Nataka Rais Magufuli ashindwe

Nataka Rais Magufuli ashindwe

Status
Not open for further replies.
JINA: TUJISAHIHISHE

MWANDISHI: J.K.Nyerere

MWAKA: 962.

Hiki ni kijitabu alichokiandika Mwl Nyerere pindi alipouacha uwaziri mkuu na kuingia kwenye Uraisi-Jamhuri.

Katika kitabu hiki Mwalimu anajaribu kuelezea mambo kadhaa ambayo--kwa mtazamo wake--aliamini ni makosa na mapungufu mbalimbali yaliyojitokeza ndani ya TANU--kama si Tanganyika kwa ujumla-- ambayo anaisihi jamii iweze kuyasahihisha..(Kujisahihisha ni njia ya kujitafakari na kuamua kurekebisha unapoona hapako sawa).

Mwalimu anaanza kwanza kwa kuufananisha umoja wa binadamu ndani ya jamii na mfumo mzima wa viuongo vya mwili wa mwanadamu. Viuongo hivi ni lazima vitii kanuni za afya na mwili ili visidhuru utendaji wa mwili(jamii). Anasisitiza kiuongo kimoja kikipata hitilafu, inaweza zuia viungo vingine vyote visifanye kazi i.e jamii nzima ishindwe kutimiza malengo yake.


Makosa ya kusahihisha.

1. Unafsi(ubinafsi).
Hili ni jambo ambalo Mwalimu amelieza zaidi ya mara mbili katika kijitabu hiki. Mwalimu anasema kosa kubwa linalofanyika ndani ya jamii au TANU ni wanachama kuishi kibinafsi kwa kuamini kuwa TANU inapaswa kuwafanyia kazi wao na si jamii nzima. Mwalimu anasema watu wa namna hii malengo yao binafsi--na si ya jamii--- yasipotimia basi kwao chama ni kibaya.

2. Woga.

Mwalimu nasema kosa hili hutokana na kosa la kwanza(unafsi). Hii inapelekea katika jamii , watu kushindwa kukemea maovu. Mkubwa anashindwa kukemewa kosa kisa yeye ni mkubwa, na mdogo anaonewa hata kama hana kosa kisa yeye ni mdogo. Woga huu unapelekea watu kutanyamazia maovu na dhuluma zinazofanywa na watu fulani kwa jamii kwa kuhofia kupoteza vyeo vyetu au maslahi fulani--ubinafsi.


3. Fitina

Mwalimu anaielezea hii kwa kuimulika ahadi ya mwanaTANU kuwa, nitasema kweli daima, fitina kwangu ni mwiko. Mwalimu anasema uwepo wa fitina ndio unaopelekea mtu kutoambiwa ukweli wa dhahiri. Mtu anafanya kosa lakini haambiwi pale hadharani, badala yake watu wanaenda msengenya pembeni. Fitina pia mwalimu anaioanisha na watu kumuonea mtu mmoja aliyefanya kosa dogo kulikuza kosa lake na kuonekana kubwa kama mlima kilimanjaro, na kosa lingine kubwa la mtu mwingine linaonekana kama si kosa.

Mwalimu anaeleza watu wafitini msingi wa 'Ukweli' kwao si msingi wa ukweli wenyewe bali ni mtu...

Fitina inapelekea , wakati mtu mwingine ni kweli kabisa amekosa lakini hakoselewi kwa sababu ya kosa lake, bali hoja zinazotumika kukosoa ni za unafsi.


4. Uchaguzi wa viongozi.

Mwalimu anasema kosa jingine ni kuchagua viongozi kwa msingi wa unafsi. badala ya kuchagua kiongozi kwa misingi ya TANU ,anachaguliwa kwa misingi ya ubinasfsi. Mwalimu anasema hii ni kuua chama.


5.Kutokujielimisha.

Moja ya ahadi ya mwanatanu ni kujielimisha. Mwalimu anasema ni lazima mwanatanu au mwanadamu azidi kujielimisha kila siki, na kujielimisha si tu kwenda darasani. Bali kuutafuta ukweli.

