Natamani kuchana vyeti!

Natamani kuchana vyeti!

Kazi utapata tu ipo siku amini ilo. Tuma maombi na Cv kila mahali usiangalie NGOs tu. Jaribu kuingia kwenye webste za mabenki mbalmbali na micro finances kama pride na Finca hutakosa. Kwa ninavyojua Pride ina watu wa SUA na sociologists wengi . All the best
 
Kazi utapata tu ipo siku amini ilo. Tuma maombi na Cv kila mahali usiangalie NGOs tu. Jaribu kuingia kwenye webste za mabenki mbalmbali na micro finances kama pride na Finca hutakosa. Kwa ninavyojua Pride ina watu wa SUA na sociologists wengi . All the best
Ahsante ndugu!
 
Jamani mwenzenu tangu nimegraduate 2011, B.A Community Development, tena nina GPA nzuri tu, na ni mtu wa kujituma, lakini sijawahi pata ajira mahali popote, NGOs ni nyingi lakini sijawahi hata kuitwa kwa interview katika NGOs zote nilizoomba. Japo naendelea kupambana na maisha ktk nyanja za kilimo na ufugaji lakini duuuh nikiwaona wenzangu wapo makazini (tena wengine nilikua nikiwabeba kwenye group assignments) napata shida nafsini mwangu to the extent that natamani kuchana vyeti vyangu vyoote nikae kama vile sikuwahi kwenda shule kabiiisaaaa!
Kuna wakati nilitembea maofisini katika ofisi ambazo nafahamu fika wanafanya shughuli zinazohusiana na maendeleo ya jamii nikiomba kujitolea buuureeee kabisa, nauli yangu, lunch yangu, wao wanipe kazi tu niwe nazifanya, tena nitazifanya kwa moyo, lakini sikupata hata pahala pamoja! nina mapenzi makubwa sana na profession yangu lakini sasa navunjika moyo, najiuliza nini kinasababisha nisikubaliwe hata pale ninapokua tayari kufanya kazi bure (Volunteering), nimefunga na kuomba kwa kila hali, sasa nimebaki kuhangaika na nafsi tu, nawaza kuchana vyeti vyangu vyote, na mabaki niyachome moto, iwe habari yangu ya shule imeishia hapo!
acha ujinga! inawezekana akiri yako ni ndogo ila hujijui bado! mpaka umefikia kuwaza kuwa uchane vyeti????kwani lazima upewe kazi? acha mambo yako ya kitoto! unaweza ukachana ukiamua lakini alafu suburi uone baraha lake!
 
Kuwa na cheti/vyeti ndiyo msingi - Keep themy. Ila tusisahau kuwatumia credible referees? Usije ukawa uliwatukana "wakunga" huko chuo.....
 
hicho kitu mbina rahisi sana chakufanya chukuwa vivuli vya vyeti vyako , barua ya kuombea kazi , na cv yako weka kwenye bahasha alafu vifanyie maombi ya wiki nzima alafu peleka sasa kuombea kazi uone kama utakosa tena.
 
Jamani mwenzenu tangu nimegraduate 2011, B.A Community Development, tena nina GPA nzuri tu, na ni mtu wa kujituma, lakini sijawahi pata ajira mahali popote, NGOs ni nyingi lakini sijawahi hata kuitwa kwa interview katika NGOs zote nilizoomba. Japo naendelea kupambana na maisha ktk nyanja za kilimo na ufugaji lakini duuuh nikiwaona wenzangu wapo makazini (tena wengine nilikua nikiwabeba kwenye group assignments) napata shida nafsini mwangu to the extent that natamani kuchana vyeti vyangu vyoote nikae kama vile sikuwahi kwenda shule kabiiisaaaa!
Kuna wakati nilitembea maofisini katika ofisi ambazo nafahamu fika wanafanya shughuli zinazohusiana na maendeleo ya jamii nikiomba kujitolea buuureeee kabisa, nauli yangu, lunch yangu, wao wanipe kazi tu niwe nazifanya, tena nitazifanya kwa moyo, lakini sikupata hata pahala pamoja! nina mapenzi makubwa sana na profession yangu lakini sasa navunjika moyo, najiuliza nini kinasababisha nisikubaliwe hata pale ninapokua tayari kufanya kazi bure (Volunteering), nimefunga na kuomba kwa kila hali, sasa nimebaki kuhangaika na nafsi tu, nawaza kuchana vyeti vyangu vyote, na mabaki niyachome moto, iwe habari yangu ya shule imeishia hapo!
Ukiachana na hiyo issue ya ku-develop community, ni field gani zingine upo competent kuifanya? Funguka,u never know mkuu.
 
