jeshi la Polisi lijiridhishe pasipo na Shaka kuwa hayatasababisha madhara yoyote na hayata ingilia haki za watu wengine ambao hawataki kuandamana. Huu ni mtego niliokuwa nawaambia...
NINI KINAWEZA KUTOKEA?
Kinachoweza kutokea baada ya katazo la jeshi la Polisi ni watu wenye nia ya kuandamana kutaka kuandamana kwa nguvu. Ukifanya hivyo moja kwa moja utakuwa unatenda kosa la UHAIN ambalo ndio kosa kubwa kuliko yote nchini kwa mujibu wa ibara ya 28 ya katiba yetu.
Sheria inatuambia kwamba kama ukifanya yafuatayo utakuwa umefanya uhaini katika nchi yako.
( a ) Kifungu cha 39 ( 1 ) cha kanuni za adhabu kinasema kuwa mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri ya muungano au popote akajaribu kumuua rais atakuwa ametenda uhaini.
( b ) Pia mtu yeyote aliye ndani ya Jamhuri ya muungano au popote na akaanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya muungano atakuwa naye ametenda kosa la uhaini.
( c ) Mtu yeyote ambaye yuko ndani ya Jamhuri ya muungano au popote ambaye atajenga, kusababisha au kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri, kuhusu kifo, kumlemaza, kumzuia, au kufungwa kwa rais atakuwa ametenda uhaini.
( d ) Mtu yeyote ambaye yuko ndani ya Jamhuri ya muungano au popote ambaye atajenga, kusababisha au kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kumwondoa rais madarakani visivyo halali atakuwa ametenda uhaini.
( e ) Mtu yeyote ambaye yuko ndani ya Jamhuri ya muungano au popote ambaye atajenga, kusababisha au kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kumwondolea rais heshima na jina la mkuu wa nchi, amiri jeshi mkuu, au kiongozi wa serikali atakuwa ametenda kosa la uhaini.
( f ) Mtu yeyote ambaye yuko ndani ya Jamhuri ya muungano ambaye atajenga, kusababisha au kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kupindua serikiali iliyo madarakani, kutishia serikali, bunge au mahakama atakuwa ametenda kosa la uhaini.
Rudia kusoma kipengele D Hadi ukielewe ukishindwa mwite na Mwenzako mkisome kwa pamoja.
Aidha ifahamike kuwa kwa mtu yeyote atakayekutwa na hatia ya kutenda kosa la uhaini adhabu yake ni kifo na sheria hiyo ya kifo imeelezwa katika kifungu cha sheria namba 39 na 40 cha kanuni za adhabu.
Hivyo watanzania kwa umoja wetu tunapaswa kuzijua sheria za nchi yetu ili kuweza kujiepusha kutenda makosa ya jinai dhidi ya nchi yetu.
Wale wanaowachochea kwenye kampeni waambieni Siku hiyo wanayotaka kuandamana waje na familia zao wake Mbele kabisa maana Hao wakishapata Vyeo hulia kivulini, wanasoma shule Bora kabisa, Wana Mali mpaka nje ya nchi, wakiumwa wanatibiwa hospital Bora kabisa. Ukiona familia zao zipo Mbele waungeni mkono.
Ole Mushi.
0712702602