Nataka kuacha kazi .

Nataka kuacha kazi .

Unasomesha watoto shule za gharama mno kulingana na Hali ya maisha yako.
Jitahidi wapeleke watoto shule za kawaida kulingana na kipato chako.
Kwenye hiyo 220k,toa 100k Kila mwezi ya ada za watoto,inabaki,120k,hujanunua chakula,maji na matumizi mengineyo ya nyumbani,hapo hakuna hata nguo mpya kumbuka

Jamaa nilishamtoa akilini manake nilimsihi Sana anisaidie,akawa anasema atatuma ila akawa hatoi,so nikaacha kumwomba
Hali ni ngumu sana,bado Kodi ya nyumba,inakatisha tamaa kwakwel
 
Hebu hao watoto wapeleke kwa baba yao kwanza. Umaskini jeuri hauna mwisho mzuri. Unapowang'ang'ania eti unamwogopa mwanamke mwenzio ulishawahi kuwaza unaweza kudedi wakati wowote na hao watoto wakalelewa na huyuhuyo mama wa kambo??
Kwanini wanawake hamuaminiani namna hii? Kwanini hampendani?
Pole kwa wanayokusibu ila nakushauri usiache kazi kabla hujapata mbadala wa kukuingizia kipato.
BTW hujapata buzi la kukupunguza nyege? Nyege zikizidi huleta hasira na mawazo ya kijinga kabisa. Ndo maana unawaza hata kujiua au kufanya biashara za usiku
Swali la kizushi: Nini kilifanya ndoa yako ivunjike?
Babu anaongea na mjukuu wake. 😂😂😂😂😂
 
Habari za asubuhi wana jukwaa.

Mie ni mtumishi wa umma na niliajiriwa mwaka 2013.Nina watoto wawili wa kiume,Nina viwanja vitatu ambapo kimoja nimejenga nyumba iliyoishia kwenye linta.

Toka aingie mkulu maisha yamekuwa magumu Sana,si furahii kazi yangu hata kidogo naenda tu kazini kuonekana nipo.Na siyo kuwa ni mpiga madili Wala,zamani tulikuwa tunapata hata viextra duty vinatuboost mwezi unaisha,ila saivi Nina mwaka wa tatu siijui posho.Tulikuwa tunaenda kazini hadi jmos angalau tupate chochote tulishe family.

Nimejaribu kuuza kiwanja kimoja at least nimalizie nyumba nihamie,manake Kodi inanitesa Sana huku nilikopanga ila nimekosa mteja.wanangu wanasoma mmoja baby class na mwingine class one.Bado mfanyakazi kumlipa hapo hujasaidia ndugu wanao ona nalipwa mamilioni ilihali mwisho wa mwezi napokea laki mbili na ishirini(220,000) ambayo haikidhi mahitaj yote.

Am a single parent kwahiyo mimi ndiyo baba na mama kwa wanangu.Baba yao tuliachana akaoa,na alitaka wachukua watoto ila sikuwa tayari kuacha wanangu wa under 7 years walelewe na mama wa kambo,hivyo kawasusa hatoi hata Senti tano kwaajili yao,so am their only hope.

Naona napoteza muda,nimeshafikiria hata kujirusha ghorofan ili nitoweke duniani ila nikiwafikiria wanangu roho inauma naona sitawatendea haki.So nimewaza nikaona si bora niache kazi,niuze Kila nilichonacho ingawa wateja wanakuwa tabu,nihame mji,nende sehemu nyingine nikaanze upya.Nimewaza pia kufanya nite business at least watoto wale na nipate Kodi ya nyumba,sema dhamira inakataa.

Mkuu hata Kama tulikuudhi tusamehe,tunadhalilika na familia zinateseka.Binafsi sioni faida ya kuitwa mtumishi wa umma ilhali Kuna wakati nakosa hadi nauli ya daladala kwenda kazini.Pia toka nimeajiriwa sijawahi panda cheo.

Naombeni ushauri wadau nifanyeje?je niache kazi?then niende wapi ama nifanye Nini baada ya kuacha kazi,Ningekuwa Sina watoto ningeshaondoka kitambo,tatizo mustakabali wa maisha ya wanangu utakuwaje,nikiwaza Hilo nachoka,naishia kumwaga machozi kama mtoto.
rusha picha yako tukuone,, utajiri umeukalia
 
Nitafute nikushauri
.Mini ni mhanga Kama wewe.Najua ulikopa Bank ukitegemea kurenew mikopo na ulitegemea mishahara kupanda.Nicheki 0787938347
No kabla bodi hawajaanza nikata nilikuwa napokea kiasi kinachokidhi matumizi ya nyumbani,walipoanza kunikata ndipo tatizo lilianza,manake nililetewa Deni la tshs mil 18 Kwa miaka 4 niliyokuwa chuo kwani nilipata mkopo 100%.
 
Mamii...nakuelewa sana...tena mno..hivi mm hapa niko kwenye mchakato wa kumshauri Mr ateme kazi ..mmepishana kidogo sana...yaan mm alifika kipindi akawa anakopa CRDB ile akipata mshahara wanafyeka chao then anakopa tena ya mwezi...🤗🤗🤗

Acha woga...hapo shoga utapiga marktime za kufa mtu..hebu ufuate ushauri wa@Khan..!tena bora ww..kamaliza Msc 2012 ila mpk leo hajaanza kulipwa..alafu alivyo ccm damu..ahhaa may mosi akaniambia dogo mie nahamia ACT😂😂..niongoze sala ya toba..jaman maisha ya wafanyakazi wa serikalin ni magumu mno mno nyie jaman...Kama unaweza njoo machimboni tupige hela😍😍😍!nw mtumishi wa serikali ukimtumia laki 1 Anakushukuru Mwezi mzima😂😂💎💎💎💍🔥🔥🔥!
Kuna mikoa mingne nuksi tu kuishi..hela inapatikana kwa mbinde sana . hama huko njoo geita my dear jipe 8mths..tutakuita boss mama😍😍 (weka hela pata mapesa)

na kama utahitaj kushikwa mikono nipo hapa..pole!
 
Hebu hao watoto wapeleke kwa baba yao kwanza. Umaskini jeuri hauna mwisho mzuri. Unapowang'ang'ania eti unamwogopa mwanamke mwenzio ulishawahi kuwaza unaweza kudedi wakati wowote na hao watoto wakalelewa na huyuhuyo mama wa kambo??

Kwanini wanawake hamuaminiani namna hii? Kwanini hampendani?

Pole kwa wanayokusibu ila nakushauri usiache kazi kabla hujapata mbadala wa kukuingizia kipato.

BTW hujapata buzi la kukupunguza nyege? Nyege zikizidi huleta hasira na mawazo ya kijinga kabisa. Ndo maana unawaza hata kujiua au kufanya biashara za usiku

Swali la kizushi: Nini kilifanya ndoa yako ivunjike?
Anaye wanae naye so hawawezi pata huduma Kama wazipatazo kwangu,isitoshe kama hakuwahi wahudumia chochote wakati tukiwa pamoja tena wakiwa wawil tu wadhan saivi ndio atawahudumia na ilhal anao wengine huko kwenye ndoa yake?
Na kuna sababu gani ya msingi wanangu walelewe na mtu baki ilhal mie nipo?
 
Pole sana! Unaishi wapi? Kiwanja unauza bei gani?

Usiache kazi! Anza na kubadili life style kwa muda wa mpito. Kwanza wapeleke watoto shule za kawaida (Kayumba).

