Habari wanajamvi,
Niliimuuliza mwenzangu ambae aliruka akakasirika na kutishia kuniacha...nilimbembeleza kumwambia kama sio kweli basi tuendelee. Yakapita tukaendelea.Hivi karibuni nimepata tena simu kutoka kwa mtu wetu wa karibu aliyeniambia jambo hilo hilo tena na details za kutosha kumhusu mpenzi wangu.
Nimekosa furaha sana na sina amani.Natamani nichunguze ili nijiridhishe ile sijui pakuanzia. Msimamo wangu ni kutoingia katika ndoa na mtu aliyezaa tayari bora angeniambia mapema, nijue moja natamani nijue kwanini alinificha kwa miaka zaidi ya minne.
Naombeni busara zenu juu ya hili
Asanteni
Kwanza hongera kwa kulelewa vyema na wazazi wako,wanakupenda sana na wanakujali sijui wewe ndo mtoto wa pekee katika hiyo familia...
Inaelekea pamoja na miaka yote minne ya Uchumba wenu either hamjuani vyema au humjui vyema mwenzako.
Anyway,binadamu anaweza kukosea na kujirekebisha katika makosa yake,ila kama wewe ni mkristo ndoa ukiikosea ni msalaba wa kufika nao Golgota huo.Kwanza niseme wajibu uliokuwa unatakiwa kuufanya wewe wamefanya wazazi wako,washukuru sana kwa hilo narudia wapongeze kwa dhati.
Pili niseme,kuwa na mtoto kabla ya kuoa sio kosa,lakini hapa katika suala lako naona kuna kasoro flani ambazo ni bad alert kwako,zingatia.
Kwasababu ukweli umefahamika then unataarifiwa mtu analeta VITISHO,hakuna nia nzuri hapo kwasababu suala ilikuwa sio kukataa bali ni namna aliyotumia kukataa,ujue there are so many hidden of bad behaviour,ni kweli unaweza kukataa ili kushusha presha yako then aje aseme ukweli ibaki wewe kuuliza maswali yako,ila kwa yeye kutumia njia ya vitisho ujue haitaishia hapo.
Nafikiri hapa utapata majibu mengi,ila njia ya mwisho kaa na familia yako,hasa mama,shangazi,dada na kaka zako kama wapo watakupa ushauri mzuri sana.
Unatkiwa umjue mwenza wako wakati wa shida hasa migogoro na hasira anai-handle vipi...
In relationship kuna vitu vya msingi sana e.g God fearing person,communication,trustworthy,faithful na mtu anayewajibika na kujali familia..je hayo anayo?
Mwsho uamuzi ni wako ila kwa ushauri wangu BIG "NO"