Jamani mwenzenu tangu nimegraduate 2011, B.A Community Development, tena nina GPA nzuri tu, na ni mtu wa kujituma, lakini sijawahi pata ajira mahali popote, NGOs ni nyingi lakini sijawahi hata kuitwa kwa interview katika NGOs zote nilizoomba. Japo naendelea kupambana na maisha ktk nyanja za kilimo na ufugaji lakini duuuh nikiwaona wenzangu wapo makazini (tena wengine nilikua nikiwabeba kwenye group assignments) napata shida nafsini mwangu to the extent that natamani kuchana vyeti vyangu vyoote nikae kama vile sikuwahi kwenda shule kabiiisaaaa!
Kuna wakati nilitembea maofisini katika ofisi ambazo nafahamu fika wanafanya shughuli zinazohusiana na maendeleo ya jamii nikiomba kujitolea buuureeee kabisa, nauli yangu, lunch yangu, wao wanipe kazi tu niwe nazifanya, tena nitazifanya kwa moyo, lakini sikupata hata pahala pamoja! nina mapenzi makubwa sana na profession yangu lakini sasa navunjika moyo, najiuliza nini kinasababisha nisikubaliwe hata pale ninapokua tayari kufanya kazi bure (Volunteering), nimefunga na kuomba kwa kila hali, sasa nimebaki kuhangaika na nafsi tu, nawaza kuchana vyeti vyangu vyote, na mabaki niyachome moto, iwe habari yangu ya shule imeishia hapo!
Pole sana kijana. Wakati mwingine network ni muhimu sana. Nilikutwa na hali kama hiyo 1997/8 baada ya kumaliza Chuo. Uzuri mimi sikuwa na fikra za kuajiriwa kabisa. Nilirudi Bush(Morogoro), nikawa napiga issue binafsi za kununua na kuuza mazao na mbao. Maisha yalikuwa mazuri mpaka mwishoni mwa 1998 wakati mzigo wangu wa mbao ulipoibiwa na pia zingine kuchukuliwa na mvua za El-Nino.
Nikawa frustrated kidogo, ila kwa sababu nilikuwa na kaakiba ka kama 900,000/= hivi nikirudi dar kujaribu kutafuta ajira. Nilitafuta kwa zaidi ya miezi tisa bila mafanikio mpaka hiyo akiba yangu ikawa inaangukia kwenye upande wa NEGATIVE FIGURE. Ikanibidi nijibanze kwa fundi viatu(Jina kapuni), nikawa napiga dai waka la kupiga kiwi viatu kama watu wengine wasio na elimu. Ajira yangu ya kwanza niliipatia hapo.
Huyu mshikaji alikuwa na ndugu yake jeshini, akamwambia kuna ajira somewhere ila ni lazima uwe graduate. Pale kijiweni hakukuwa na graduate yeyote zaidi yangu. Nikampelekea bro wake vyeti vyangu, akavikagua na kuniunganisha wa wahusika. Nikala ajira. NAomba kukiri kuwa namuheshimu yule fundi na watu wengine wa madaraja ya chini mpaka leo.
Bila ya kuwa pale kwa yule fundi viatu aliyekuwa na NETWORK sijui mpaka leo hii ningekuwa wapi.
SALI na jenga Mtandao, unaweza kubahatika. INSHAALLAH
 
Nenda Ustawi wa Jamii wanatafuta watu wa kujitolea, kwanini unatafuta kujitolea kwenye ma NGO?
 
You can count years my dear, wadogo zangu wanaanza vyuo wanamaliza, wanapata kazi mimi nipo nawaangalia tu! I really, feel bad to the extent I don't want to set my eyes on my certificates anymore! Over a long period now I am thirsty of tearing my certificates into smallest pieces and I must make sure they remain only ashes!
Duhhhhhhhhhhhhhhhhhh, Pole.
Hama apo ulipo, kwani hata mitume baada ya kuona mambo hayaendi pale walipo, walihama. Inaonekana riziki yako haipo hapo.HAMA
 
Mbna UN wana program ya ku volunteer tena zengine ukibahatika unalipwa kabisa, jaribu huko acha kukata tamaa
 
Jamani mwenzenu tangu nimegraduate 2011, B.A Community Development, tena nina GPA nzuri tu, na ni mtu wa kujituma, lakini sijawahi pata ajira mahali popote.... nimefunga na kuomba kwa kila hali, sasa nimebaki kuhangaika na nafsi tu, nawaza kuchana vyeti vyangu vyote, na mabaki niyachome moto, iwe habari yangu ya shule imeishia hapo!
Ndugu,
Kwanza lazima ujue kuwa maisha ya mtaani ni shule tofauti. Elimu yako inaweza isiwe msaada sana wakati mwingine. Huo ni ukweli wa maisha. Lazima ufike sehemu ukubaliane na ukweli wa maisha na usonge mbele. Kwa mfano huwezi kufanya kazi tofauti na ulichosoma?

