Natafuta kibarua

Natafuta kibarua

A.Abdon

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2013
Posts
217
Reaction score
38
Wadau wa humu ndani hodi hodi

Mimi ni mwanaume wa miaka 29 sina mke wa mtoto.Tatizo langu kubwa sins kibarua cha kunipatia kipato kwa sasa.Nina elimu ya degree ya Social Science .Kwa yeyote mwenye Upendo nahitaji anilink au anisaidie nipate kibarua hakika nimeapply sana but nahitwa kwa interview cpati ajira sijui kwanini.

Nimejaribu kufanya bishara mambo hayaendi mara mbili biashara imekata najaribu kuomba kazi now napo kimya.Right now am broke na hata Pesa ya kuendesha maisha yangu ni shida pambo la nilipopanga linaisha this month hakika no majanga sijui tatizo langu nini hakika moyo waniuma sana ndugu zangu.

Nachoweza sema nahitaji msaada wenu wa halo wa Mali nipate ajira wadau nami nikae poa. Nitashukuru kama yoyote atanisaidia katika hili.please pm me kwa more talk na kma umeguswa.

Nawasilisha.
 
Pole ndugu(tatizo la ajira linatukabili wengi),mie ningependa kukushauri ukawaone watumishi wa Mungu kwa maombi au dhamiria kufunga na kusali maana Mungu yu mwema atafanya njia tu.
 
Ushauri mzuri ndugu thank you nitaufanyia kazi .Ubarkiwe
 
Pole ndugu(tatizo la ajira linatukabili wengi),mie ningependa kukushauri ukawaone watumishi wa Mungu kwa maombi au dhamiria kufunga na kusali maana Mungu yu mwema atafanya njia tu.

Umenena vyema sana. Nina masters lakn nilihangaika sana kupata kazi. Nilimuona mtumishi wa Mungu tuliomba kwa muda wa masaa matatu. Kuna nguvu za giza zilinifunga. Huwez amini baada ya yale maombi siku ile KESHO yake kuna sehemu nilikua napiga deiwaka wakaniambia niandike barua waniajiri. Kuna kitu katika ulimwengu wa roho kinachokua kinafunga maisha yako pasipo kujua. Mtoa mada nakushauri ingia kwenye maombi au muone mpakwa mafuta ya BWANA muombe pamoja njia yako itafunguka. Hata mm nilikua nafanya interview lakn kazi sipati. Baada ya maombi next day tu nikapata ajira. Mungu aliyenikumbuka mimi akukumbuke na wewe mleta uzi.
 
Pole sana..inaonyesha hzo biashara zako hauzifanyi kitaalamu mkuu?
 
Mwakasege anafanya semina ya maombezi kuanzia Ijumaa hadi Jumapili viwanja vya jangwani, nakushauri twende wote. Tumtumaini Mungu kwa kila jambo.
 
Maombi kwanza, mengine yanafuata......biblia inasema utafuteni kwanza ufalme wake ndipo hayo yote mtazidishiwa....amen..
 
Pole sana kaka na hizo changamoto zinazokukabili kingine cha msingi kufanya maombi unaweza kushirikisha familia ikusaidie kwenye maombi kabla haujaenda kwenye any interview pili fanya tafiti katika kila interview unayoitwa wanaulizaje maswali yao hata kwa kutafuta mtu anayefanya kazi huko kwenye hiyo kampuni au hapa jukwaani I wish mambo yatakunyookea kaka all the best
 
Mmmmh kaka maombi? Unadhani Mungu anahitaji wenyeshida ndio awasaidie? Mungu anachukia kuombwa ombwa ila anapenda kushukuliwa kwanza ukienda kuombewa kashukuru kwa uhai ulio nao na elim uliyo nayo baada ya mwez mmoja Wa shukran sasa ndio uombe. Lakin unatatizo haiwezekani uitwe interview then ukose Kazi utakua hujui kitu au unajua lakin hujiamini maana ndio shida zenu wana vyuo kutokujiamini na kua hamjui chochote kwa uzembewenu Wa kusoma kufaulu sio kusoma kuchapa Kazi
Ila sahau kuhusu kulogwa hujalogwa wala nini ... na familia kua makini kuwashirikisha kama ni wazee usiwashirikishe kwasababu utawaumiza tuu kwa mawazo kwa hela walizowekeza kwako
Biashara nenda kwa washauri Wa biashara watakusaidia... asante
 