Mwalimu anasema ni kosa na dhambi kubwa kwa mtu kuamini kuwa anajua kila kitu na haitaji tena kujielimisha


6. Kujitweza sababu ya elimu.

Mwalimu anasema lengo la Elimu ni kuitumia elimu yako kwa manufaa ya jamii nzima na si kuwa na elimu na kisha elimu hiyo ikuwekeee mipaka na watu wengi na kuanza kubagua na kudharau watu sababu hawana elimu.


7. Ubaguzi wa kivyama

Mwalimu anasema ipo dhana katika wanaTANU kujiita 'Wao wanaTANU na wale sio wanaTANU.

Hii mwalimu anaieleza watu wasio wanatanu wanachukuliwa kuwa si wananchi na raia bora. Hata wataumishi wa umma hata wawe bora kiasi gani, kama si wanatanu wanaonekana si lolote


8. Ubinafsi wa mawazo

Mwalimu anasema lipo kosa baya linalojengeka katika jamii kuwa wapo watu mawazo yao wanayaona ndio mawazo ya jamii. Likipingwa jambo lao wanachukulia limepingwa jambo la jamii nzima na kujitafutia uhalali kwa jamii, jambo lao linapopingwa eti, ni la jamii nzima.


9. Kuheshimu mawazo

Mwalimu anasema katika jamii kunankuwa na mawazo ya wengi na ya wachache. Katika mjadala ni lazima wachache wapewe nafasi ya kusikilizwa na kuheshimiwa mawazo yao. Lakini hii haimaanishi kuwa ni lazima watakubaliana na mawazo ya wengi. Hata baada ya maamuzi na wachache kukubaliana na mawazo ya wengi, bado demokrasia inawaruhusu kuendelea na imani yao juu ya suala wanaloliamini.


10. Kusingizia mambo juu ya matatizo yetu.

Mwalimu anasema kutokana na kutotumia akili sawa sawa, mwanadamu anatafuta majawabu mepesi kwa mambo magumi. Kukimbilia kusingizia ukoloni au wazungu juu ya matatizo ya watanganyika ni kukwepa ukweli na kutotafuta njia sahihi za kutatua matatizo. Pia mwanadamu anakimbilia kupiga ramli kwa mganga badala ya kutafuta suluhu halisi ya matatizo


HITIMISHO

Mwalimu anahitimisha kwa kusema kuwa kufanya kosa ni kawaida kwa mwanadamu lakini busara ni kujisahihisha na kuepuka makosa. Anatoa mfano, kipofu akikunyaga ni ubinadamu kumpiga kofi, lakini si busara kujitoboa macho ili na wewe umkanyage.
Pia anasema ni ubinafsi kutaja makosa ya watu na kujifanya wewe huna makosa au kuficha makosa. Hata yeye mwalimu anasema anaweza kuwa nayo makosa, bali muhimu ni kutumka akili zetu wanadamu kwa huru bila kutu(makosa hayo) ili kutimiza lengo letu binafsi na ya jamii nzima.

Kwa lengo la kujihukumu wenyewe ( ambalo ni jambo gumu na busara--asilolipenda mwanadamu) na si kwa lengo la kuwahukumu wengine ( ambalo ni jambo rahisi--na alipendalo mwanadamu), mwalimu ameyataja makosa hayo ya WanaTANU ili TUJISAHIHISHE.


*************Mwisho*****************
 
Hivi mtu akisema Dangote anahamia Kenya wakati hahamii kuna tatizo gani? Huoni watu waliosema Dangote anahamia Kenya ndio waliomuibua JPM na Dangote baada ya sisi kuchoshwa na mawaziri wetu ambao walikuwa na lugha gongana kwa suala hilo hilo moja?

Majukwaa kama haya ni majukwaa ambayo huweza kuandika lolote ikiwemo tetesi, hivyo serikali inapaswa kuiangalia JF kama mahali panapoweza kuwekwa tetesi, au maoni tu ya mtu yakajadiliwa, hivyo haipaswi kutunisha misuli dhidi ya tetesi na maoni yetu, maaana ni haki yetu kuwa na maoni hata yale yanayotofautiana na approach ya serikali katika mambo mbalimbali.

