View attachment 3414079
UNAJUA FAIDA YA KUWEKA KIKINGA MALKIA KWENYE MZINGA WAKO?
Wafugaji wengi wamekuwa wakifuga Nyuki kwa kutumia mizinga yenye chemba moja (Single Box) badala ya ile ya chemba mbili (Double Box) maarufu kwa jina la Mizinga ya Ghorofa au kwa jina la kitalaamu la #Langstroth. Ili kutumia Kikinga Malkia lazima mzinga wako uwe wa aina ya Langstroth au (Double Box) na Sanduku hizi kila moja inakazi zake ambapo Sanduku la chini huitwa Blood Chamber (Chemba ya Uzazi) na juu huitwa Super Chamber (Chemba ya Asali).
Kwa kawaida sanduku hizi mbili hutenganishwa kwa katikati kuwekwa Kifaa maalum ambacho kinajulikana kama Queen Excluder (Kikinga Malkia). Chemba ya chini ndiyo inayopaswa kuwa na malango wa nyuki kuingia na kutoka ili Malkia na Nyuki waingie kwanza kuanza kuishi/kufugwa. Wapo baadhi ambao hutumia mizinga yenye chemba mbili (Double Box) lakini huweka wavu wa madirisha ya nyumba.
Kutumia Wavu wa madirisha kama mbadala wa kikinga Malkia (Queen Excluder) kwa lengo la kupata Asali zaidi wakati wa uvunaji lakini wavu huo hausaidii sababu una matundu makubwa zaidi ya mm 4 yanayoruhusu Nyuki dume na Malkia kupita. Lakini Kikinga Malkia kimetengenezwa kwa kipimo ambacho ni size inayozuwia Malkia na madume kupita.
Ukitumia kikinga Malkia tunatarajia kupata faida nyingi ambazo ni;
• Asali ivunwayo katika supers Chamber (Chemba ya Juu) ambako Malkia hafiki huwa safi kutokana kutokuwepo kwa Malkia au mayia, watoto.
•Nyuki hueenea zaidi kwenye masega ya majana (watoto) kuliko masega ya asali hivyo hurahisisha kazi ya uondoaji wa nyuki kutoka kwenye masega ya asali kuwa rahisi na wa haraka.
•Husaidia uchunguzi wa magonjwa na kutambua uimara wa Malkia iwapo anaweza kufikia idadi ndogo ya fremu (viunzi) katika eneo dogo la koloni au laa.
•Masega ya Majana (Watoto) huwa meusi zaidi kutokana na shughuli za uleaji watoto, lakini masega ya chemba ya juu ya asali hutoa Nta Safi na nzuri yanapochakatwa.
•Hata Mfugaji anapochelewa kufuga Asali anaweza kuikuta kutokana na madume walao Asali haraka kuwa chemba ya chini.
Hizi ni sehemu tu ya faida ambazo nimekudokolea leo.