FIRST
1. Kakucheat mpaka kapata mtoto
2. Anakataa wakati ni kweli( Wazazi wako sio wajinga maana hawana sababu ya kuongopa)
Kubwa kuliko yote ni kukutishia kukuacha, yani hili ndio baya na ndio ambalo unatakiwa kuliangalia zaidi kuliko hata Swala la kutokuwa muwazi.
Jamaa hakupendi, anakuchukulia poa maana angekuwa na busara na upendo asingekutishia kukuacha wakati yeye ndio mkosaji. Hapo hamna mume dada yangu
SECOND
1. Umewadharau wazazi wako na kutowaamini
2. Mtu anakutushia kukuacha halafu na wewe unajaa upepo unapanic
Kawaombe msamaha wazazi wako kwa ulichowafanyia, wanakupenda mpaka wakakusaidia kufanya uchunguzi ambao wewe ulitakiwa ufanye au utambue sababu ni mtu wako.
Mwisho kabisa acha Kuwa kama kipofu, Kupenda gani huko ambako unaona red flag waziwazi halafu unang'ang'ania tu kuendelea na mahusiano kisa kakuahidi ndoa!! Ndoa haina maana kama unaolewa na mtu ambaye hajali hisia zako kiasi cha kukutishia kukuacha kwa kosa lake mwenyewe. Atakuendesha sana huyo
MWISHO
Mimi nina mtoto nje ya mahusiano yangu Lakini huyo jamaa yako sikushauri aisee sababu hana busara,ishu sio mtoto bali ni jinsi gani kama mwanaume anayekupenda ambavyo anatakiwa kulishughulikia hilo swala.be careful.
Kazi Kwako
I am out