Jambo linalofanyika sasa ni la hatari na halipaswi kuungwa mkono hata kidogo. Na kwa kifupi haya huweza tu kufanywa na serikali isiyojiamini katika kile inachokisimamia. Wananchi sio wajinga kiasi cha kushindwa kuona utendaji wa serikali kwa kupofushwa na kinachoandikwa JF au mahali pengine. Kama serikali inafanya mazuri haina sababu ya kuweweseka. hata siku moja, serikali isitarajie itasifiwa tu, hilo halipo. Mtafungia JF, magazeti na redio lakini njia za mawasiliano ndio kwanza zinazidi kuibuliwa. Dunia ya sasa sio ya kukimbizana na maoni ya watu, bali ni dunia ya kutafakari na kufanyia kazi maoni hayo!
Haya endelea kuamini hivyo
 
DAH, mkuu umeongea POINT sana ,tatizo watu wanaendeshwa ka mihemko badala ya kuufikirisha ubongo na tafakuri za kina,kweli kuna haja ya uwepo wa uhuru wa maoni tena mpana na usio na mwisho lakini uhuru huo usiwe wa mtu kaamka na mindoto yake anakuja humu anatoa stori za ajabu ajabu za kutunga tunga kisha aachiwe tu,

hata huko kwa wenzetu uhuru hupo ila wanautumia kwa nji ipasavyo,mfano kuna mijitu hapa Jf lazima kila siku iweke uzi ambao hauna kichwa wa miguu mradi tu naye aonekane ameweka uzi,kwa kweli ukifikiria sana unaona sisi wenyewe ndio tunajikosea heshima na kuifanya serikali itafute nji ya kuminya uo uhuru,ikumbukwe haijakatazwa kukosoa,kaa kukosoa tukosoe sana tena bila aibu wala hiyana yeyote lakini katika kosoa hiyo tuzingatia ukweli,staha na madhara ya huo ukosoaji wake,

wakati mwingine unasoma uzi unajiuliza huyu ni mtanania kweliii au ni pandikizi la mataifa jirani? ndugu zanguni machafuko ya Misri,Tunisia Libya na nchi nyingin za kiarabu kwa kaisi kikubwa yalitokana na watu kulishana matango pori juu ya serikali zao na hiyo ilikuwa ni mikakati ya nnchi za ng'ambo kuziharibu nchi za kiarabu,atokeo yake watu wakaamini propaganda na kuamua kujiweka rehani kwa kitu ambacho hakina ukweli wowote ule,leo hii hata hawajielewi .

Leo hii walibya wanalia,wamisri wanalia,watunisia wanalia ,wamepoteza ndugu na jamaa zao kwa ujinga ,kwa kudanganywa na kuchonganishwa,

Kuhusu suala la mmiliki wa Jf kukamatwa na leo inasemekana atafikiswa mahakamani,nazani watanzania hapa hatuahitaji kuwa kama WEHU,tusio jua nini maana ya mahakama,maadamu imebainika kile kilichosababisha akakamatwa na kuzuiliwa ndani ,vema tukawa watulivu huku tukiacha mahakama kazi yake ,ndio tuanze kuja na hayo malalamiko yetu mara baada ya maamuzi kutoka kwani ukitazama sheria Mmiliki wa JF na polisi wote wako sawa katika madai yao.

Mwisho watanzania nchi hii ni yetu sote,hakuna mwenye kusema hii ni nchi yangu,kama umezaliwa tanzania mkono wako wa kulia unaalama ya ndui,ni wajibu wako kuilinda tanzania dhidi ya wanapropaganda wanaoishi kwa kueneza maneno ya ajabu ajabu juu ya Tanzania,maneno ambayo hayana hata tone la ukweli.

Tukikubali hali hii mwisho wa siku tutajikuta tunalia na kujutia,mifano ya misri,libya na tunusia sio ya kubeza,tunachotakiwa kuzingatia hapa tusikubali yaliyotokea huko yanatokea hata hapa kwetu,japo kweli kuna baadhi ya maeneo ambapo serikali haijafanya vema lakini subra na utulivu ulio na uvumilivu vibaki kuwa mioyoni mwetu, wenzetu wa Ghana walivumilia mwisho akafanya maamuzi ya kistarabu na maisha yanaendelea,so na sisi hatuna budi kufanya hivyo kama tu tumewachoka watawala hawa tulio nao.

