Nasumbuliwa na Shahidi wa Yehova

Nasumbuliwa na Shahidi wa Yehova

Bujibuji Simba Nyamaume

Platinum Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
78,144
Reaction score
166,082
Huyu jamaa alikuwa akinipigia simu kila siku usiku na kutaka nihamie kanisani kwao. Nimemkataza kunipigia, kwa kweli ameacha, lakini namba yangu nahisi kaigawa kanisa zima, maana napigiwa simu hadi na watoto wakinitaka nihamie huko kanisani kwao.
Kwasiku napokea simu zisizo na idadi.
 
Nenda kawasikilize then utaamua. Uzuri ni kwamba ukiwaambia huna usafiri wa kuja church watakupatia ride/lift kwenda na kurudi ama hata kukukodishia taxi, na msosi huko ni free
 
Huo ni ujumbe wa Mungu sio usumbufu, itafika siku utatamani upate ujumbe huo. Nenda kawasikilize,kisha waambie msimamo wako basi.
 
hata me naungana na wa2 waliopita nenda kawasikilize then utaamua na mungu akusaidie.
 
kha watu wagumu na maneno ya mungu...kwani wanatumia muda gani kuongea na wewe kama si dk 15 na unafaidika
 
Kumbukumbu zangu kwenye Biblia sijaona mahali Yesu alikuwa analazimisha watu kumfuata...
Na msafara wake ulikuwa hauishi watu, kwa sababu matendo yake na mafundisho yake pekee yalijitosheleza kuvuta umati wa watu..
Sasa iweje hawa walokole hawafuati mfano wa Yesu na kuacha watu waamue wenyewe kuwafuata baada ya kuona miujiza yao?
Ina maana hawajiamini mpaka wajitangaze redioni na kwa kupigia watu simu??
 
Kumbukumbu zangu kwenye Biblia sijaona mahali Yesu alikuwa analazimisha watu kumfuata...
Na msafara wake ulikuwa hauishi watu, kwa sababu matendo yake na mafundisho yake pekee yalijitosheleza kuvuta umati wa watu..
Sasa iweje hawa walokole hawafuati mfano wa Yesu na kuacha watu waamue wenyewe kuwafuata baada ya kuona miujiza yao?
Ina maana hawajiamini mpaka wajitangaze redioni na kwa kupigia watu simu??
Mashahidi wa yehova sio walokole.
 
Kumbukumbu zangu kwenye Biblia sijaona mahali Yesu alikuwa analazimisha watu kumfuata...
Na msafara wake ulikuwa hauishi watu, kwa sababu matendo yake na mafundisho yake pekee yalijitosheleza kuvuta umati wa watu..
Sasa iweje hawa walokole hawafuati mfano wa Yesu na kuacha watu waamue wenyewe kuwafuata baada ya kuona miujiza yao?
Ina maana hawajiamini mpaka wajitangaze redioni na kwa kupigia watu simu??
haya baba paroko
 
Huyu jamaa alikuwa akinipigia simu kila siku usiku na kutaka nihamie kanisani kwao. Nimemkataza kunipigia, kwa kweli ameacha, lakini namba yangu nahisi kaigawa kanisa zima, maana napigiwa simu hadi na watoto wakinitaka nihamie huko kanisani kwao.
Kwasiku napokea simu zisizo na idadi.
Pole. Sijui hadi sasa unaabudu wapi au u dhehebu gani. Maana kama ni mkristo jamaa wana mafundisho tata kwelikweli tena ya kubumba hadi kuichakachua hata Biblia!
 
Pole. Sijui hadi sasa unaabudu wapi au u dhehebu gani. Maana kama ni mkristo jamaa wana mafundisho tata kwelikweli tena ya kubumba hadi kuichakachua hata Biblia!
Hawa jamaa ni noma, yaani wana Biblia yao iko tofauti kabisa na Biblia za kawaida, ni wapinga Kristo ni bora kutowasikiliza kabisa.
 
hawa jamaa wana moyo sana wa kushuhudia na kukaribusha watu ktk ibada zao, yaani ukushahudhuria kanisani kwao ni kosa kila siku ya ibada watakutafuta popote pale hawataki kupoteza kondoo hapo kuna mawili either ulikuwa mshirika pale umekengeuka so wanakurudisha kundini or ulishawahi kuabudu nao au ulipromise kuwa nao
 
Huyu jamaa alikuwa akinipigia simu kila siku usiku na kutaka nihamie kanisani kwao. Nimemkataza kunipigia, kwa kweli ameacha, lakini namba yangu nahisi kaigawa kanisa zima, maana napigiwa simu hadi na watoto wakinitaka nihamie huko kanisani kwao.Kwasiku napokea simu zisizo na idadi.
Mashahidi wa Yehova hawalazimishi mtu kwenda kwenda kwenye ibada zao au kuwa Mmoja wa waumini wao utaratibu huo haupo kwani kuwa Shahidi wa Yehova na kuhudhuria ibada nilazima ujifunze mambo kadhaa ya msingi kupitia home Bible study na unaweza kuwa na hii home Bible study huku ukiendelea na imani yako na hawata kulazimisha kuacha mpaka hapo wewe utakapokuwa umeweza kutofautisha uliko wewe na upande wa Mashaidi then kwa hiyari yako utachangua ipi ni njia na hiyo ndiyo falsafa yao. Na wao hudeal na wale wanaonyesha interest na belives zao. Sasa ikiwa wanakulazimasha inawezekana wewe ulipendezwa awali ukanza kujifunza sasa inawezekana hupendezwi tena,
 
Hawa jamaa ni noma, yaani wana Biblia yao iko tofauti kabisa na Biblia za kawaida, ni wapinga Kristo ni bora kutowasikiliza kabisa.
Nimewahi ona bible wanayotumia ina kitabu kinaitwa SILAS, ambacho kilikataliwa kisiingizwe ktk Biblia takatifu.
 
mafundisho yao utata mtupi, wanakataza hata kumuongezea damu mgonjwa, siwataki.

Mafunsidho yao ni ya uongo. Hawafundishi sawasawa na Biblia. Kwa mfano wanadai hakuna mbingu mpya ila ni hapa tu duniani yale majumba mazuri mazuri ndo watakaa humo. Usithubutu kwenda huko maana kama huna nguvu ya Kiungu katika ulimwengu usiionekana utaenda ukapandikizwe mapepo huko.
 
jamani kuna mwenye kuwafahamu hawa wanaojiita THE BOOK OF MORMON maana nna kama miezi miwili wananipiga darasa mpaka nahisi kama navutika nao,nsijeingia choo cha kiume buree
 
Back
Top Bottom