Natamani sasa kuolewa

Natamani sasa kuolewa

Usijipe moyo mama et kua MUNGU ni mmoja ndo sbb ya kubadili dini na YESU je nae vipi, kuna tofauti kubwa sana kati ya hizi dini 2 unless useme hata huo ukristo huujui vizuri

Katika mambo ya kushangaza watu wengi hawajui kuwa huwezi kuwa muislam bila kumkubali Yesu.
 
Maamuz ya mwisho n yako lkn kumbuka mapenz yanaishia hapahapa dunian sister huyo jamaa hatakutetea mbingun...na unaweza ukabidili dini kwa sababu ya mtu na bado akakutosa mbelen,hebu tafakari sana kabla hujamkana YESU afu mek sure unaijua vizur iman yako.

Kuwa muislam haimaanishi kumkana Yesu jamani jifunzeni kujua imani zingine ili muwe katika nafasi nzuri ya kutoa maoni.
 
Usitumie huo mstari wa kujifariji,, it doesnt make it ryt. Mungu wetu si wamajaribio, nakubali kabisa kwamba yupo Mungu mmoja anayestahili kuabudiwa kwa dhati but haimaanishi unaweza kumwabudu popote tuu coz ni mmoja.

Unaona tofauti gani kati ya dini ya kikristo na kiislamu? Hauoni utofauti wa kumwabudu Mungu kati ya dini hizo mbili? Hama dini/dhehebu ukiwa umeamua kwa udhati kutoka moyoni mwako sio kwa ajili ya mapenzi uliyenanayo kwa mtu(mpenzi wako). Mara nyingi akili ya mwanadamu inapotamani kufanya jambo basi hutafuta jinsi ya ku-justify maamuzi haya(kama ilivoonekana kwenye hiyo kauli yako)

Tulia, Mwombe Mungu wako akuongoze kwenye maamuzi yako, I am sure He will.

HAPPY HOLLY WEEK
Aiseeee I really appreciate you bidada
 
Ila ukweli ndio huo, muulize muislam yoyote anae jua sharia za kiislam akujuze mkuu muslam hatakiwi kwenda msibani/kumzika mtu asie kuwa muislam, hata kama ni mzazi wako hauruhusiwi kwenda kwenye msiba wake ikiwa yeye amekufa akiwa mkristo!

Sio kweli mkuu fanya utafiti au uliza kabla hujatoa hukumu labda nikuelimisha kidogo kwanza uislam unatoa heshima kwa dini zote na zaidi ukristo na hata wafuasi wa mwanzo wa uislam walipoteswa sana na wapagani wa makka walienda ukimbizini kwa ndugu zao wakristo na wakapewa hifadhi.na Muhammad saw alilipa deni la shukurani la kuwalinda wakristo popote katika Arabia na akaacha usia wa kuwalinda wakristo kwa watakaokuja kuongoza nyuma yake na ndio maana mpaka leo kuna wakristo zaidi ya milioni mia mbili wa madhehebu ya coptic toka mwaka 420 mpaka leo katika Arabia jamani tuzungumze mambo ambayo tuna hakika nayo kuliko chuki tunazopandikizwa kwa maslahi ya wachache.
 
Nawaza mengi apa,,mara naolewa mwaka mmoja anataka aoe mwngne din yake yaruhusu dini yangu nimeikana ntakuwa mgeni wa nani??


Hapo sasa na hilo ndio kubwa, kwenye uislam hakuna mchepuko Kwa wanamme inaruhusiwa, Bali Kwa wana wake tu ndio hairuhusiwi cos mwanamme akichwpuka anaruhusiwa cos wanajua anataka kuoa mke wa pili, make sure ume make your mind puting into consideration the worst scenario kwamba ndio anaoa mke wa tatu, ukiweza kumudu hio basi ujue uko tayari kuolewa au kubadili dini, all the best
 
Haya mahusiano ya hivi mm huwa nayaogopa sana..mbeleni ndoa lazima iwe na vurugu...
Mimi wa dini tofauti ntaishia kummega tu...ikitamkwa ndoa nachapa lapa..!