Nimekuelewa sana tatizo mihemko ya kisiasa imetawala sana vichwa vya watu
 
Rais ana nguvu nyingi sana ... Rejea kauli za Mwl JK Nyerere ....

Miezi michache iliyopita rais Magufuli alisema anatamani malaika ashuke [sijui ashuke toka wapi] aje kuizima mitandao ya kijamii ambayo tumekuwa tukiitumia kupashana habari na kubadilishana maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali.

Baadhi yetu tuliyachukulia maneno hayo kama ishara ya mambo yajayo kuhusu uminywaji wa hii mitandao na haki ya watu kuitumia kwa kujieleza, kutoa maoni, na kuikosoa serikali.

Sasa kitendo kilichotokea jana cha kukamatwa kwa Max kimethibitisha kuwa huu utawala wa Magufuli umeazimia kutuziba midomo kwa kutumia mabavu ya dola.

Kwa hilo mimi nataka huyo Magufuli ashindwe na alegee kabisa. Sitaki kabisa afanikiwe hata kidogo na watu wote wenye akili zao timamu hawana budi kumpinga na kuifanya hizo azma yake iwe muhali.

Kupinga udhalimu ni jambo la adhama. Na huyu mtu tayari keshaonyesha dalili zote za udikteta. Hivyo tumpinge kwa pumzi na nguvu zetu zote. Kwanza ni mtumishi wetu na si vinginevyo.

Hizi siyo zama za kupelekeshana kwa vitisho. Haogopwi mtu zama hizi.

Akichemka tutamkosoa tu. Akichapia Kiingereza tutamcheka tu. Kama hana ngozi nene ya kuweza kumudu na kuvumilia kuongelewa kwa namna yoyote ile basi aondoke. Aachie ngazi.

Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha.

Sikuwahi hata siku moja kudhani kuna mtu angekuja kumpiku JK kwenye ubomu lakini ndani ya mwaka tu huyu jamaa keshamuacha mbali mno JK. Pata picha hiyo miaka minne iliyobaki hali itakuwaje.

Huyu mtu tumdindie. Tukinywea atavimba kichwa na kujiona ana nguvu nyingi ilhali hana. Hana nguvu za kuweza kuzidi nguvu ya umma.

Kwa hiyo mimi nataka ashindwe. Tena ashindwe vibaya. Je wewe mdau wasemaje?
 
Miezi michache iliyopita rais Magufuli alisema anatamani malaika ashuke [sijui ashuke toka wapi] aje kuizima mitandao ya kijamii ambayo tumekuwa tukiitumia kupashana habari na kubadilishana maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali.

Baadhi yetu tuliyachukulia maneno hayo kama ishara ya mambo yajayo kuhusu uminywaji wa hii mitandao na haki ya watu kuitumia kwa kujieleza, kutoa maoni, na kuikosoa serikali.

Sasa kitendo kilichotokea jana cha kukamatwa kwa Max kimethibitisha kuwa huu utawala wa Magufuli umeazimia kutuziba midomo kwa kutumia mabavu ya dola.

Kwa hilo mimi nataka huyo Magufuli ashindwe na alegee kabisa. Sitaki kabisa afanikiwe hata kidogo na watu wote wenye akili zao timamu hawana budi kumpinga na kuifanya hizo azma yake iwe muhali.

Kupinga udhalimu ni jambo la adhama. Na huyu mtu tayari keshaonyesha dalili zote za udikteta. Hivyo tumpinge kwa pumzi na nguvu zetu zote. Kwanza ni mtumishi wetu na si vinginevyo.

Hizi siyo zama za kupelekeshana kwa vitisho. Haogopwi mtu zama hizi.

Akichemka tutamkosoa tu. Akichapia Kiingereza tutamcheka tu. Kama hana ngozi nene ya kuweza kumudu na kuvumilia kuongelewa kwa namna yoyote ile basi aondoke. Aachie ngazi.

Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha.

Sikuwahi hata siku moja kudhani kuna mtu angekuja kumpiku JK kwenye ubomu lakini ndani ya mwaka tu huyu jamaa keshamuacha mbali mno JK. Pata picha hiyo miaka minne iliyobaki hali itakuwaje.