Mmmmh kaka maombi? Unadhani Mungu anahitaji wenyeshida ndio awasaidie? Mungu anachukia kuombwa ombwa ila anapenda kushukuliwa kwanza ukienda kuombewa kashukuru kwa uhai ulio nao na elim uliyo nayo baada ya mwez mmoja Wa shukran sasa ndio uombe. Lakin unatatizo haiwezekani uitwe interview then ukose Kazi utakua hujui kitu au unajua lakin hujiamini maana ndio shida zenu wana vyuo kutokujiamini na kua hamjui chochote kwa uzembewenu Wa kusoma kufaulu sio kusoma kuchapa Kazi
Ila sahau kuhusu kulogwa hujalogwa wala nini ... na familia kua makini kuwashirikisha kama ni wazee usiwashirikishe kwasababu utawaumiza tuu kwa mawazo kwa hela walizowekeza kwako
Biashara nenda kwa washauri Wa biashara watakusaidia... asante

naiman umepata kitu kwa wadau hapo juu
 
Baada ya maombi (ambayo ni nonstop) unatakiwa ufanye kwa vitendo sasa, na mimi nakushauri zungukia NGO uombe ku volunteer. Ingia Google tafuta NGO in Tanzania utapata nyingi sana. Najua kuna kuwa na contact zao tuma email yenye Cv yako utapata tu. Ila usimsahau Mungu kwa namna yoyote Ile. Hasa kutubu kila siku
 
Mshirikishe mungu kwanza...Mshukuru kwa kila jambo na yote aliyokujalia....then fanya maombi...onana na mtumishi wa mungu kwa ajili ya maombi..huwezi amini binadamu huwa tunafungwa na mambo mengi ni kazi ya shetani...mimi ni shuhuda wa haya pia...ushuhuda wa karibu ni wiki iliyopita, biashara zangu zilikwama na nilihitaji kiasi cha hela .....nilimuomba mtumishi tufanye maombi nyumbani kwangu na familia yangu tukiwa na partner wangu wa biashara..na tukapata upako siku ya jpili 13 Sept......siku iliyofuata jtatu 14 Sept asubuhi nimepigiwa simu mbili za kibiashara toka kwa watu nisiotegemea kabisa!!!!ingawa sijakamata hela mpaka hivi sasa lakini niko kwenye hatua za mwisho kupata nilichokiomba....Mungu anaweza.....Mungu ni Mwema!!!Imani yako itakuponya!!
 
Ahsanteni SNA wadau maoni yenu ni mazuri sana nitayafanyia kazi hakika.
 
Pole sana ndugu yangu omba sana...ijumaa jangwani kwa mtumishi mwakasege inakuhusu nenda
 
Mwakasege anafanya semina ya maombezi kuanzia Ijumaa hadi Jumapili viwanja vya jangwani, nakushauri twende wote. Tumtumaini Mungu kwa kila jambo.

Ushauri mzuri sana huu,ufanyie kazi mkuu na Mungu atajibu maombi yako
 
kweli maombi ndo kila kitu, nilikua sina kazi pia ila nilimkabithi mungu akaniona na kunipatia kazi pia' Mungu ni mwema ukiomba kwa imani mkuu
 
Kazurikazuri ijumaa kesho kwa Mwakasege sio.
 
Unajua sometime nashindwa elewa nimefanya biashara mingo za Pesa mingo kidogo had I kifungua kikampuni nimefanya hadi network marketingi.Nimeapply job mpka mwisho nimeapply scholarship kibao nimesoma hadi ILETS pale British Council.Cpati support kutoka kwa MTU yyote ndugu zangu wa frnd hakuna anaejua Nikipi kinanisibu wote hawapo nami am alone.kila naemwambia jambo awaresponde kwangu always they assume kwamba Mimi nipo vizuri ndio kwanza naombwa Pesa.why me?
 
Wadau wa humu ndani hodi hodi

Mimi ni mwanaume wa miaka 29 sina mke wa mtoto.Tatizo langu kubwa sins kibarua cha kunipatia kipato kwa sasa.Nina elimu ya degree ya Social Science .Kwa yeyote mwenye Upendo nahitaji anilink au anisaidie nipate kibarua hakika nimeapply sana but nahitwa kwa interview cpati ajira sijui kwanini.

Nimejaribu kufanya bishara mambo hayaendi mara mbili biashara imekata najaribu kuomba kazi now napo kimya.Right now am broke na hata Pesa ya kuendesha maisha yangu ni shida pambo la nilipopanga linaisha this month hakika no majanga sijui tatizo langu nini hakika moyo waniuma sana ndugu zangu.

Nachoweza sema nahitaji msaada wenu wa halo wa Mali nipate ajira wadau nami nikae poa. Nitashukuru kama yoyote atanisaidia katika hili.please pm me kwa more talk na kma umeguswa.

Nawasilisha.

Nenda kafanyiwe maombi mkuu, huenda kwenye ukoo wenu kula roho ya kutokufanikiwa au roho ya kutokukubalika popote pale, sasa itakuwa inakuandama, jaribu kuwafata watumishi wa mungu wakuombee wavunje laana za mababu au nguvu zote za shetani zinazokuandama, kwa mungu hakuna kinachoshindikana.

Pia unaweza ukawa unafanya biashara hazifanikiwi kwa kuwa tu wewe mawazo yako yapo kwenye kuajiriwa na sio kujiajir au huenda huipendo hiyo biashara unayoifanya, ni vizur ukatafuta biashara unayoipenda wewe
 
swali la kizushi. hivi na application letters, resumes, written interviews unaandika kwa style hii?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom