mkuu malila nami nahitaji shamba hasa msata na miono. naomba uni pm tafadhali
Kwa eka moja ilikuwa Tsh 50,000/ kwa eka, juzi nilisikia imepanda mpaka 80,000/ kwa eka. Naamini baada ya hawa jamaa kutoka mashariki ya kati kuvamia itakuwa inacheza kwenye laki moja hivi.
Nikirudi Dar mwisho wa mwaka tutafutane tukatembee mitaa ya kule.
Asante Malila una contact za mtu hapo Madesa? Hao wafugaji vipi sio wasumbufu? Eka moja inauzwaje? Leo nimetembelea wenzangu wa Kiwangwa eka inafika 1.2ml sio muda ardhi itakuwa haishikiki.
wakuu natafuta shamba la kununua lenye ukubwa usiopungua hekari 30, kwa ajili ya project yangu ya kilimo mwaka ujao ninayotegemea kuifanya nje kidogo ya jiji la dar es salam, shamba hilo naomba liwe na sifa zifuataazo:
- liwe na ardhi yenye rutuba kwa ajili ya kilimo hususani mahindi
- liwe eneo lenye water-table iliyo karibu, eneo ambalo nikichimmba kisima cha ku-drill nitapata uhakika wa maji kuanzia lita 5,000 kwa siku, na iwe ni kwa mwaka mzima.
- liwe pembezoni mwa mji lakini umbali usizidi km 50 kutoka dar es salaam.
- liwe linafikika kwa urahisi kwa gari kwa ajili ya kusafirisha mazao yangu kutoka shambani
- uwepo wa umeme japo si muhimu sana
kwa mwenye kuwa nalo au yeyote mwenye kuuza naomba tuwasiliane hapa au kwa pm hususani kwa mambo kama bei, vibali na location.
Natanguliza shukrani
Mkuu hapajajaa huko? kama bado niinbox namba ya dogo tafadhaliLeo nilikwenda Buyuni, ndani ya kata ya Vigwaza ktk jimbo la mkuu Kawambwa, ni km 9 toka Vigwaza barabara ya Chalinze unaingia ndani kulia kwako kama waenda Chalinze. Kule kuna land ya uhakika kwa kilimo cha Pwani na ufugaji. Kwa sasa maji ya bomba yamefikishwa yanasubiri wanasiasa kukata utepe.
Pana ardhi nzuri ya kilimo ( Mahindi,mihogo,ufuta,mtama,viazi,korosho,kuna jamaa ameanzisha ufugaji wa nyuki kisasa, inatia raha, kuna mifugo pia, bado wananchi wa Buyuni ni Watz aliowaacha Nyerere. Nchi ni safi na natural kabisa. Kwa wanaopenda mitaa hii ya Buyuni karibu na Ruvu basi tuwasiliane. Mimi sio dalali, nakupa simu ya dogo anayetuunganishia sisi, kila kitu ofisini kuanzia ngazi ya Kitongoji.
Kuna 29 acres pale Viazi, less than 30 km from Dar city centre. lina sifa zote. Except umeme unahitaji bidii kidogo
Watu wa JF wananishangazaga sana kwenye issue za biashara, mtu anaweka details nusu nusu ili umuombe au umbembeleze roho yake isuuzike kuombwa.
Hii yote ni sababu ya Umwinyi.Ni sawa na jamaa wanaotoa hela kumpa mtu mpaka abembelezwe na kupigiwa magoti ama kusifiwa sana ndio umchomoe mtonyo.Ni shida sana.
Nauza heka tano, Morogoro Sehemu inaitwa Njovu, wilaya ya mvomerohabari mpya za mashamba tupeni mliokuwa updated. za bei rahisi au mapori ya bei Che .
Kila heka ni milioni moja tu, ni shamba zuri sanahabari mpya za mashamba tupeni mliokuwa updated. za bei rahisi au mapori ya bei Che .
Muwe mnaweka na beiMkuu. ni tafute kwa namba hii 0758144703..shamba liko kijaka kimbiji ni ekari 34..katkati kuna mto unapita maji yake hayakauki majira yote.karibu sana.hakuna udalali.