Huyu mtu tumdindie. Tukinywea atavimba kichwa na kujiona ana nguvu nyingi ilhali hana. Hana nguvu za kuweza kuzidi nguvu ya umma.

Kwa hiyo mimi nataka ashindwe. Tena ashindwe vibaya. Je wewe mdau wasemaje?
Hiyo itakusaidia nini?
Unune, ucheke, hata uafanyeje huyo ndo rais wetu
Rais hafanyi kazi kwa kukupendelea wewe
Cha maana ni kufuta sheria na utaratibu
 
Miezi michache iliyopita rais Magufuli alisema anatamani malaika ashuke [sijui ashuke toka wapi] aje kuizima mitandao ya kijamii ambayo tumekuwa tukiitumia kupashana habari na kubadilishana maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali.

Baadhi yetu tuliyachukulia maneno hayo kama ishara ya mambo yajayo kuhusu uminywaji wa hii mitandao na haki ya watu kuitumia kwa kujieleza, kutoa maoni, na kuikosoa serikali.

Sasa kitendo kilichotokea jana cha kukamatwa kwa Max kimethibitisha kuwa huu utawala wa Magufuli umeazimia kutuziba midomo kwa kutumia mabavu ya dola.

Kwa hilo mimi nataka huyo Magufuli ashindwe na alegee kabisa. Sitaki kabisa afanikiwe hata kidogo na watu wote wenye akili zao timamu hawana budi kumpinga na kuifanya hizo azma yake iwe muhali.

Kupinga udhalimu ni jambo la adhama. Na huyu mtu tayari keshaonyesha dalili zote za udikteta. Hivyo tumpinge kwa pumzi na nguvu zetu zote. Kwanza ni mtumishi wetu na si vinginevyo.

Hizi siyo zama za kupelekeshana kwa vitisho. Haogopwi mtu zama hizi.

Akichemka tutamkosoa tu. Akichapia Kiingereza tutamcheka tu. Kama hana ngozi nene ya kuweza kumudu na kuvumilia kuongelewa kwa namna yoyote ile basi aondoke. Aachie ngazi.

Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha.

Sikuwahi hata siku moja kudhani kuna mtu angekuja kumpiku JK kwenye ubomu lakini ndani ya mwaka tu huyu jamaa keshamuacha mbali mno JK. Pata picha hiyo miaka minne iliyobaki hali itakuwaje.

Huyu mtu tumdindie. Tukinywea atavimba kichwa na kujiona ana nguvu nyingi ilhali hana. Hana nguvu za kuweza kuzidi nguvu ya umma.

Kwa hiyo mimi nataka ashindwe. Tena ashindwe vibaya. Je wewe mdau wasemaje?
Tulimpenda wenyewe. Tujipime sisi wenyewe kama upendo wetu bado upo kwake? kama haupo basi siku hazigandi kabisa tutunze machungu yetu na hasira zetu mpaka wakati utakapo wadia tujitokeze na kumpinga katika karatasi ya Kura. Hii ndiyo demokrasia wandugu.
 
Kwani mtu ukitoa maoni yako pasipo kutoa matusi au ukianzisha uzi wenye uhalisia na usio wa kichochezi unakuwa na hofu ya nini?

Tatizo lililopo kuna baadhi yetu tumekuwa maarufu kutunga stori za uongo na kuzijengea hoja then tunataka jamii iamini kama ni kweli kumbe ni upotoshaji

Mtu kama umeanzisha mada yako na ushahidi unao kwa nini uogope? Endapo utahitajika polisi si unapeleka ushahidi?

Fikiria mtu anayeanzisha uzi hapa eti Dangote anahamishia kiwanda Kenya na hizo habari zinasambaa dunia nzima kumbe ni uonge pasipo kufikiria negative impacts kwa wawekezeji walioko huko nje. Mtu kama huyu leo hawezi fanywa kitu sababu tu anatumia ID feki sishangai kesho akaibuka na jambo jingine

Watu wa namna hii lazima washughulikiwe hakuna kulea ujinga. Watanzania tumekuwa maarufu sana wa kupika majungu

Ninakubaliana na wewe kabisa uhuru wa kutoa maoni lazima uheshimiwe na watawala kwani ni takwa la kikatiba lakini uhuru huo lazima uzingatie utu na nidhamu.

