Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,932
- 30,045
Binti hakuna gari utakayotumia chini ya elfu kumi kwa siku !
Ngoja tuweke mambo sawa.
Mwenge - Posta ni kama 10km hivi. Ukifanya na kurudi inakua 20km. Na labda foleni + AC ni mafuta ya 5km, so kwa siku ni 25km bila misele mingine.
Vigari vinavyozungumzwa hapa vinaenda kuanzia 10km/lt - 15km/lt, so average au approximatee tufanye 13km/lt. Ndio kusema kwamba vitahitaji lita mbili kutoka Mwenge hadi Posta na kurudi.
Bei ya mafuta approximate ni Tshs 2,000/- kwa lita. So lita 2 ni kama Tshs 4,000/- kwa siku. Ndio kusema kua kwa yule wa siku tano za kazin atatumia Tshs 4,000 x 5= Tshs20,000 kwa wiki bila kuweka misele ya wikiend.
Hesabu hizi zimeweka assumptions mbalimbali kwamba kila siku unapita njia hiyohiyo tu. Pia Injini ya gari ipo kwenye same condition daily. Assumption ingine ni kwamba gari hii inakwenda 13km kwa lita, so kama inakula poa zaidi ya hapo, mafuta yanaweza kufika wikiend. Pia assumption ingine ni kua foleni + ac = 5km kwa siku, so kama vio viko chini ni faida zaidi.
Ukanyagaji wa kibati cha mafuta nao unachangia. Kama we unaendesha kama upo kwenye Formula one nalo ni tatizo pia.