Kwakwel nimekupenda bure ,bora ww ata unathubutu kuwamega,mm kigezo changu cha kwanza kbl cjampenda mtu ni dini ,akiniambia cjui mm muislamu yaan crudishi kisogo changu tena km ni cmu cpokei yaaan hanion tena ,naepuka kumpenda mtu wa dini tofauti na ya kwangu kuepuka matatizo mwisho wa siku,
 
Kubadili dini siyo tatizo kwangu coz naamini Mungu ni mmoja,,tatizo ni baba yangu ambaye ni mzee wa kanisa??atanikataa kabisa

Sikia sauti hii ya mtu aliye nyikani"USIMWACHE YESU KWA SABABU YA KUOLEWA"
Kumbuka jambo hili usije kusahau,"HUWEZI KUURITHI UFALME WA MUNGU WALA KUMUONA YEYE,PASIPO KUPITIA KWA YESU.
Kaa katika utakatifu,MUNGU atakupa mume mzuri,
WOKOVU/YESU ni zaidi ya kuoa/kuolewa.
Usipoisikia sauti ya MUNGU WAKO,NA WAZAZI WAKO,
Ipo siku utajuta,YESU
WANGU AKUSAIDIE!!
 
Endelea kuota tu kama unshindwa ku-work out tofauti ya dini zenu
 
Yesu alisema anikanae mbele za watu, na mimi nitamkana mbele za baba yangu sasa hapo akili kicwani mwako, ya dunia yanapita tu.
 
haya mambo yapo complicated sana , hapo ufanye maamuz magumu tu uamue moja kuwa kinyume na wazazi kwa sababu ya huyo wanaume au kumuacha mwanaume.
lakini kumbuka mwanaume sio ndugu yako,

mi nakushauri wanaume wapo wengi na Mungu huwa hachelewi, KUWA NA SUBIRA, huo ni mtihani tu Mungu anakupa kukupima imani yako, yupo wa dini yako anaekusubiri,,,ACHANA NA HUYO BEFORE ITS TOO LATE,
 
Mie mkristo pure tena nmelelewa katk din kabsa mwenzang muslim hapo ndo kikwazo

Fungeni ndoa ya kiserekali maana inaruhusu kila m1 kuendelea kubakia na dini yake. Ingekua mie weiyeee ningeshaclozg zaaamani sema tu ndio hivyo bahati bado xna.
 
Ushawah kumgusia huyo mpenz wako yeye kubadili dini akufate,maana kama kwao hawana matatizo ya ye kubadil dini,n bora abadil yeye akufate.Ili msije kosa baraka za baba yako ktk ndoa yenu.Embu ongea naye juu ya hilo
 
Natamani kuolewa sasa jamani,,
Niishi na mume wangu,asubuhi aniamshe twende kazini jion niwahi nyumban nimpikie akija nimfungulie mlango natamani natamani sijui itakuwa tarehe ngapi kikwazo ni dini zetu MUNGU simama sasa !!aaaaaaggg

Kwanza hata huyo mume angekuwa mkristo mwenzio hiyo ndoa ingekushinda mapema maana unaingia kwa sababu batili.

Pili wewe umelelewa kwenye dini na unamuogopa babako, si Yesu. Manake ni kuwa wewe si Mkristo ila umelelewa na wazazi wakristo ila ulipokuwa mkubwa hukumkiri Yesu. Mkristo kwa maana ya mtu aliyemkiri Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake _ kwamba alizaliwa na Bikira Mariam, akateswa, akafa wa ajili yake na kufufuka na baadae akapaa kwenda kumuandalia makao, na kwamba atarudi tena kuhukumu walio na wafu na ameikubali neema ya wokovu- kamwe, lije jua, ije mvua, hawezi kumuacha Yesu kwa ajili ya mume/mke ambaye ni kitu cha muda.

Hata dini yako inakwambia uwaheshimu baba yako na mama yako. Mtoto anayeweza kujinyima furaha ya nafsi yake ili kutekeleza amri hii hakika Mungu hatamuacha. Na wazazi wanakunyima hili kwa WEMA kabisa. Usipoolewa kwa sababu ya kuwaheshimu wazazi na si kuwaogopa utakuwa umefanya jambo sahihi.

Una habari siku utakaposilimishwa utatamka maneno kama haya? "namkataa Issa Bin Maryam...ya kuwa si Mungu, wala Bwana wangu....." Mkristo anayejitambua hawezi, kwanza hata ulimi hautaweza kunyanyuka kutamka haya maneno. Lakini unaweza usibadilishe dini kila mtu akabaki na ya kwake, lakini Mkristo ameambiwa asifungwe nira na wasioamini. Wa kwako ni asiyeamini. Hata angekuwa Mkristo mwenzio kama haamini sawasawa hutakiwi kufungwa nae nira.

Mwisho nisema Muislam na Mkristo wanaweza kuoana na kuishi bila shida endapo watakuwa ni majina tu - yaani wanaenda msikitini na kanisani siku za sikukuu au wanaenda kila siku ila wanaabudu miungu yao kwa vinywa tu.
 
Mmmh jaman dini ni kikwazo kikubwa nyie hamjui tu
 
Back
Top Bottom