Leo mtu akimchukia mtu flani sababu za kiitikadi za vyama au jambo lolote, kesho anamtungia tuhuma na kusambaza kwenye mitandao. Vitu vya namna hiyo siyo vya kulea
acha kubwabwaja kama kasuku, njia pekee ya kubishana kwa hoja ni kujibu hoja nothing else, hoja ikiwa dhaifu hapa jf inakua debunked tu so if there is nothing to hide there is nothing to fear about any post.
 
Jpm wewe sio Mungu na kumbuka kuna maisha baada ya kufa

Umewaza mbali.ila in viongozi wachache sana.wanaokumbuka hayo.wengi ulewa madaraka.angalia godwin gondwe.wakati anasoma taarifa ya habari itv.na sasa hivi alivyo.
 

Umewaza mbali.ila in viongozi wachache sana.wanaokumbuka hayo.wengi ulewa madaraka.angalia godwin gondwe.wakati anasoma taarifa ya habari itv.na sasa hivi alivyo.
tunapaswa tuwakumbushe maana nao ni binadamu km sisi pia isipokua Mmungu amewapa vyeo tu hivyo hawapaswi kujisahau na pia hakuna atakayedumu milele

Yuko firauni?Hitler ,nk Mwisho wa siku kila mja atarudi mavumbini
 
Hivi mna u hakika kuwa Rais ndiye kaagiza, kiongozi wetu hapa JF akamatwe?
====
Staha katika kumshauri rais ni muhimu.
Si wanasemaga mtu hasemi kisichokuwa mayoni. Malaika ni muujza. Watu wengine sijui wanatoka wapi. Mkiambiwa someni mnaleta phd fake . Haya sasa ndio matokeo yake.
 
Miezi michache iliyopita rais Magufuli alisema anatamani malaika ashuke [sijui ashuke toka wapi] aje kuizima mitandao ya kijamii ambayo tumekuwa tukiitumia kupashana habari na kubadilishana maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali.

Baadhi yetu tuliyachukulia maneno hayo kama ishara ya mambo yajayo kuhusu uminywaji wa hii mitandao na haki ya watu kuitumia kwa kujieleza, kutoa maoni, na kuikosoa serikali.

Sasa kitendo kilichotokea jana cha kukamatwa kwa Max kimethibitisha kuwa huu utawala wa Magufuli umeazimia kutuziba midomo kwa kutumia mabavu ya dola.

Kwa hilo mimi nataka huyo Magufuli ashindwe na alegee kabisa. Sitaki kabisa afanikiwe hata kidogo na watu wote wenye akili zao timamu hawana budi kumpinga na kuifanya hizo azma yake iwe muhali.

Kupinga udhalimu ni jambo la adhama. Na huyu mtu tayari keshaonyesha dalili zote za udikteta. Hivyo tumpinge kwa pumzi na nguvu zetu zote. Kwanza ni mtumishi wetu na si vinginevyo.

Hizi siyo zama za kupelekeshana kwa vitisho. Haogopwi mtu zama hizi.

Akichemka tutamkosoa tu. Akichapia Kiingereza tutamcheka tu. Kama hana ngozi nene ya kuweza kumudu na kuvumilia kuongelewa kwa namna yoyote ile basi aondoke. Aachie ngazi.

Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha.

Sikuwahi hata siku moja kudhani kuna mtu angekuja kumpiku JK kwenye ubomu lakini ndani ya mwaka tu huyu jamaa keshamuacha mbali mno JK. Pata picha hiyo miaka minne iliyobaki hali itakuwaje.

Huyu mtu tumdindie. Tukinywea atavimba kichwa na kujiona ana nguvu nyingi ilhali hana. Hana nguvu za kuweza kuzidi nguvu ya umma.

Kwa hiyo mimi nataka ashindwe. Tena ashindwe vibaya. Je wewe mdau wasemaje?
Maneno yako na yakapate kibali, kwa Mungu ili yatimie 2020, Ee Mungu baba tunakuomba ukatuinulie Edward Lowasa awe rais wetu wa Tanzania, tunaomba na kushukuru kwa Jina la Yesu...wote tuseme amen
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom