Nataka kuacha kazi .

Nataka kuacha kazi .

Asante sana
Tatizo watoto,ila nawaza ningekuwa Sina watoto zaman ningeacha kazi
Namshukuru kwa hawa vijana wangu ni baraka mno maishan mwangu,sikufuru ila Kuna wakati nawaza ningejua ningefanya kama wazungu kuzaa uzeeni

Hahaha..unahis huku hakuna shule nzuri..ni vile bad hujaamua...!kila la heri
 
Nahisi nikiacha kazi nitapata msukumo wa kujua Cha kufanya
Kazini napoteza muda tu kiukwel
Nina mpango wa kufungua kampuni,nishaandaa Hadi momerandum,nahangaikia kuisajil tu
Then nijitose,huenda nikikosa hata hiyo 220k nitapata akil Zaid na hasira ya kufanya vizuri zaid
Wakati unahangaika hiyo kampuni isimame utakuwa unaishi vipi ?

Building a company from scratch ain't something that easy.

Na usijidanganye kujilipua ki-bahati nasibu, wanao wataomba mikate barabarani.

Smart people always take calculated risks.

Usijidanganye kabisa, hata duka tu huwezi kufungua leo na ukalitegemea kuishi- LITAKUFA.

Relax. Be wise !
 
Pole sana! Unaishi wapi? Kiwanja unauza bei gani?

Usiache kazi! Anza na kubadili life style kwa muda wa mpito. Kwanza wapeleke watoto shule za kawaida (Kayumba).

Kuhusu kuhamia kwako unaweza kuhamia kwa gharama isiyozidi laki 3. Kwa kufanya yafuatayo. Uweke tofali kozi mbili mbele ya chumba kimoja ktk hyo nyumba yako. Halafu uwezeke kwa milunda, ambapo mlunda mmoja nielfu 3 . Chumba kimoja hutotumia zaidi ya milunda kumi na bati kama 6.
Kama utakuwa interested nitafute leo tushauriane namna rahisi ya kuhamia kwako.

Tambua hayo ni mapito tu. Kama wataka kuuza kiwanja uuza kimoja tu. Ila ningekuwa mimi kwa mshahara huo na watoto hao Nisingeuza. SIKUSHAURI UUZE KIWANJA. TAMBUA BADO UPO KTK STATUS NZURI.

Usiangalie ulipotoka, angalia inapokwenda.
Kiwanja ni mil 8,ila kiuhalisia Bei yake ni mil 15 hadi 12
Niko dsm hapa wanapojenga barabara ya njia 8, lifestyle nishabadil kitambo tatizo Kila leo afadhal ya jana
 
Vumilia ndugu yangu kamwe usikate tamaa muombe sana mungu ipo siku atajibu maombi yako
 
Habari za asubuhi wana jukwaa.

Mie ni mtumishi wa umma na niliajiriwa mwaka 2013.Nina watoto wawili wa kiume,Nina viwanja vitatu ambapo kimoja nimejenga nyumba iliyoishia kwenye linta.

Toka aingie mkulu maisha yamekuwa magumu Sana,si furahii kazi yangu hata kidogo naenda tu kazini kuonekana nipo.Na siyo kuwa ni mpiga madili Wala,zamani tulikuwa tunapata hata viextra duty vinatuboost mwezi unaisha,ila saivi Nina mwaka wa tatu siijui posho.Tulikuwa tunaenda kazini hadi jmos angalau tupate chochote tulishe family.

Nimejaribu kuuza kiwanja kimoja at least nimalizie nyumba nihamie,manake Kodi inanitesa Sana huku nilikopanga ila nimekosa mteja.wanangu wanasoma mmoja baby class na mwingine class one.Bado mfanyakazi kumlipa hapo hujasaidia ndugu wanao ona nalipwa mamilioni ilihali mwisho wa mwezi napokea laki mbili na ishirini(220,000) ambayo haikidhi mahitaj yote.

Am a single parent kwahiyo mimi ndiyo baba na mama kwa wanangu.Baba yao tuliachana akaoa,na alitaka wachukua watoto ila sikuwa tayari kuacha wanangu wa under 7 years walelewe na mama wa kambo,hivyo kawasusa hatoi hata Senti tano kwaajili yao,so am their only hope.

Naona napoteza muda,nimeshafikiria hata kujirusha ghorofan ili nitoweke duniani ila nikiwafikiria wanangu roho inauma naona sitawatendea haki.So nimewaza nikaona si bora niache kazi,niuze Kila nilichonacho ingawa wateja wanakuwa tabu,nihame mji,nende sehemu nyingine nikaanze upya.Nimewaza pia kufanya nite business at least watoto wale na nipate Kodi ya nyumba,sema dhamira inakataa.

Mkuu hata Kama tulikuudhi tusamehe,tunadhalilika na familia zinateseka.Binafsi sioni faida ya kuitwa mtumishi wa umma ilhali Kuna wakati nakosa hadi nauli ya daladala kwenda kazini.Pia toka nimeajiriwa sijawahi panda cheo.

Naombeni ushauri wadau nifanyeje?je niache kazi?then niende wapi ama nifanye Nini baada ya kuacha kazi,Ningekuwa Sina watoto ningeshaondoka kitambo,tatizo mustakabali wa maisha ya wanangu utakuwaje,nikiwaza Hilo nachoka,naishia kumwaga machozi kama mtoto.

Hivi mtu unamaliza shule unaenda kuajiriwa na SERIKALI?

Hakuna majitu dhalimu na system dhalimu dunia hii kama kitu kinachoitwa SERIKALI!

Ni dude linaloendeshwa kwa matakwa ya wanasiasa!

It is a murder engine!
 
Wakati wengine wanatafuta ajira wengine wanataka kuacha, uza kiwanja kimoja malizia nyumba na kazi usiache
 
Kwani shida iko wapi unalipwa mshahara ambao huufanyii kazi effectively? Unafika ofcn unacheza gemu kwa komputa mwisho wa mwezi unaenda ATM kutoa mshiko, shida iko wapi?
 
Hivi mtu unamaliza shule unaenda kuajiriwa na SERIKALI?

Hakuna majitu dhalimu na system dhalimu dunia hii kama kitu kinachoitwa SERIKALI!

Ni dude linaloendeshwa kwa matakwa ya wanasiasa!

It is a murder engine!



Ni vile nchi yetu maskini tu..mie mdogo wangu anasema anajuta hata kupeleka cv huko...ovyo sana...alafu watumishi wamekuwa wanyoooongeee..tena mwez huu qwngine mshahara umechelewa sana sana kutoka..shenzy kbs
 
Back
Top Bottom