Nataka kuacha kazi .

Ki ukweli hawamu hii watu wengi wanakufa kwa msongo wa mawazo na ndiyo maana kuna ongezeko la misiba mingi sana kwa sababu ya waTz wanatikisika kinamna yake si mfanyabiashara,si mtumishi wa Mungu,si mtumishi wa umma wote wapo hoi.
 
Huu uzi pm zitakuwa nyingi sana ..wapenda miteremko tunawaona tu[emoji134]
Teh teh teh wangejua nimepigika hadi najichukia,naichukia hata kazi yangu
Laiti ningalijua nisingeajiriwa serikalin,nilikuwa private Kwa mwaka mmoja ,walipotangaza ajira kiherehere nikajitosa,kumbe naingia pori la miiba
Halafu plot zenyewe ni potential sema hamna wanunuzi,kimoja Cha makazi nilichojenga,kingine nilipanga kujenga mjengo wa kustaafia sema naona dream zi ebadilika na upepo,na Cha mwisho ni industrial plot hiki,nilipanga nipate mwekezaj tuingie partinership sema disko limeingia mmasai.
 
Una kipindi kigumu kama changu.
2016 September nilikopa 10 millions, million moja nikaitumia kwa family matters, million 6 nikapata viwanja 2 na 3 million nikafungua duka na likafa au nikaliua baada ya kuona linanitesa, yaani Mimi nikageuka kulihudumia badala ya kunihudumia .
Ila sasa nakopesheka ingawa si hela nyingi, nilipitia kipindi kigumu sana mpaka nilipanga chumba cha elfu 30 kwa mwezi hapa dar ilhali nina familia.
Sasa napumua Mungu kanifungulia mlango mwingine naishi kwa uhuru kiasi.
Pole, jipe moyo yatapita.
Ushauri:Mtafute dalali auze kiwanja chako kimoja kwa bei ya shiida kisha fungua biashara za contracts kama bodaboda, saloon za kiume n.k
Hapa namaanisha msimamizi utakubaliana naye akuletee fixed amount kila wiki au siku.
Awamu hii kuna biashara usithubutu kuzifanya kama hutoweza kusimamia mwenyewe 24 hrs.
 
Usiache hiyo kazi kama bado hakuna uhakika na unapo paangalia UTASAGA MENO
 
Hivi mtu unamaliza shule unaenda kuajiriwa na SERIKALI?

Hakuna majitu dhalimu na system dhalimu dunia hii kama kitu kinachoitwa SERIKALI!

Ni dude linaloendeshwa kwa matakwa ya wanasiasa!

It is a murder engine!
Acha tu,nilikuwa na ndoto nyingi nzuri tu
Saivi nimejikatia tamaa,hata ofisini kutwa nashinda nimejiinamia
 



CHOMA MOTO MELI WEWE
 
Kwani shida iko wapi unalipwa mshahara ambao huufanyii kazi effectively? Unafika ofcn unacheza gemu kwa komputa mwisho wa mwezi unaenda ATM kutoa mshiko, shida iko wapi?
Sijawah cheza game ofisin kamwe
Nina vyeti 2 ,kimoja Cha mfanyakazi bora,kingine Cha best performer katika fani yangu Kwa mwaka 2017/18
 
Ni vile nchi yetu maskini tu..mie mdogo wangu anasema anajuta hata kupeleka cv huko...ovyo sana...alafu watumishi wamekuwa wanyoooongeee..tena mwez huu qwngine mshahara umechelewa sana sana kutoka..shenzy kbs
Acha tu tumekuwa wanyoonge hadi basi
Ila nahisi nilikuwa na ndoto kubwa sana na elimu yangu,tatizo kuzishusha ziwe average nashindwa
 
Kama unaweza kuwaza kufanya nite business kwanini usiwaze kudanga mchana na wanaume za watu?,maana km moyo wa kimalaya unao kabisa ni ujasiri kidogo tu unahitajika.

Ukiuza hivo vitu na kuacha kazi ndo inasaidia Nini???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…