Kuhusu kuhamia kwako unaweza kuhamia kwa gharama isiyozidi laki 3. Kwa kufanya yafuatayo. Uweke tofali kozi mbili mbele ya chumba kimoja ktk hyo nyumba yako. Halafu uwezeke kwa milunda, ambapo mlunda mmoja nielfu 3 . Chumba kimoja hutotumia zaidi ya milunda kumi na bati kama 6.
Kama utakuwa interested nitafute leo tushauriane namna rahisi ya kuhamia kwako.

Tambua hayo ni mapito tu. Kama wataka kuuza kiwanja uuza kimoja tu. Ila ningekuwa mimi kwa mshahara huo na watoto hao Nisingeuza. SIKUSHAURI UUZE KIWANJA. TAMBUA BADO UPO KTK STATUS NZURI.

Usiangalie ulipotoka, angalia inapokwenda.
 
Vipi ukihamia hata chumba kimoja karibu na kazini ukapunguza matumizi ya nauli na nguo ukawa unanunua hata kila baada ya miezi 3 bila kujali watu watasemaje maana ofisi zetu tunazijua ?

Kumbuka wewe ndio unajua uko katika hali gani, usilazimishe kujionesha kwa public mambo mazuri wakati unaumia maana utaharibikiwa zaidi.

Finally utakuja kugundua hakuna anaejali sana kuhusu unaishi vipi na hata kama yupo anaweza kuwa ana matatizo makubwa kuliko wewe.
Nina watoto wawili,mie mwenyewe na mfanyakazi wa ndani,kweli tuishi chumba kimoja?
Nguo sikuhiz nanunua za watoto tu,mie Nina mwaka siijui nguo mpya
 
Pole sana Mtumishi wa Umma
Siku zote kazi huachwa pale mbadala wake unapokuwa ushapatikana.
Ukisema uache kazi ufanye biashara pia utakumbana na changamoto ambazo kuna wakati utakitamani kile kidogo ulichokuwa wakipata.
Nafikiri cha kufanya:-
wahamishe watoto, wapeleke shule yenye gharama ambayo haitakuumiza kulingana na kile unachokipata.

Kama nyumba uliyopanga ni gharama ya kubwa jaribu kupunguza ukali wa maisha kwa kuhamia nyumba yenye gharama nafuu.
Yote haya utayafanya ukiwa watafuta mustakabali wa plan B ili kukupunguzia msongo wa mawazo.

Usikope pesa taasisi yoyote inayokopesha kwa dhamana uliyonayo (kiwanja/viwanja) kwasasa ili kumudu mahitaji ya ada, kodi + chakula.

Baada ya kufanya yote haya, jaribu kuangalia ni biashara ipi (ndogo, isiyohitaji mtaji mkubwa) na inayofaa mazingira uliyopo na unayoweza kuifanya ukiwa waendelea na kazi ya kuajiriwa.

Naelewa muda wako wa kufanya mambo mengine hautoshi kwa kuwa muda mwingi wautumia ofisini, kama kuna ndg.wa karibu atakayeweza kuisimamia biashara hiyo jaribu kufanya hivyo. ( Kwa kuwa pesa ya kumlipa kijana wa kuisimamia itakuwa tatizo).
 
Usiache kazi mkuu wakati bado tunatafakari ya kufanya.
Nahisi nikiacha kazi nitapata msukumo wa kujua Cha kufanya
Kazini napoteza muda tu kiukwel
Nina mpango wa kufungua kampuni,nishaandaa Hadi momerandum,nahangaikia kuisajil tu
Then nijitose,huenda nikikosa hata hiyo 220k nitapata akil Zaid na hasira ya kufanya vizuri zaid
 
Anaye wanae naye so hawawezi pata huduma Kama wazipatazo kwangu,isitoshe kama hakuwahi wahudumia chochote wakati tukiwa pamoja tena wakiwa wawil tu wadhan saivi ndio atawahudumia na ilhal anao wengine huko kwenye ndoa yake?
Na kuna sababu gani ya msingi wanangu walelewe na mtu baki ilhal mie nipo?
I rest my case!
 
Anaye wanae naye so hawawezi pata huduma Kama wazipatazo kwangu,isitoshe kama hakuwahi wahudumia chochote wakati tukiwa pamoja tena wakiwa wawil tu wadhan saivi ndio atawahudumia na ilhal anao wengine huko kwenye ndoa yake?
Na kuna sababu gani ya msingi wanangu walelewe na mtu baki ilhal mie nipo?
Shangaa na ww
 
Pole sana! Unaishi wapi? Kiwanja unauza bei gani?

Usiache kazi! Anza na kubadili life style kwa muda wa mpito. Kwanza wapeleke watoto shule za kawaida (Kayumba).

Kuhusu kuhamia kwako unaweza kuhamia kwa gharama isiyozidi laki 3. Kwa kufanya yafuatayo. Uweke tofali kozi mbili mbele ya chumba kimoja ktk hyo nyumba yako. Halafu uwezeke kwa milunda, ambapo mlunda mmoja nielfu 3 . Chumba kimoja hutotumia zaidi ya milunda kumi na bati kama 6.
Kama utakuwa interested nitafute leo tushauriane namna rahisi ya kuhamia kwako.

Tambua hayo ni mapito tu. Kama wataka kuuza kiwanja uuza kimoja tu. Ila ningekuwa mimi kwa mshahara huo na watoto hao Nisingeuza. SIKUSHAURI UUZE KIWANJA. TAMBUA BADO UPO KTK STATUS NZURI.

Usiangalie ulipotoka, angalia inapokwenda.



Huenda na ww kimahesabu hauko vyema..take home anachukua 220k..hujanunua mchele..unga mafuta mkaa gesi .humo huml nauli ya watot shule km ni school bus..humo hmo aende saluni..hebu waza tena
 
Nahisi nikiacha kazi nitapata msukumo wa kujua Cha kufanya
Kazini napoteza muda tu kiukwel
Nina mpango wa kufungua kampuni,nishaandaa Hadi momerandum,nahangaikia kuisajil tu
Then nijitose,huenda nikikosa hata hiyo 220k nitapata akil Zaid na hasira ya kufanya vizuri zaid
Kabla ya yote niambie FANI YAKO NI IPI na "nite business" uliyokusudia ni ipi.
Trust me utaupenda ushauri wangu.
 
Mamii...nakuelewa sana...tena mno..hivi mm hapa niko kwenye mchakato wa kumshauri Mr ateme kazi ..mmepishana kidogo sana...yaan mm alifika kipindi akawa anakopa CRDB ile akipata mshahara wanafyeka chao then anakopa tena ya mwezi...

Acha woga...hapo shoga utapiga marktime za kufa mtu..hebu ufuate ushauri wa@Khan..!tena bora ww..kamaliza Msc 2012 ila mpk leo hajaanza kulipwa..alafu alivyo ccm damu..ahhaa may mosi akaniambia dogo mie nahamia ACT..niongoze sala ya toba..jaman maisha ya wafanyakazi wa serikalin ni magumu mno mno nyie jaman...Kama unaweza njoo machimboni tupige hela!nw mtumishi wa serikali ukimtumia laki 1 Anakushukuru Mwezi mzima!
Kuna mikoa mingne nuksi tu kuishi..hela inapatikana kwa mbinde sana . hama huko njoo geita my dear jipe 8mths..tutakuita boss mama (weka hela pata mapesa)

na kama utahitaj kushikwa mikono nipo hapa..pole!
Asante sana
Tatizo watoto,ila nawaza ningekuwa Sina watoto zaman ningeacha kazi
Namshukuru kwa hawa vijana wangu ni baraka mno maishan mwangu,sikufuru ila Kuna wakati nawaza ningejua ningefanya kama wazungu kuzaa uzeeni
 
Mkuuu usijirushe ghorofani hali hii tunapitia wengi sana,kuwa mvumilivu,kama unaweza pika mandazi yapeleke dukani kwa muha na mangi
 
Back
Top Bottom