Uchaguzi 2020 Natamani katika haya majimbo 11 ya Ubunge uchaguzi uwe Huru na wa Haki ili nipime nguvu ya upinzani Tanzania!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,965
141,970
Ni majimbo yafuatayo:

1. Kawe

2. Mikumi

3. Iringa mjini

4. Mbeya mjini

5. Tunduma

6. Hai

7. Karatu

8. Bunda

9. Tarime mjini

10. Tarime vijijini

11. Arusha mjini

Natamani kuona nguvu ya wapinzani katika maeneo haya "kiuhalali" kabisa kwa sababu majisifu yao yamezidi sasa.

Maendeleo hayana vyama!
 
Waulize watu wajikoni na duara la ndani kama uko nao karibu watakupa hali halisi! Ni surprise ya aina yake
 
Kwahiyo umeshajua uchaguzi sio huru na haki kwa ujumla wake, ila unataka majimbo hayo tu ndio uwe huru na haki. Kwa taarifa yako uchaguzi huu ukiwa huru na haki, hakuna uwezekano wa Cdm au ccm kushinda kwa zaidi ya 55%@. Na ikitokea hivyo ujue uchaguzi ujao ndio mwisho wa ccm. Ccm sio chama cha kizazi hiki, bali vyombo vya dola tu ndio vinaibeba.
 
Kwa nini hayo tu?

Tunataka uchaguzi wote uwe huru na haki mtu arejee Chatto kuchunga ng'ombe na farasi wake.
 
Kule Tarime vijijini CCM imebanwa mbavu mpaka imelazimika kuomba msaada tume na polisi angalau wawabambikie kesi watu walioko kwenye ngome ya Heche...Mwita Waiatara katulizwa vibaya
 
Kwa kweli mkuu majimbo mawili tu ambayo yataenda CCM lkn mengine cjui hali ni tete vijana wanataka mabadiliko mifuko yao haina kitu wamebaki ombaomba ndani ya nchi yao

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Kwahiyo umeshajua uchaguzi sio huru na haki kwa ujumla wake, ila unataka majimbo hayo tu ndio uwe huru na haki. Kwa taarifa yako uchaguzi huu ukiwa huru na haki, hakuna uwezekano wa Cdm au ccm kushinda kwa zaidi ya 55%@. Na ikitokea hivyo ujue uchaguzi ujao ndio mwisho wa ccm. Ccm sio chama cha kizazi hiki, bali vyombo vya dola tu ndio vinaibeba.
Kwa mujibu wa mbunge mstaafu wa CHADEMA mh Lijualikali ni kwamba wabunge wa CHADEMA huwa wanashinda kwa mbinu za gizani.
 
Hahaha Johniiii eti mijisifu imezidi sasa
Uchaguzi huu ni bumper to bumper, mkijifanya mnapindua matokeo kitawaka tu
 
Back
Top Bottom