Lakini pia kuna swali lingine, una hakika mahali ulipoomba kujitolea wanahitaji mtu wa aina uliyowaaminisha uko? Inawezekana wana uhitaji lakini ni wa Karani na sio afisa.

Anyway siwezi kukushauri mengi kwa kuwa taarifa hazitoshi na umeandika kwa kukata tamaa.
Cha msingi tu ujue mapambano ya maisha ni mpaka unavuta pumzi ya mwisho ya uhai kisha unaingia katika maisha mengine ... raha au taabu!
 
Pole sana kijana. Wakati mwingine network ni muhimu sana. Nilikutwa na hali kama hiyo 1997/8 baada ya kumaliza Chuo. Uzuri mimi sikuwa na fikra za kuajiriwa kabisa. Nilirudi Bush(Morogoro), nikawa napiga issue binafsi za kununua na kuuza mazao na mbao. Maisha yalikuwa mazuri mpaka mwishoni mwa 1998 wakati mzigo wangu wa mbao ulipoibiwa na pia zingine kuchukuliwa na mvua za El-Nino.
Nikawa frustrated kidogo, ila kwa sababu nilikuwa na kaakiba ka kama 900,000/= hivi nikirudi dar kujaribu kutafuta ajira. Nilitafuta kwa zaidi ya miezi tisa bila mafanikio mpaka hiyo akiba yangu ikawa inaangukia kwenye upande wa NEGATIVE FIGURE. Ikanibidi nijibanze kwa fundi viatu(Jina kapuni), nikawa napiga dai waka la kupiga kiwi viatu kama watu wengine wasio na elimu. Ajira yangu ya kwanza niliipatia hapo.
Huyu mshikaji alikuwa na ndugu yake jeshini, akamwambia kuna ajira somewhere ila ni lazima uwe graduate. Pale kijiweni hakukuwa na graduate yeyote zaidi yangu. Nikampelekea bro wake vyeti vyangu, akavikagua na kuniunganisha wa wahusika. Nikala ajira. NAomba kukiri kuwa namuheshimu yule fundi na watu wengine wa madaraja ya chini mpaka leo.
Bila ya kuwa pale kwa yule fundi viatu aliyekuwa na NETWORK sijui mpaka leo hii ningekuwa wapi.
SALI na jenga Mtandao, unaweza kubahatika. INSHAALLAH
Ahsante mkuu, nimekuelewa sana
 
Kuna Bro wangu alisomea mambo ya Meli sasa alipotemwa kwenye Meli basi kazi zingine hataki anataka za huko huko tu huwa simuelewi kabisa... Dada yetu na wewe fanya kazi yeyote tu acha kuchagua uliyoisomea ndio maisha ya kibongo bongo yalivyo
 
Usikate tamaa huenda mwaka huu wa 2016 Ikawa mwisho wa kutoajiriwa na ndivyo itakavyokuwa, Hali hiyo uliyonayo imewahi kutupata hata sisi wengine lakini takribani miaka Kama yako baada ya kuhitimu shule tulipata ajira na kuna watu walitutia Moyo Kama tunavyofanya kwako kwamba hata ipite miaka Sita mpaka kwa Saba utapata kazi ya kuajiriwa tena Serikalini.
 
Fungua NGO yako, utafanikiwa na ndio utakuwa Mwanzo wakujiajiri na kuajiri wengine wenye kozi kama yako. Tatizo mnasoma kozi kwa kufuata mkumbo. Siku hizi mtu akikaribia kustaafu anamuandaa mtu wa kushika nafasi ile na wewe ukiiga inakula kwako.
 
Amina! Na ikawe hivyo mbele za Mungu ninaemwabudu!
Usikate tamaa huenda mwaka huu wa 2016 Ikawa mwisho wa kutoajiriwa na ndivyo itakavyokuwa, Hali hiyo uliyonayo imewahi kutupata hata sisi wengine lakini takribani miaka Kama yako baada ya kuhitimu shule tulipata ajira na kuna watu walitutia Moyo Kama tunavyofanya kwako kwamba hata ipite miaka Sita mpaka kwa Saba utapata kazi ya kuajiriwa tena Serikalini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom